Jumapili, 11 Septemba 2016

De 28

Gangstar noma
By: benchrys
28

......merry aliyumbisha kichwa pembeni na kulala kitendo ambacho kilinifanya nisijue ni nini cha kufanya niliita kwa sauti #meriiii zaidi ya mara saba lakini sikuweza kuitikiwa kwa sauti yeyote nikajiuliza inamaana alikuwa anaumwa au mbona hivi..kiufupi sikuwa na jibu sahihi niliichukua simu yake ilinijue kama kuna namba yoyote ya dsktari ili aweze kuja atoe msaada kama ikiwezekana nilipochukua simu yake ilikuwa na lock za pattern hii too much nilinisemea mwenyewe baada ya kuona vile nikaamua niondoke ili niende hata kwa majirani pengine naweza pata msaada
Nilifungua mlango kisha nikatoka nje lakini kabla sijapiga hatua nyingi nilihisi nyuma yangu kama kuna kitu kimepita kwa mwendo wa haraka niligeuka na kurudi nyumbani ile nafika mlangoni nilisikia sauti ya mlango kubamizwa kabla ya kufungwa niliuwahi na kuingia ndani ndipo nilikutana na mtu ambae kwa kumwangalia alikuwa kajazia sana maeneo ya kifua, nae alipohisi nimeingia alicheka kwa dharau kisha akanigeukia lakini kwa kuwa babu alinipa staili nyingi za kupigana kule porini nilijua tu kuwa nae anataka anifanye mbabe pale. Baada ya kuniangalia na kucheka kwa dharau akanisogezea uso wake karibu na wangu akawa anaongea kwa sauti ya chini
""""dogo humu ndani kama ulikuja kuleta shobo zako leo hutoki humu ukiwa hai sitahitaji kujua wewe ni nani na huyu ni nani yako hayo unafahamu wewe mimi ilimradi nikamilishe kazi yangu kwa amani na usalama zaidi na ndio maana nikampulizia huyu ile dawa hadi amelala hivi na hapo hajielewi kabisa hebu njoo huku"""

Baada ya kumaliza kusema yale alinishika kwenye shati langu wenyewe mnaitaga t shirt sijui sana, baada ya kunishika vile alinisogeza hadi sehemu fulani ambayo ilikuwa na uwazi katika ile nyumba hapo ndipo aliniachilia ile t shirt yangu kisha akasema ngoja kazi nikuonyeshe sio swala la mda mrefu wait......kisha akaondoka ila mimi baada ya kuangalia niliona kwenye dirisha ambalo nipo jirani nalo hakuna nondo isitoshe lipo wazi ni kitendo cha haraka sana nilikwea lile dirisha na kuingia ndani kisha nikatokea chumba cha mery na kufika sebuleni muda huo kabla ya yule mbabe kuingia maana nilishajua dhumuni lake,,,,sikuzubaa nilimnyanyua merry na kumpeleka kule kwenye chumba cha siri kwenye ile nyumba kisha nikatoka haraka nikiwa na nguo maalumu za kung fu fighter kama masta fulani wa kichina nguo hizi nilipewa na babu kule porini

       Baada ya mda kidogo yule mbabe alikuwa akifungua mlango ili kuingia ndani. Nilijiandaa pindi aking'aza tuu sura yake ndani lazima ajute baada ya sekunde tu aliweza kuufungua mlango lakini alirudishwa nje alikotoka kwa mateke mawili mazito moja likitua kichwani na jingine kifuani......alitua nje kama peto la mtumba baada ya hapo na mimi nilinfuata huko nje nikiwa namngoja ili asimame tuoneshane

Alinyanyuka kwa hasira sana kisha akachomoa kisu mfukoni mwake na kuanza kunisigelea lakini kidume hata sikutishika hata kidogo nikabaki tu nimesimama huku nikimngoja ili nijue anachotaka kufanya nae bila woga alisogea akiwa katanguliza kile kisu chake.....aliponikaribia tuu aliongeza mwendo wake kunifikia lakini kabla hajafika nilichumpa juu na kujigeuza kama paka nilipokuwa natua chini kisu tayari kilikuwa mikononi mwangu nae kwakuwa alishakariri kuwa mimi boya kama wengine akajua hii ilikuwa bahati mbaya tuu akajipanga na kunisogelea tena kwa spidi ila kabla hajanifikia niliruka na kuzunguka mara tatu hewani kisha nikampiga mateke mawili ya uso hali iliyomfanya apepesuke kama mgonjwa wa maralia kali na kwenda chini kama kipeto kisichokuwa na maana sana mda wote huo mimi nilikuwa kimya kikazi zaidi
Baada ya kutua huko aKapata nguvu tena na kujivuta ili anisogelee tena nilimwangalia kisha nikafanya kama naondoka kuelekea getini nae ndipo akajua amepata wakati mzuri wa kunivaa kumbe nilimwekea kama mtego wa kumpeleka hadi kabisa ya nyumba ile___nilipiga hatua chache nae akawa kwa mwendo wake tayari yupo jirani na mimi, nilidunda katika ukuta wa pale jirani na geti akiwa hana hili wala lile nilitua moja kwa moja kwenye mgongo wake kwakuwa geti lilikuwa wazi aliweza kupitiza hadi nje kabisa ya hii nyumbani hakutamani hata kugeuza uso wake mana alikuwa akinizarau lakini shughuli  aliyoipata hakuweza kuamini kabisa kama amemfunza adabu Kamanda mzima......

******huko nyumbani naomi akiwa katumwa dukani akanunue baadhi ya mboga akiwa njiani alibetuliwa bila kujielewa alianguka chini puu duuh alilia sana lakini baada ya dakika chache akakakuta akinyanyulia na mtu baada ya kugeuka kumbe alikuwa ben kafikaje hadi hayo maeneo hakuna anaejua.....baada ya kumnyanyua nilimruhusu aendelee na safari yake ili nichuane na huyu aliyembetua ngwala nae baada ya mimi kumnyanyua naomi na kumruhusu aende ilionekana ni kitendo kilichomuudhi sana akanisogelea na kunishika roba shingoni kama kunitisha lakini alishangaa kuona mimi nacheka tu akataka anipige zinga la kofi lakini ni kama kitendo cha sekunde alikuwa tayari kakunjwa mkono wake yaani akileta fujo nilimwambia navunja....hakuwa na la kufanya ilibidi aombe samahani na mimi nilimwachia aendelee na safari zake niliifuata pikipiki niliyokuja nayo aina ya boxer kisha nikaendelea na safari zangu nilitembelea mitaa mingi sana siku hii badae niliamua kurudi nyumbani.
..naomi nae alipofika nyumbani aliwaeleza yaliyomkuta njiani.......nikiwa bado katika usafiri nikielekea nyumbani kwa naomi simu yangu ilikuwa ikiita lakini kabla sijaipokea mbele yangu niliweza kuona.......itaendeleaaaAa

benchrys.blogspot.com

De 27

Gangstar noma
By: benchrys
27

.........kulikuwa na polisi wanne ambao waliwekwa kama walinzi kwenye ile hospital kwahiyo rasta ule mda wote walikuwa wakimtazama tuu jinsi anavojitia yeye ndiye kidume katika ile hospital jukumu walilochukua wao hata hawakutaka kujisumbua sana walimtuma mmoja wao ambae alikuwa kashika zile fimbo maalumu ambazo zina cheni ndani yake baada ya hapo alimpiga katika bega lake la upande wa kushoto huku yule mwenzake ambae wapo pamoja akibaki kushangaa, lakini nae haikupita mda mrefu akajikuta akiwekelewa pingu kwenye mikono yake huku akiamrishwa asonge mbele tens bila kuuliza swali lolote lile. Kiukweli hii siku rasta na mwenzie ni siku ambayo waliifurahia sana lakini kutokana na majanga haya wakajikuta wakiilaani vibaya maana hawajui hatima yao kitakuwa nini....mana wameibiwa hela pamoja na funguo za gari wakajitahidi kuwahi hospital ili wasimpoteze ben ila bado wamemkosa kibaya zaidi wamemaliza hata kiasi kidogi cha pesa ambacho walikuwa nacho.....
    
    Walifika kituon wakiwa na wale maafande wa ile hospital kusha wakaamrishwa washuke, kwakuwa walikuwa chini ya ulinzi hawakuweza kubisha kwa lolote walifuata masharti yote.  Lakini baada ya mda kidogo akaja afande mmoja ambae alionekana kidogo ni mkarimu kupita wale wengine wote alimsogelea rasta na yule mwenzie na kuwauliza
:nawaona nyie wote hapa ni wageni samahani ningetaka au niombe kujua ni nini kiliwasibu
:rasta kwa kimbelembele akajifanya kujua sana kwa kutolea maelezo ya uongo....kiukweli afande hapa tulikuwa tumekuja kumwona mgonjwa wetu ambae kabla ya kufikishwa tulielewana na dereva kwamba ajitahidi kukumbuka chumba namba ngapi, na baada ya dereva kusema hafahamu lolote mimi nilijua labda labda katuuzia mgonjwa wetu ndipo nilipatwa na hasira kisha nikampiga lile kofi..alieleza vile rasta

Afande..ok chukua simu yako ili uwape taarifa ndugu zako juu ya jambo hili. :rasta baada ya kuambiwa vile akaona huyu afande inaonekana hana msaada kwakuwa yeye pale hakuwa na simu kutokana na simu yake kuipasua kule hospital

Samahani afande hapa sina simu labda nimuombe mwenzangu maana tulikuwa wote....aliongea vile rasta

Ndio nini sasa simu yako iko wapi hadi uazime ya mwenzako...afande aliongea
Rasta nae akajibu iliangua kule hospital kisha iliharibika kabisa..kwakuwa afande alikuwa ni mtu mwenye busara akamruhusu kuazima simu ya huyo mwenzake.  Basi rasta alimwita mwenzake kisha akamwomba simu lakini hawakufanikiwa na pia afande aliondoka baada ya kusikia kuwa mwenzie na rasta nae hana simu mahali pale kwasababu nae simu yake iliachwa kule kwenye gari ambalo funguo zipo na ben........

********
********
      Ivi jamanj humu ndani inakuaje kipindi hiki!!!! We naomiiiiiiiii uko wapi hebu njoo kuna jambo nahitaji kukuuliza hapa....alikuwa akiongea mama huko nyumbani baada ya kuona mambo yasiyoeleweka mule ndani
Bee mama nimefika...naomi
  Mama: hapa kuna jambo nimeliona halafu hata sijalielewa sijui ni nini hiki sasa, hivi hizi bastola humu ndani zinatokea wapi?
:naom: kiukweli mama hicho kith alirudi nacho ben sikumoja hivi ambapo aliwahi kurudi kama unakumbukua ile siku amerudi sa 9 ndipo alirudi na hivo vitu mimi sielewi alipata wapi kwakweli
Mama: ok sawa nitamuuliza wee endelea na shughuli zako...lakini alipokuwa akiondoka alimtumia meseji ben ikisema kwamba ""mama ameziona zile pisto ulizorudi nazo ile siku akaniuliza ni vya nan ila nimemwambia kuwa ni vyako, ukiona nomekosea nisamehe tuu bure ben""

Nikiwa nimekaa kwa merry baada ya kutoka kutembea huko kwenye simu yangu iliingia meseji, nilipoifungua ndio alikuwa naomi niliifungua nikakutana na ujumbe ule aliouandika kunipa taarifa za bunduki zile ndogo ila sikichukulia uzito wowote nilimuandikia ""akikuuliza tena mwambie ahifadhi ndani vizuri" kisha nikaituma kwa naomi.. Kwakuwa iliingia giza nienda ndani na kuendelea kucheza na computer ya kule chumbani kwangu, sikukaa sana merry aliniita kisha tulipa chakula na kuelekea kulala

********nikiwa usingizini*****

.....dogo safari hii utakamuliwa hadi utumbo maana kama ni kutusumbua akili umetusumbua vya kutisha nadhani wakati umeisha sasa. Aliongea mmoja na mwingine kisha mmoja akasema...niko tayari hata nigombane na ukoo wako wote ile tuu nikamilishe hii kazi sijui kama unsnisoma we dogo alipomaliza akanibamiza kofi jipya la 5g duuuuh kidogo nilie maana wakati huo wote nilikuwa nilikuwa nimekalishwa chini huku nimefungwa kamba kwenye nguzo fulani...nikiwa na hasira sana niliomba sana Mungu alete miujiza hii kamba hata ikatike itakuwa powa sana..huku wao wakiendelea kunitupia maneno mengi

Aaaah   mungu mkubwa nilijisemea kimoyomoyo tena kwa furaha mana kuna mbwa sijui alitokea wapi alianza kutafuna ile kamba kwakuwa ilikuwa usiku hakuna aliyeweza kuinasa hadi nilifanikiwa kukimbia lakini nikiwa natoka njee sikuweza kuamini nilianza kujisemea pekeyangu hivi hapa nimekwepa au ndo nishatumbukia....hayo maneno yalitokana na hali iliyokuwapo njee ya nyumba kulikuwa shimo kubwa ambalo sikujua hata limechimbwa mda gani, nilisogeza mguu kutaka kujua n nini kipo mle nikiwa nasogeza mguu wangu udongo ule ulianza kuvunjika ukielekea kwenye lile na mimi hapo nilitereza kutumbukia kwenye shimo***nikaja kustuka kumbe nlikuwa naota usiku ule duuh.. Nilichukua saa na kuangalia ilikuwa ni saa 10 na nusu usiku kwa kuwa nlikuwa bado nnausingizi nilivuta blanket tena ili nilale ndani ya dakika tano tayari nilishachukuliwa na rafiki wa wengi ambae ni usingizi
    Ilifika asubuhi niliamka lakini nikiwa naelekea bafuni nilipita jirani na chumba cha merry nikasikia sauti ya mtu analia, sikujali sana nikapita ile naludi bado niliona bado ile hali ila bado sikujali sana nikaingia chumbani kwangu nikavaa nguo nyingine na kutoka ndipo nlimkuta merry amekaa sebuleni akiwa bado analia, nilimsogelea taratibu ili kumwuliza lakini nilipofika tuu jirani naye pale kwenye aliyumbisha kichwa na.... Itaendeleaaaaaa

benchrys.blogspot.com