Alhamisi, 28 Julai 2016

De 6

Gangstar noma
By: benchrys
6
Madam umee   ese  ma nikungoje niliuliza kwa kigugumizi swali hilo kwa madam linda mana nilihisi huyu pengine ndio anataka atimize lengo lake la kulazimisha apajue nyumbani ili awape wazazi ukweli wote juu ya mambo ambayo nayafanya huko shule l..mimi nikiwa nawaza hayo joel nae alikuwa akiningoja kwasababu tulishapigiana simu kuwa siyo mida mingi ntakuwa nishafika kwao mana siyo mbali sana kutoka pale sisi nyumba yetu ilipo nikiwa nimesimama huku nikiendelea kumngoja yule madam mara simu yangu ikaanza kuita ngrrrrr ngrrrrrr nikainyanyua na kuipokea nikijua wazi kwamba huyu atakuwa ni joel anataka kuulizia mbona nachelewa kufika hivo lahaula kumbe hakuwa joel niligundua hilo jambo baada ya kuipokea ile simu na kuanza kuongea.....hallo vipi jo...kabla sijamalizia kusema joel ili nikamilishe kusema hilo jina nikazuiliwa kuendelea kuongea na sauti ambayo niligundua kabisa hii siyo sauti ya joel mana ilikuwa ni sauti ya mkwaruzo tena kavu kama ambae chai yake ni kokoto au anashindia bangi tuu kila siku ndipo aendelee kuongea....
   Oya mdogo wangu upo wap saizi ninamishe na wewe kama upo tayari tukutane ili tuchonge mipango yote iende fresh,,,,,,,,mbona hunijibu au hujanisikia. Sikujibu nilibakia kimya bila kujibu chochote hapo ndipo akili yangu kidogo iruke maana huyu madam madam kanambia nimngoje halafu kibaya hadi saivi hatokei nikiondoka itaonekana ninadharauu na tena nikabaki hapa kisha nije kukutana na majanga tena mana aliyepiga hii simu simjui na shida yake nini..hayo yalikuwa ni mawazo ambayo yalianza kusumbua sasa kichwa changu uchaguzi ni wangu huu niepuke kipi na nikiache kipi duh.. Nionekane namdharau ticha au nimpuuzie joel au nimpuuze aliyepiga hii simu Nilkuwa katika wakati mgumu kulingana na jambo lililo....licha ya kuwa ticha ataniadhibu ila hakitaharibika kitu chochote ila kwa huyu boya ambae simjui lazima anaweza kuwa ni mpuuzi yule alitemteka yule bint mbona sauti zao kama zinalingana hivi anaweza kuwa anajua niliko mahali salama hapa ni homu tuu...nilikuwa nayafikilia hayo ndipo nkachukua uamuzi wa kuondoka pale tena kwa haraka lakini nikiwa nimetoa hatua kama tano hivi ilisikika sauti ya kike tena nadhani alikuwa ni madam linda nikiwa na haraka kama mtu mwenye safari halafu kakumbuka kuwa amesahau nauli na gari mda wa kupita unakaribia,,,nikageuka kumbe ni kweli alikuwa madam
   Mbona unakimbia huku nmekwambia uningoje hapa kuna tatizo lolote. Muda hio yeye anaongea hayo nlikuwa nikimwangalia tuu na kubaki kimya bila kujibu lolote mawazo niliyokuwa nayo kama yule aliyepiga simu yupo jilan itakuwa matatizo kama sio kwangu basi madam anaweza kudhurika nae maana mwenye roho mbaya haangalii nani ni wakumdhuru, nikamwambia madam samahan tutaongea kesho shuleni ndio ntakupa full mkanda jinsi ilivo na ndio maana unaona hapa nnaharaka kama ivi. Sikutaka kupewa hata ruhusa nikasema madam wahi nyumbani muda m baya huu kisha nikaondoka huku nikiwa nakimbia kama nimetumwa nikakomboe hazina mahali,, mda mfupi nikawa tayari nishafika nyumbani niliingia ndani nikiwa nahema kama mtu aliyepona kunyakuliwa na tai
Nikiwa nyumbani hata sijapumzika simu yangu ikaanza kuita niliipuuzia sikutaka kuangalia hata jina la anaepiga simu huo mda...we ben inamaana hiyo simu inayoita siyo yako au...naomiiiiiii we naomiii.ilikuwa ni sauti ya mama akimwita naomi, mimi nikauliza mama inamaana naomi bado yupo hapa hadi leo tena mda huu. Mana nilijua atakuwa tayari amesharudi kwao mama akanijibu kwani kunatatizo? Ndio mi naona ni tatizo inamaana wazazi wake watakuwa hawamtafuti tuu mi naona tutakuwa tunawasumbua tuu,,mama akasema we mwanangu usiwaze kuhusu hilo tulishaongea kwamba ataishi hapahapa maana yupo likizo isitoshe baba yako kakubali na mimi pia nimekubali.. Hapo ndipo na mimi baada ya kupewa hilo jibu nikaenda kuichukua simu yangu iliniangalie ni nani alikuwa anapiga, nilipoangalia nikaona namba ngeni nikajisemea atakuwa yule mpuuzi ila nikaona tena kuna meseji imepokelewa nikaifungua kutaka niisome namba iliyoituma ile meseji haikuwa na jina kwamaana ni namba ngeni nikaendelea kufungua hapo ndipo nikauona ujumbe USIJE UKAOGOPA....nikiwa naendelea kusoma ile meseji nikaitwa beeeeen alikuwa mama akiniita tena akisisitiza nifanye haraka nikafanya kama alivomaanisha nikafika mahali alikuwa amesimama
Ben umeanza urafiki na vijana wahuni sio. Hapana, sasa inakuwaje hadi tunapata mashitaka ya namna hii.. Mbona mimi sina rafiki zaidi ya joel. Anhaa ndio mnazurura pamoja huyo joel eti, na kwanini we ni mwanafunzi harafu uwe na rafiki ambae sio mwanafunzi. Hapana joel tunasoma wote.....nilipojibu hivo nikatupa macho nje hapo nilishtuka na nikajua kwanini mama anauliza hivo ndipo nikamwambia kama ni huyo wa nje ndiye aliyetaka kumdhuru yule bint naomi,,,,,kwa sauti ya au tuseme mwizi maana huyu si mtu mwema, mama akasema subiri mimi namwondoa kwa aman tuu ila akileta ubishi ndipo ntatumia hiyo njia.
Samahani sana naomba tuu uondoke tena kwa amani mana ben hamjuani njia ile pale kama ni siku ya kudhurika kwa ben sio leo kwaheli eeee..aliongea hayo mama kwa yule jamaa. Huyo jamaa hakutaka kuleta ubishi akageuka na kuanza kuondoka lakini alipokuwa akishuka katika ngazi wote tulishtuka baada ya kuona akiwa bastola kiunoni, haraka nilipokea simu ya mama na kuchukua picha inayoonyesha ile bastola kiunoni...itandeleaaaaa

benchrys1996@gmail.com
&
benchrys.blogspot.com

Jumanne, 26 Julai 2016

de 5

Gangstar noma
By: benchrys
5
..kisha mnisubiri na mimi ntakuja na nataka mnipe maelezo ya kutosha ni upuuzi gani ambao nyie kabisa mnaruhusa ya kuongea ndani ya kipindi changu tena kwa. Msiniletee zogo hata kidogo maana mtakuwa mnaniongezea tu hasira hapa we ben unataka kusema nini. Madam alifoka baada ya mimi kutaka kujitetea hapo nikajisemea kuwa daha siku yangu ishaanza kuwa mbaya ni bora nisinge kuja hapa shuleni hii leo mbona naanza kukutana na majanga asubuhisubuhi tuu aah,,,nilikuwa tayari nishapata hasira licha ya kuwa nilishamsamehe m baya wangu ambae ni jane nilijihisi kama hasira zangu juu yake kama zinaanza kurudi tena
     Tukiwa tumeshakaa kule ofisini zaidi ya dakika kumi na tano hivi mara mlango ukafunguliwa tena kwa nguvu kumbe alikuwa ni madam alishindwa kuuhimili ule mlango aufungue taratibu kwasababu alikuwa kachukua vitabu na madaftari mengi mimi kwa akiliyangu ya kipuuzi nilitaka kusahau kama nipo kwenye majanga nikataka niangue bonge la kicheko maana nshazoeaga joke/ matani kwa lugha ya weneyewe wanasema ila nshukuru nilishtuka nikajibanza kimya wakati huo jane alikuw ameenda kwa madam na kumpokea baadhi ya madaftari mana madam alikuwa katika wakati mgumu angeshindwa kuyatua yale madaftari na matokeo yake angeyaangusha na baadhi yange anguka.
      Jane nakushukuru hata kama tabia yako sijaipenda hata mara moja kumbe kwenye ukarimu upo vyema nadhani haya madaftari nitayasahihisha badae saizi naomba kwanza kaeni hapo kwenye kiti,,alisema hayo maneno madam Linda, Linda ni jina ambalo wanafunzi wote walikuwa wakilifahamu tangu madam huyo alipojitambulisha kwa wanafunzi wote licha ya kuwa kuna baadhi ya wanafunzi walishampa jina la maneno mengi mana alikuwa akiamua hiyo siku yeye ni kuongea mambo hata mengine huyataki basi itabidi uvunge tuu na yeye kumtuliza mtu mwenye maneno mengi hakuwa anaona shida sijui katokea mkoa gani huyu mana ni mwongeaji mno
****huko nyumbani nako walikuwa wakijadili naomi - huyu beni leo atakuwa kapokea kichapo nini mana kwa jinsi alivo chelewa na nasikia kuna mwalimu wao ni mgeni na mpenda sifa kweli akiamua kukupakazia kosa hata kama huna nilazima utakubali tuu labda wewe uwe ni m bishi sana sijui kama leo kweli atapona aliongea maneno hayo naomi alikuwa kakaa na mama akimsaidia kuosha vyombo mana hadi mda huo alikuwa hajarudi kwao,, mama akema kama alichelewa alitegemea nini itabidi akubaliane tuu na hiyo adhabu. Naomi alimtazama mama kisha akaendelea na kuosha vyombo huku akisema kama ni kuchelewa kuamka ni bahati mbaya tuu
****beni na jane wakiwa darasani sijui wamemalizeje hiyo kesi yao huko ofisini
Oya huyo madam wenu mbona mnoko sana. Aliuliza joel mi sikujibu neno lolote akiwa anataka aendelee kuongea mara god nae akaingia joel na ben mnaitwa na madam.joel akauliza madam nani huyo, madam linda alijibu god tukiwa tunataka kumfuata jane akasema ben usiende huko huu mda bora uonekane mkaidi tuu.. hapo mimi nikajiuliza nisiende kwa nini au kuna jambo anajua roho ya kumsikiliza ikaanza kujileta pengine anaweza kuwa msaada.. oya joel ee mi saivi huko siendi wewe nenda ukamsikilize tuu akikwambia uniite mwambie sipo vizuri nilipomwambia hivo nikainamiana kwenye meza yangu ili nijisingizie kichwa kinanigonga,,Joel akaondoka kwenda kwa madam sio mda kidogo akarudi kakunja uso mimi sikutaka kunyanyuka nimwone licha ya kuwa nilimwona kupitia upenyo wa sweta nililolivaa..niliinamiana hadi unafika mda wa kurudi nyumbani, ulipofika ma wa kurudi nyumbani jane akanifwata tena kwa spidi na kusema leo tunaenda wote hadi kwenu nikamuone dada angu mana nishammisi ghafla mimi nikicheki yule madam yupo mbele yetu anatucheki kwa wizi wizi sikujali nikajisemea bora majanga yaishe tuu nisije maliza hili wiki vibaya nikamwambia jane mi ndio naondoka hivi kama vipi twende mana najua lazima atakuwa bado yupo home tuu. Aa ningoje kwanza nikachukue mkoba wangu pale darasani nilisahau. Powa fanya fasta ukichelewa mm hunikuti,. Jane akaondka alipoondoka tuu nikaoana madam akija tena kwangu nikajisemea hapa nishaharibu kabisa
Ben nidhamu yako ipo chini sana ivi wazazi wako hawajawahi kukufunza kuwa inabidi kuheshimu wakubwa zako unapoitwa nao kwanini umeniagizia mtu mwingine aitike wakati mimi nilimtuma god akuite wewe na sio huyo joel ambae umemtuma? Nakuuliza mwenyewe!!!
Sikujibu maana sikuelewa jambo analoongea,,,,, ok naomba tuongozane hadi kwenu sawa ben. Nilipoona kasema hivo ndipo nikatoa sauti  ya kwamba madam hilo swala litakuwa gumu sana kama ni kuhusu nidham nitajirekebisha tuu,, jane alipoona nipo na madam alipita njia nyingine na kuondoka.
****nikiwa nyumbani nishakula tayari najiaandaa kuondoka kwenye misele yangu kama kawiada simu inaita.. oya ben uko wap, npo home jee, powa basi nakuwaitia hapa home au vipi, powa.. alikuwa ni joel
Nikiwa njiani kuelekea kwa akina joel mbele nikamuona yule madam yupo kimtaani zaidi kama siyo ticha  vile. Shikamoo madam, powa ben mzima alipojibu salam ile niliduwaa kama sekunde nikajibu mm mzima sijui wewe, kama unavoniona hivi ndio hivi mzima wapi safari aliuliza madam, nikajibu naenda dukani pale. Ahaa ningoje hapohapo..itaendelea

Benchrys1996@gmail.com
&
benchrys.blogspot.com