Ijumaa, 21 Oktoba 2016

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 19

Tuliposhia>>>>

---baada ya kuingia kwa mganga bila hata hodi ghafla nikabadilika na kuwa kuwa ninja, niliweza kujiona kupitia kioo ambacho kilikuwa mbele yangu
Kiukweli nilikuwa natisha sana hadi mwenyewe nilijiogopa usoni hata kipande kidogo changozi hakikuwa kinaonekana ila kulikuwa na maski ambapo inangaa sana huku kwenye alama za macho kukiwa na vitobo vitatu kwa kial jicho ambapo kila kitobo kilionekana kinatoa kama miale ya rangi tofauti kijani, nyekundu na nyeupe
Ilikuwa nikigeukia upande huu tuu unawaka mwale tofauti hii hali hata mimi mwenyewe sikuweza kuielewa ila nilijali mimi ni nini kimenileta

Wakati huo mganga nae alikuwa anapiga piga kama kangoma fulani ambako kamepakwa baadhi ya rangi. Alipiga kwa mda fulani huku akiwa anaongea na baadhi ya maneno ambayo baadhiniliyasikia na mengine hata sikuweza kuyasikia na kuyaelewa lakini niligundua kuwa huyu hizi nyimbo zake ni za kushangilia kitu fulani lakin bado sikujua anakishagilia anachokishangilia ni nini
Baada ya hapo alikitupa kile kingoma chake kidogo mbali kidogo ambapo mimi nilipoangalia niliona kama ni ukuta lakini cha ajabu kilekingoma kilipitiliza na kitua upande wa pili na kwa gafla tuu pakawa na uwanja mkubwa sana

Kwa akili yangu nilishajua kwamba kuwa wadudu lazima anatumia kupiganishia kitu ambacho kinataka kushindana na yeye na ndio maana anafanya huu uchawi ili ajihadhali mapema na kitakacho tokea hapa
Baada ya hapo nikiwa nimesimama mara nikweza kuona mnyama wa ajabu sana ambae hata sikuwahi kufikilia kama ipo siku nitaweza kumwona katika macho yangu

Mnyama kwa kumwangalia alikuwa na meno yasiyopungua kama mia mbili ikiwezekana ni zaidi hata ya hayo
Alitoa sauti ambayo ilisababisha hadi tetemeko kubwa sana katika uwanja ule baada ya hapo akaanza kun fuata kwa mwendo wa maringo
Na mimi kwa haraka hata sikulaza damu niliuchomoa upanga wangu huku kwa mbali nikimwona mganga anacheka huku ameshika kitu fulani mithili ya mkia wa ngombe na kuuzungusha kwa satili ambayo yeye aliijua zaidi
Mara yule kiumbe alijizungusha baada ya kumwona upande wake wa nyuma alikuwa na mkia wenye unene kama gogo la nguzo ule mkia ulikuwa ukija kulikuwa na upepo ukivuma kam kuna ndege aina ya helkopta ipo upande wa juu yangu akili yangu iliweza kugundua kwamba huu unatakiwa unitandike
Ule mkia ukiwa jiran niliruka juu ili kuukwepa ambapo ukaenda kugonga nguzo moja ambayo ilikuwa jiran na uwanja ule na baada ya hapo ile ilivunjika na kudondoka chini hii ni kuonyesha ule mkia uzito wake na nguvu zake ni hatari tupu

___upande wa pili baba tayari alikuwa amesha rud kutoka kazini kwake jioni akafika na kuanza taratibu zake huku akiita boniiiiiiiiiiiiiiiii, boniiiiii uko wapi mbona sikuoni

Na baadaya kuona kimya aliamua kuchukua simu yake na kunipigia iliita kwa mda mrefu sana kisha akapokea majibu
MTEJA UNAEMPIGIA HAPOKE_____
Hakutaka kusikiliza sana akakaa simu na kisha akaendelea kufanya mambo yake mengine, kwa wakati huo ilikuwa ni saa kumi na mbili za jion
Baada ya kufanya kila kitu kilicho kuwa katika ratiba zake
Ulikuwa mda kamili wa yeye kula ili aweze kulala au kujisomea vitabu vyake
Muda wote huo alikuwa ni mtu mwenye mawazo sana. Kuhusu mwanae bon ameenda wapi hadi mda huu aliangaliaa saa yake ilimwonesha ni saa mbili karibia na nusu ila akahisi labda nitakuwa nimeenda kwa joel kwa maana ndio mahali ambako mara nyingi napenda sana kwenda kutokana na kwamba tulikuwa na urafiki wa kitambo sana
Baba alikuwa kisha akafunga safari ya kwenda kwa akina joel, lakini akakumbuka kuwa pale nje palikuwa na vifaa vya utengenezaji wa barabara, aliamua kuzungukia ili akaangalie kama wameishia wapi katika hiyo kazi yao ya kufanya uwekezaji kwenye nyumba ya mtu.
Baada ya kufika kule nyuma ya nyumba yake aliona hakuna kitu chochote
Alicheka sana huku akijisemea MLIJUA KUNA MAJINI NA BORA MMEONDOKA WENYEWE ASANTE MUNGU KWA UAMUZI ULIOUTOA.alifurahi sana  kisha ndio akashika njia ya kwenda kwa akina joel alitembea kwa mda mfupi tuu na baada ya dakika kama tano na sekunde tayari alikuwa tayari ameshatia mguu pale, ambapo alipokelewa na baba ake na joel
Ooooooh karibu baba bon
- ah asante nimekaribia kwema lakini
Hapa kwetu kwema kabisa sijui utokako
- nako nadhani kutakuwa ni kwema hivo hivo
Haya karibu ndani ila mbona umetembea pekeyako na bon umemwacha wapi tena
Baba baada ya kusikia hivi akajua kwamba mwanae bon na hapa hayupo hapo ndio mawazo yaliongezeka zaidi akazidi kujiuliza kichwani mwake maswali mengi zaidi na asipate jibu lolote, ila kwa safari hii alijifariji kuwa
Aaaah mawazo ya nini wakati sio mtoto mdogo___akiw anaendelea kufikiria bado baba joel akauliza tena lile swali lake +=bon umemwacha wapi pekeyake (

Hivi unavoniona nimekuja hapa huku nikijua kuwa bon nitamkuta hapa lakini kumbe na hapa hayupo tena

Duuuh hili tatizo sasa kwahiyo unaenda ktnagza au unaacha tuu(aliuliza baba joel
Safari hata sihangaiki kutangaza inamaana bon bado mtoto mdogo namna hiyo kila siku niwe namtangaza tuu si hata vituo badae vitanichoka maana vinaona kila siku matangazo yangu tuu kwenye redio tena kuhusu mtoto ambaye akili zake ziko sawa kabisa, huwezi jua ni kwanini ameondoka pengine akirudi atasema alikoenda hebu tusubilie tuu (aliongea baba

Kisha baba joel akajibu sawa kuonyesha amekubaliana na mwazo ya baba
Jamani majirani basi mimi niwakimbie au mnasemaje(alikuwa baba akiaga na kusimama lakini baba joel akasema ngoja nikusindikize hadi kwenu maana wewe upo wewe tuu kila siku
Sikumoja moja hahahahahahhaaaa. Walicheka pamoja kisha wakaanza safari ya kwenda nyumbani walifika hadi nyumbani ambapo baba joel alifika moja kwa moja pale kwenye meza ya baba ambayo anatumia kujisomea vitabu vyake,.
   Jirani naweza kuangalia chochote hapa au marufuku kugusa kitu
Ahaa kwenye hiyo meza wewe angalia tuu ikiwezekana kaa kabisa hadi kesho hadi utakapo ridhika kuangalia

Baba joel baadaya kuruhusiwa kuangalia chochote kadiri alivoomba alikaa na kuanza kupitia vitabu vile lakini akiwa anaendelea kutazama kuna karatasi fulani aliona maneno yanayoishia BY NON, kwa haraka akaliwahi na kutaka ajue kuna nini ndani yake alipofungua alikutana na ujumbe ambao ulimfanya amwite baba ili wasome pamoja. Waliusoma ila wakabaki wanajiuliza mama yake alimwona wapi

Tukirudi kwa mganga tunamwona bon amelala chini akiwa hana nguvu kisha-----itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 18

Tulipoishia>>>>>

Walimsogelea lakini ile kumgusa tuu walisikia kishindo kizito sana juu ya gari moja walilokuja nalo pale wote walishtuka na kuangaza macho ule upande ambao kimesikika kile kishindo, lakini hawakuweza kuona chochote mmoja waoa kachukua saa na kuangalia ni saa ngapi mda ilikuwa inaonyesha ni saa 9 na nusu usiku
  Mmmmh ila kuna watu hapa duniani wapo kwaajili ya kuwapa watu mateso ivi mwenzenu sijawahi kufikilia kuwa nitakuja kufanya kaza ya ulinzi lakini leo ndio mara yangu ya kwanza ivi wenzangu mmeonaje kuhusiana na hili swala la sisi kulala kama mapopo hivi huku tukilinda magari ya mtu bila malipo yoyote yale huu uboya.(alikuwa akiongea mwenzo mmoja)
    Aaaaah na wewe unangea nini bhana mimi nawaza kama yule jamaa akija tena hapa ambae ametupa kichapo itakuwaje mana saizi yenyewe mauza uza kibao mara vipite vivuli tuu kama hvi saiv kishindo sijui ni cha nini, shit huu uboya mi naamsha hata sasa hivi ambaye yupo tayari twenzetu
Baada ya kuongea vile alianza safari yale na kwa kuwa nyumbani kwao hakukuwa mbali sana wote waliungana na kuondoka lile eneo bila kumwacha hata mmoja wao

____ilifika asubuhi boss wao alikuja na kuanza kukagua kama waliweza kumwona baba lakini cha ajabu alifika na kuyaona tuu magari yake yakiwa pekeyake pale
Kwa mawzo yake alielewa kwambayawezekana wamelala ndani ya magari kwahiyo bado watakuwa hawajaamka
Akalifuata gari moja na kuchungulia kwenyekioo lakini hakuona kitu akafuata jingine nalo aliona ni hivo hivo. Hapo akajua kwamba hapa wala hakuna mtu alianza kuongea pekeyake
IVI HAWA WATOTO WA MTU GANI, WAMEKIMBIA NA KUACHA MAGARI YANGU HAPA HUKU NILIWAPA KAZI YA KUFANYA. SASA NTAMTAFUTA MMOJA BAADA YA MWINGINE.
Baadaya baadaya hapo alitoa simu mfukoni na kumpigia mtu mmoja
Yaa ndio mheshimiwa, aah ndio, sasa nilikuwa nahitaji mtu wa kuendesha scaveta kama watu watatu hivi nataka wakaniondolee sehemu moja hivi vyombo vyangu, ok sawa ukipata nambie, yaah hakuna tatizo kabisa, ok asante sana.
Baada ya hapo akashusha simu yake na kuingilia moja ya gari kisha akaondoka nalo

_____ilipofika mda wa kazi baba kama kawaida aliondoka na kwenda kazini kwake na kuniacha pale nyumbani
Na mimi nilipoangalai ratiba zangu nikagundua kwamba hii ni siku nzuri ya kwenda kumwangamiza yule mganga ambae ndio hufanya kazi  na akina babu na bibi ili kuwapoteza ndugu zetu
Nilichukua begi langu na kuweka baadhi ya vitu kisha nikachukua karatasi na kuandika maneno fulani kwa kalamu ambayo yalisomeka
SAMAHANI BABA NAJUA UTAJIULIZA SANA NIMEONDOKA NA KWENDA WAPI,. ILA UKWELI NI KWAMBA NIMEENDA MAHALI KWAAJILI YA KUTEKELEZA MAAGIZO AMBAYO NILIACHIWA NA MAMA MARA YA MWISHO KUONANA NAE,.. BY BON
Kisha nikaifunga na kuweka sebuleni kwenye meza yake ambayo mara nyingi hupeda kukaa na kujisomea vitabu vyake. Na baadaya hapo nikaondoka na kwenda katika duka moja ambalo lilikuwa linajishughulisha na kuuza pikipiki nilinunua pikipiki moja aina ya boxer nilipohakikisha kila kitu kipo sawa nianza safari yangu rasmi ya kwenda kwa mganga
Safari hii ilichukua masaa kama saba hadi kufika maeneo ambayo nilikusudia lakini nikakumbuka kuwa mganga huyo anaishi jirani na mtaa wa mawen ambako niliacha vitu vyangu baada ya kuondoka na kwenda kwa baba.
Baada aya hapo niliamua kugeuza na kwenda pale lakini nikapitia ili kuapata baadhi ya mahitaji yangu, nilifanya hivo kisha nikaenda hadi pale nyumbani

Nilipofika niliwaona akina asha na mwenzake amina wakiwa wamekaa tu nje wanaotea jua la jion
Uso wa asha ulionyesha unafuraha sana lakini hawezi hata kusema anishingilie kwa maana hata jina langu hakuna anaelijua katika ile nyumba

Baadaya kufika niliapaki pikipiki yangu nje na kuingia ndani huku nikiwa na badhi ya mafurushiyangu niliyotoka kununua huko ila nikakumbuka hakuna jiko humu ndani nilitoka tena nje na kuchukua pikipiki yangu kisha nikaelekea kwenye maduka yanayohusika na kuuza majiko. Nilifanikiwa kuliona duka moja ambalo ndio walikuwa wamepanga majiko mengi sana nje pale, mwendo wa fasta tuu nilisimama na kufuata lile duka ili niulizie jiko lakini nikiwa ndio nafika mlangoni nyuma nilisikia mtu anapiga lesi kwenye pikipiki yangu. Akili yangu ilinituma kwamba hapa nitaibiwa halafu nishindwe kufanya kazi ambayo imenileta hadi huku.
Haphapo niligeuka na kurudi hadi kwenye pikipiki nae alipoona narudi kwakuwa kuondoka alisha chelewa akaamua kushuka akiwa nalengo anipige ili yeye apate kuondoka na pikipiki
Alifika kichwakichwa tuu na kunirishia ngumi asijue mi mtu wa namna gani
Ile maurusha tuu mkono niliudaka haraka na kuuvunja kisha nikamwacha pale akiwa na maumivu ya kuvunjwa mkono yani ilikuwa ni ndani ya nusu dakika tu tayari mtu ashaachiwa ukilema kisa wizi
Niligeuka na kurudi tena kwenye majiko kisha nikachagua jiko linalonifaa na kuchukua pikipikikisha nikaondoka na kurudi nyumbani ile nimekaa nyumbani mda kama wa saa tatu hivi nikawa sauti kutoka nje watu wanaongea
+++nilisikia anakaa  hapa tena nahisi ni humu ndani kama siyo ngoja kwanza tukagonge ili tuone kama kweli
Sema mwanangu inatakiwa tuingie kwa akili sana mana asije akawa ni mtu wa hatari mana ukifuatilia tangu anaingia tuu siku ya kwanza usiku ni mtu ambae hata hapendi ujinga ujinga na mtu licha ya kuwa anaonekana ni mpole sama kwa usoni.
Kudadeki acha uoga wewe inamaana tumetembea tuu bure mwenzetu amevunjwa mkono halafu tulifumbie tuu macho suala kama hili kwa upande wangu mimi sikubaliani hata kidogo yani ama zake ama zangu liwalo na lile.(walikuwa wakijibizana hivo wasijue kwambakila wanachoongea nimesha kisikia tayari
Baada ya hapo walifika hadi mlangoni kwangu na kuanza kugonga kwa fujo kweli
Ngongongongo
Nani unagonga (niliuliza kisha nikajibiwa
Binadamu..ok sawa kama wewe ni binadamu nahisi mimi ni binaugali au maji sawa kaa hapohapo kama mlinzi kama huwezi kujitambulisha sawa
Halafu acha uboya hebu fungua mlango vipi wewe utajuaje kama mimi ni balozi?
Sidhani kama balozi unauhuru wa kutoa majibu ya chooni kama hayo kwa usalama wako nakuomba tuu ondoka (niliwaambia hivo  badaya kuona kama wananiletea nyeusi tuu)
Na hapa haondoki mtu sasa hadi kieleweke tuu(walinijibu )
Poa ngojeni kwanza kitaeleweka tuu hata msijali nisubirini nyie si ndio wasumbufu wa nyumba za watu.>baada ya kuongea vile nilinyanyuka na kutokea dirishani kisha nikawazungukia hadi mlangoni na kuanza kuwafumua tuu makofi kama naadhibu mwanangu hivi. Baada ya kuona makofi tuu wamelizika waliamua kuondoka mbio na kurudi makwao

Baada ya hapo kwa kuwa nilishukuwa nimekula na kushiba safi kabisa nilichukua pikipiki tena na kuondoka hadi kwa mganga kisha nikapaki pikipiki mbali kidogo kisha nikaingia hadi ndani bila hata hodi------itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 17

Tulipoishia>>>>>

Baada ya mimi kutoweka pale ile gari ilisogea hadi jirani kabisa kisha akashuka yuke baba aliyeyejitambulisha kwa jina la mkuti kule ofisini kwa baba
JAMANI YULE KIJANA YUPO WAPI NAMHITAJI ILI NIKAMPELEKEE BABA AKE MAITI YA MWANAE MAANA ANANILETEA DHARAU AMBAZO HATA SIZIELEWI(laiti angejua jinsi alivokuwa anawaboa hawa wafanyakazi wake ambao aliwapa ile kazi hata asingethubutu kuongea yale ambayo anayaongea kutoka mdomoni mwake mda huu
Jamani hivi sinawauliza nyinyi au siongei na nyinyi mimi tayari nimeshakuwa chizi au. Licha ya yeye kuongea maneno mengi mfululizo lakini hakuna aliyeweza kunyanyua mdomo wake ili atoe angalau hata jibu maana wote pale walikuwa wanaugulia maumivu ambayo wameachiwa kama zawadi na bon a.k.a ninja halafu yeye anawaletea nyeusi. Mmoja uvumilivu ulimshinda akaamua kupwayuka tuu
<<<<mzee kama uliona kazi sio lazima sana kuifanya ni bora ungeniacha niendelee kusafisha tuu mitaro kule ulikonikuta sio kuanza kuagiziana watu ili watufanye vilema tena bila hata faida hata ya mia mbovu, sihitaji niongee sana cha kufanya nipe tuu changu kwa maana umenisumbua tuu na hakuna nilichokipata

Boss wao baada ya kumsikiliza sana akaona huyu tayari asahaanza kuwa kichaa au kachanganyikiwa na maisha hadi anapwayuka maneno kama haya.
Aisee nimekusikiliza sana lakini hata sijakuelewa kwa lolote labda saizi hapa naomba kujua unamaana gan kuongea maneno kama hayo ambayo unayaongea. Baada ya kuongea hivo akamgeukia mwingine lakini wote sura zao zilikuwa zimekunjamana mbaya hadi boss akaanza kujiuliza maswali inamaana hawa watu wameamua kumnunia, ila bado akajiuliza inamaana ile pesa aliyowapa haijatosha chochote au ndio mbongo huwaga hawezi kulizika akapepesa macho huku na kule ili amwone yule ambae alimkabidhi ile briefcase yenye hela za kuwapa wenzake lakini hakumwona, akaanza kutembea tembea kidogo kwa mbele aliweza kuna mtu amelala chini kama amekufa vile lakini aliposogea hadi jirani aliweza kugundua kuwa bado anahema akajaribu kumsogelea jirani nakumtikisa ili aone kama anaamka, kwanza akashtuka kuonandio yule ambaye alimkabidhi ile briefcase yenye pesa zile. Lakini akabaki na maswali inakuwaje hadi yupo katika hali hii. Alijaribu kumwamsha ili hata mawili tuu lakin hakuamka, hapo boss andio akajua kwamba huyu kazimia lakini bado hajajua ni kwasababu gani hadi amezimia pia akawa anajiuliza mbona na wale wengine wapo katika hali ile
Akiwa anaendelea kujiuliza akageuka nyuma kuangalia vifaa vyake kama vipo sahihi bado kwanza aliangalia lile gari ambalo walikuja nalo akaona vioo vya upande wote vina vumbi la hatari sana kana kwamba hata kama ndani kuna kitu huwezi kuchungulia na kuona chochote kidogo nae achanganyikiwe

_____bon_____
Muda wote baadaya kumaliza kazi ya kuwatuliza wale wafanyakazi wa mkuti niliingia ndani na kufungua ile briefcase kisha nikaanza kuhesabia pesa ambazo zilikuwa mle ndani ya brifcas nilihesabu huku masaa yakiendelea kwenda ila nikakumbuka baba sio mda mrefu sana anaweza akarudi sasa akifika hawa bado wapo hapa nje lazima waanze kumsumbua na mimi sitaki hata mtu mmoja ajue kuwa bon ni nani katika upande wa mkono, nilichokifanya ni kupiga simu kwa baba na kumwambia leo itabidi kidogo achelewe kurudi hapa nyumbani kisha nikamwelekeza ni kwanini namwambia hivo,,. Baba nae alinielewa kwa haraka kisha akakata simu nakuniambia atakapo kuwa anarudi atanambia kupitia simu kisha simu ikakatwa

Huku nje baada ya kukaa kwa mda mrefu kumbe ni kweli walikuwa wanamngoja baba ili wajue siri ya hili eneo kumbe hakuna siri yoyote ile isipokuwa tuu wameingia kwenye mikono mibaya na kujikuta wakikunjwa kama chapati inaandaliwa kunywewa na supu

Walikaa sana masaa yalienda hadi ikafika usiku wa saa nne hivi wakajisemea hapa hakuna mtu kutoka hadi tujue hatima ya huyu mzee
Ila mmoja waoa akasema>kinachomchelewe nini mbona sijawahi kuona mzee akiwa ananajaribu hata kunywa au kwenye sehemu za starehe sijawahi kumwona
    Ivi kuna binadamu ambaye unaweza ukakariri tabia yake kwa jumla we kaa hapo hadi arudi ili na sisi tupate chetu sawa chogo
  Kudadeki tutazinguana hata kama ni usiku tena maeneo ya watu nani chogo tabia kama una*****

Wewe nikaushie huko hasira nyingi halafu hujiwezi mamaza mengine bhna

Halafu nyie acheni uboya huo(kilisikika kibezi kikitokea upande mwingine wote waliogopa kumbe alikuwa ni mwenzao) nae baada ya kuona wameogopa na kutulia akacheka na kuwaambia mnajifanya mnachimbana kumbe wote manyoro tuu shit

____kwa bashir ___mda wa saa mbili kama nusu tunamwona bashir akiwa anatoka kwa asha wpangaji wenzake wakamwona kisha wakaanza kucheka baada ya kuona anajinyoosha kama alilala juzi vile na miayo mingi kweli ila aaaaaamh kama anataka kummeza mtu vile

Hahahahahaaaaaa bashir kichaa lao mbona upo hasso hivo vipi tena ulikuwa na mtanange au (alikuwa ni rafiki yake mmoja kwa jina la john
Licha ya kuongeleshwa hayo maneno mengi lakini bashir hata hakujibu chochote maana kwanza alikuwa akachoka sana isitoshe alikuwa na njaa sana mana toka azimishwe mchana hajaamka hadi saizi ndio anakurupuka
Alienda moja kwa moja hadi kwenye chumba akitegemea atamkuta mke wake lakini chaajabu aliona hata taa imezimwa kuonesha dhahiri kwamba humu ndani hakuna mtu kwa wakati huu. Aliingia ndani na kuwasha taa yake lakin bado hakuona mtu ila alishangazwa baada ya kuangaza mle ndani aligundua kuwa kuna baadhi ya mabegi hayapo mle ndani. Alianza kama kichaa au kapandwa na mapepo doriii, dorii hadi wapangaji wengine wakawa wanajiuiza inamaana dori bado yupo tuu
Kumbe mke wa bashir aliitwa dori na inaonyesha dori ameondoka kaenda wapi haieleweki
Bashir akabaki mdogo zaidi basi hakuwa na njia nyingine aliamua kuchukua pesa yake na kwenda kwa mama ntilie ili akapate chakula alale ili aione kesho

____bon__nikiwa nimekaa tuu mle ndani meseji iliingia kwenye simu yangu nilipotazama niligundua kuwa ni baba., nilinyata hadi kwenye geti kumbe nae alikuwa kabana kwenye maua ambayo yalikuwa jilani na geti nilipofungua tuu geti mara moja nae akaingia ndani kisha tukafunga geti tukala la kisha mimi nilienda kulala na kumwacha baba pale sebuleni
Na huku nje wale waliopanga kukutana na baba bado tuu walikuwa wakingoja huku wakiwa na imani kwamba bado hajarudi na ndani ya nyumba nipo mimi tuu pekeyangu

Wakiwa bado wanazunguka nyumba yetu mara wakahisi kama kuna kitu kimepita tena kasi hadi kinaacha upepo wote walistuka na kuwa makini sana ili kukiangalia kama kitapita tena lakini hakikupita tena.
Ni kama saa sita usiku yule aliyekabidhiwa hela na boss ndio alikuwa anazinduka akiwa na maumivu sana upande wake wa mgongo mana ndio ile ngumi ilikokita. Alianza kujinyoosha kwa kupiga kelele kama mtu anatapika vile na kulia humohumo hadi wale wenzake walishtuka ila wakagundua kuwa ni mwenzao ndio anaamka walimfata na kumshika, lakini ile kumgusa tu-----itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 16

Tulipoishia>>>>

Bashir baada ya kugonga mlango na kuona hafungiliwi aliamua kuusukuma kwa nguvu ili aingie ndani kumfunza adabu huyo asha ambae yeye mara nyingi ni mshabiki kipindi kama bashir akiwa kakutana na majanga hasa ikitokea amepigwa na mtu fulan
Bashir alitumia nguvu hadi alifanikiwa kufungua ulemlango lakini alipoingia ndani kabla hajaweza kuona chochote alipigwa na kitu kizito kichwani kwake kilicho mpelekea hali ya kuweweseka na kuanguka chini puuuuuu kama mzigo kisha asha akaanza kushangilia kuwa ameweza kujitetea na mbaya wake baada ya hapo asha alitimuka na kutoka nje hadi hadi kwa rafiki yake amina hata kama walipigana ila bado utani kwao ulikuwa ni wa damu kabisa
Shogaangu nifungulie mlango basi
Jiheshimu wewe umefumaniwa au inakuwaje mbona upo haraka hivo
Ahaa we acha tuu nifungulie kwani tuongee bhana,. Usinizingue hebu ngoja kwan nifanye yangu ndio nafungua kaa hapohapo kama mlinzi sawa., daha kwakuwa ni kwako nakaa ila usinzingue., asha hakuwa na namna nyingine zaidi ya kumngoja tuu amina amfungulie mlango wake

Mlango ulifunguliwa amina akaingia ndani huku akiwa kama hajiamini hivi,.. mana bada ya kuingia tuu ndani aliufunga mlango tena kwa ndani kisha akaanza kumwelezea

Ivi wewe leo unanini wadudu wako leo inaonekana umewapa maji ya moto haya niambie kinachokukimbiza namna hii nini
Shogaangu we acha tuu bashir alikuja akangonga mlango wangu sikufungua maaana nlishajua kabisa anataka anipe kipigo
Basi akalazimisha had amefungua___alieleza maelezo yote kisha wakacheka sana kwa maana asha alivofanya alionekana kama shujaa sana kwa kumkomoa bashir licha ya kuwa amezimia wao walishajua ataamka tuu.,>>>>

>>>>ilipofika asubuhi nyumbani mimi na baba tulifanya utaratibu wote kisha baba akaelekea kazini kwake hukuakiniacha tuu pale nyumbani sikukaa sana nikaondoka na kwenda kwa joel ambae nilipotezana kitambo kidogo
Ngo ngo ngo hodiiiii
Hodiiii wenye wenye nyumba
///mmmmh hii mbona kama sauti ya bon hivi ngoja nikacheki kwani,. Alikuwa akiongea vile joel mda ule yupo na babaake.
Joel alisimama na kuja hadi mlangoni ambapo hakuamini kukutana live na uso wa beni maaana ni miezi mingi sasa imepita tangu nipotee na kutangazwa kwenye baadhi ya vituo vya redio lakini bado sikupatikana
    Dahaa  babaaaaa ni bon kweli aisee daah nambie mwanangu mbona adimu sana ulipotelea wapi mana kitambo kinoma
Dah mdau mi nipo mbona sema mambo ya hapa na pale tuu ndiyo yanafanya hadi hatuonani nilimjibu vile huku nikijua kabisa hata weza kuridhika kabisa na hili jibu. Kisha akaendelea kuongea
Bon unazingua mishe za hapa na pale huku tangu skuli watu tulikutafuta kinoma mahafali yenyewe ulisepa hukuonekana, au ulipata mishe kabla hata hujapata cheti cha umeme?
Usijali ntakutonya tuu ngoja nikamcheki mshua si yupo humo ndani au
Yah yupo ndani((((tuliingia ndani huku tukiwa bado tunaongea mambo meng tuu kisha nikafika na kumsalimia baba yale lakini nae alionyesha anashauku ya kujua wapi ambako nilipotelea kwa mda wa karibia mwaka mzima sijaonekana hadi wananitafuta bila mafanikio,. Lakini wote niliwaambia ni stori ndefu sana

Tukiwa tunaendelea kupiga stori pale kwa akina joel mara gafla tuu nilipitiwa na usingizi na kuanza kuota nyumbani kuna greda na d6 yapo yanavunja nyumba. Hii ndoto ilinishtua sana hadi nikajikuta nikinyanyuka pale kwenye kiti huku nimechoka sana
We bon vipi mbona kama hatupo wote hapa unasinzia ndani ya dakika tano na kushituka kama ulilala jana vipi bhana kuna tatizo au(aliuliza hivi babaake wa joel lakini sikujibu kitu nikasimama na kuwaaga kuwa mi naenda wote hawakuweza kuelewa ni nini maana ya hili jambo lakini ukweli wote ulikuwa ndani ya moyo wangu
Samahani mambo yakiwa vizuri badae nakuja hata kukesha tuu ila kwa saizi naomba niende nyumbani. Sikuhitaji ruhusa nikafungua mlango na kuondoka ili nikaone nyumbani kupo katika hali gani. nilipiga hatua za haraka haraka sana kwa mda mfupi tuu tayari nikawa nimeshafika nyumbani.
Nilipofika nyumbani nilishangaa kuona kuna magari ya wide road yapo pale huku pembeni kuna greda moja na d6 moja kwa mbaaaali nikaona kile kigari cha kushindilia nacho kikija usawa wa pale nyumbani

Sikutaka kubaki kimya nikaamua kuuliza
ETI SAMAHANI HIVI VITU VINAELEKEA WAPI
Aliyekuwa jirani akanijibu vimesha fika
Nikamuuliza tena inamaana hii nyumba inavunjwa nae akanijibu ndio tuliagizwa na boss
Mara akaja mzee mmoja na briefcase kisha akamkabidhi mmoja wao na kuwaamuru kuwa huyu kijana mwangamizeni kwa haraka sana inavowezekana pale pale wote walinigeukia na huku wengine wakiwa na sepetu a.k.a spedi nyie mnaita na kuanza kunifuata nazo nikaona namna yakufanya hapa ni kukimbia tuu na sio njia nyingine
Baada ya kuona upenyo nilitoka spidi kali kama upepo wote pale walibaki tuu wakishangaa wasijue nimeenda wapi wakiwa wametulia bado wanafikiria nitakuwa nimeenda wapi ili wanifuate watimize kauli ya mkubwa wao
Mara ukaja upepo mkali sana eneo lote lilikuwa ni rangi ya vumbi tuu hii ni style ambayo niliisoma katika kile kitabu kidogo ambacho niliachiwa na mama ninapoagana nae mara ya mwisho kule kwenye lile jumba
Baada ya upepo kuvuma wengi walianza kujiziba usoni kuzuia vumbi
Hadi yule aliyepokea ile briefcase yenye hela alijisahau ile anageuka aangalie zile hela ile briefcase ndo kwanza akaona inazamia kwenye upande wa pili wa paa la nyumba hakuweza kuamini akataka apwayuke kwamba watu waingie mle ndani lakini kabla hajaongea chochote alitulizwa na ngumi yenye uzito kama tufe kisha akatua chini puu akiwa hana hata fahamu kitendo kile wengine nao walikiona baada ya hapo wakamwona ninja akiwa katokea upande ambao upepo ulikuwa umetokea hapohapo wote waklidamka na kuanza kusogelea silaha zao ambazo ni sepetu mapanga wenye spana walichukua spana zao na kujipanga ili wapambane nami sikakawia nilitoka na mwendo wa kasi huku nikiruka juu na kuzunguka nikaachia mateke kwa watu watatu mfululizo ambao walienda kuwasukuma na wenzao kama watatu tena. Baada ya hapo nikasimama kati ili mtanange uanze na hii siku nilishawapania wakijifanya wabishi sana nachinja mmoja wao ili uwafundishe na wengine.
Walianza kujongea huku wakizishika silaha zao kiufundi lakini mimi nilitoa tuu nyororo moja yenye goroli kibao na kuanza kucheza nayo, kila ambaye ilimpata alikuwa ni lazima akajifiche kwenye magari ya kazi niliwafunza wote hadi wote tayari wakawa wapo hoi kisha nikaongea kwa sauti fulani ya bezi la kulazimisha
      ONDOENI UCHAFU WENU TENA NISIWAONE KABISA KATIKA HILI ENEO kisha nilimshika mmoja na kumrusha kule
Katika hawa wote hakuna aliyeweza kugundua kama ni mimi mtoto wa MPL ndio ambaye nimefanya hivi maana wote waliamini mimi nilikimbia mapema kabla ya zari kumbe niliwapangilia.
Wakiwa wanaanda magari yao ili waondoke wakampe taarifa boss wao, mara waliona kwa mbali kuna gari linakuja, kwakuwa hata mimi hilo gari sikulitambua sikupoteza mda nilichumpa juu sana na kupotelea kusiko eleweka lakini ndio ilikuwa ndo njia ya mimi kuondoka pale------itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 15

Tulipoishia>>>>

------baada ya kuingia duka lililokuwa jiran nae aliweza kujieleza ili apatiwe msaada wa kupata simu ili apige nyumbani
Nani akuamini wewe na wakati unajua kabisa umeniona pale duka la simu ukanipiga kibega tena kwa maksudi na yule dada anakuambia ila ukajifanya unaleta maringo kana kwamba hela zako ndio zinazosumbua sana watu wote (aliongea vile yule dada ambaea alikuwa katika m pesa fulani kule mjini

Dadaangu nisamehe na mimi ni binadamu tuu kama ni simu nitalipa tuu ila naomba msaada huo nisaidie
Yaani hapa enock alikuwa mdogo ghafla tuu mana yeye hakuweza kuriri sura ya mtu ambae amemharibia simu yake. Baada ya kuomboleza sana ndio alipewa msaada wa kuongea na simu alimpigia baba ake nyumbani na kumwambia amevamiwa na kuporwa hela zote lakini simu tuu ndio imeachwa, kwakuwa alikuwa ni mtoto wa pekee kwa huyu mzee mda huohuo tuu ziliingia hela mpesa kwa namba ya yule dada kisha wakaitoa, enock alishukuru sana kwakuwa alisaidiwa, baada ya kuhesabu hela ambazo alikuwa akihitaji alichukuwa kiasi kama cha laki tano na kumkabidhi huyu dada ambae amemsaidia, kisha akasimamisha bodaboda ambayo alitaka imfikishe hadi eneo ambalo lilikuwa na gari yake, mambo yalipokamilika akapanda gari na kupitia sheli ili ajaze mafuta kisha akarudi nyumbani salama kabisa

_____kwa baba______
Wiki moja liliisha na wafanyakazi wote walikutana tena katika ofisi zao na kuendelea  na kazi zao kama kawaida. Ilipita muda kama wa mwezi mmoja hivi walitembelewa na baba mmoja ambae alijitambulisha kwa jina la Mkuti, akadai yeye ni mwekezaji hivo alikuwa anatafuta eneo ambalo ni zuri ili aweze kufanyia shughuli yake. Lakini katika mapendekezo yake akapendekeza eneo ambalo ni  karibia na nyumbani. Baba baada ya kusikia vile akamwambia kwa hilo eneo hata haitawezekana kabisa kwa sababu lile eneo ni dogo sana na pia lilishakuwa na mipango ambayo tayari imeshaanza kufanyiwa utekelezaji, kajaribu sehemu nyingine
Lakini yule mgeni kwa jina la mkuti akaonyesha kama hajaelewa kabisa kuhusu kuzuiliwa na maelezo hayo alichowajibu ni kwamba ataenda kuongea na watu wa serikali ili wamuangalizie kuhusu hilo eneo. Baada ya kuongea vile akaondoka hata hakuhitaji kuanza kukaa tena pale wasije wakaendelea kumzuia zaidi
Aliondoka na kwenda kutimiza kama alivoahidi pale kwenda kuongea na wakubwa ikiwezekana hata kwa hongo ili tuu apate anachokihitaji yeye. Baada ya kuongea nao walikubaliana vizuri kabisa kisha simu ikapigwa kwa baba kumpa zile taarifa za kukatwa kipande cha eneo lake, baba hakutaka kukubaliana nao kabisa lakini kwakuwa walisha kula hongo ya pesa ndefu wakaamua kutumia comand kwamba atake asitake ni lazima tuu eneo likatwe kisha simu ikakatwa hivo
Baba alibaki akijiuliza maswali mengi sana pale ofisini lakini hakupata jibu lolote akiwa ametulia simu yake ilianza kuita namba ngeni aliiangalia kwa kuwa alikuwa na mawazo sana akataka aikate lakini roho ikasita akaipokea
Akiwa amepokea akabaki ameduwaa asiamin kituanachokisikia kwenye simu ile,
Nini wewe bon uko wapi kwa sasa, ahaa basi njoo hadi ofisini kwangu kabisa, ya nipo ofisini ndiyo, ok nakungoja ukifika gonga tuu sekretari akakuleta hadi ndani
----duh bon kaondokaje kule tutajua tuu----

Baba akiwa amekaa ofisini kwake mara mlango ukagongwa
Yes karibu
Waooooooh alinyanyuka na kunikumbatia kwa furaha mana ni kama mwaka umeisha tangu tupotezane pale nyumbani. Ulikuwa ni mda wa furaha sana baba alisahau kama kunamtu ashamtibua mda si mrefu sana,
Baba aliondoka na mimi pale ofisini na kulekea nyumbani lakini tukiwa bado hatujafika nyumbani tupo njiani kuna gari lilikuja na kusimama mbele kisha akashuka jamaa mmoja ambae alionyesha sio mtu mwema hata kidogo. Alikuja hadi kwenye kioo cha gari ambalo sisi tupokisha akasema kwangu wewe dogo sogea kwanza namhitaji huyo  mzee kwanza ninashida nae. Lakini nikaleta ubishi kidogo kwa kumwuliza kwani kama unamfahamu  na unashidanae si bora ingamfata kwa busara tuu sio kumzuia hata asiende mbele,
Dogo acha shobo nimekwambia ninashida na huyo mzee wewe mbona shobo nyingi au wewe ndio powa shuka wewe basi ili nikupe shida yangu ambayo nahitaji huyu mzee aifanye.
Baada ya yeye kusema vile nikamwambia ok nashuka ili niikamilishe hiyo shida yako.

Niliufungua mlango wa gari na kushuka kwenye gari nae akanivutia hadi mbele ya gari ya gari lake baada ya kufika kule akasema sasa nakupa dawa ya shobo zako we siunajitia mwehu sana eeee sasa ngoja, baada ya kusema vile alikunja ngumi huku akijiandaa kunipiga tumboni, nikawa namwangalia tuu bila kuchelewa akanipiga ngumi ya kwanza ya tumbo lakini sikushtuka akapiga ya pili sikushtuka bado alitaka kupiga ya tatu niliudaka mkono wake na kuunyonga ikasikika tuu sauti (koooo) kilichofuatia hapo ni kilio. Nami sikupoteza mda nikarudi kwenye gari kisha nikarudisha nyuma kidogo na kuipisha ile gari yake hadi tunafika nyumbani. Tulifika na kufanya taratibu zote kisha tukala na kulala_____

_____katika ile nyumba ambayo anakaa bashir kulikuwa na mabishano makubwa sana ambapo bashir alikuwa kazongwa na wpangaji wote huku wakimpa vipondo tuu
   Dadeq zako kwa hiyo saizi umeamua uache zile bangi zako na huyu jamaa ungeendelea kuleta shobo zako za kike angekuua wewe eti street fighter jiite hvohvo na saizi.
kantangazeeeeee kweli kila mbabe na mbabe wake. Bashir umepoa kama unasubiri upulize pola, aliongea vile asha kisha amina akamdakia ivi wewe asha mbona na wewe shobo  nyingi kama umejigundua unashombo wakikunyonyoa tu kilio kama umekutana na popobawa, lione kwan
afu wewe shoga au bashir unakuwaga na promise nae mana kila siku ilaonekana kama unajisikia mbaya mno nikiongelea kumhusu kuwa wazi tuu manfongo wewe..
hheheee shoga tena unikome nini.
Hujasikia au ndo mideko. Ushuzi kweli wewe
Amina na asha walisimama na kushikana ilionyesha kwamba kila mmoja ameshindwa kuvumilia yale maneno waliyokuwa wakipeana. Hapakukalika kabisa katika hii nyumba kama kawaida ya wadada wanapopigana matusi ya nguoni ni kawaida timbwili lilitembea kwa mda wa dakika kumi kila mmoja akawa ameenda ndani kwake kwa hasira sana.
Bashir akiwa ameenda kwenye chumba cha bon akakuta mlango upo wazi alijaribu kugonga lakini hakuna aliye jibu wala kufungua mlango. Kwakuwa alikuwa na hasira sana na bon alifungua kwa tahadhali sana na kuingia ndani ambapo aliona kuna vitu vichache tuu mle ndani ilikuwa ni kitanda, godoro na mablanket na shuka zaidi ya hapo hakuna akajisemea leo huyu lazima ajute humu naondoka na kila kitu siachi hata kimoja.
Baada ya kuongea vile akagusa kitanda kwenye kona ili akikague kama kipo vizuri lakini anagusa tuu alipigwa na shoti ya umeme,kumbe ulikuwa ni mtego tuu umewekwa kwa yeyote atayefanya anataka kuingia mle ndani na kuondoka na kitu, bashir kuona vile alikata tamaa tena ya kutaka  kujua zaidi akashika mlango kwa umakini akauvuta na kutoka nje, anapotoka mlango ulirudi kwa kasi sana na kumbonda hadi alienda kutulia kichwa.
HAHAHAHAHAHAHA. HAHAHA BASHIR VIPI TENA., kumbe kile kitendo kuna jamaa walikaa nje pale walikishuhudia vizuri kabisa bila chenga. Baada ya hapo bashir aliondoka kwa lengo akamfunze adabu asha ambae anamdomo sana. Alifika hadi mlangoni kwa asha na kugonga baada ya kuona hafunguliwi alisukuma mlango kwa nguvu kisha------itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I (mimi ni nani)
Benchrys
No. 14

Tulipoishia>>>>

-----simu ilianza kuita nikaitazama ni nani lakini sikuweza kujua namba kwa maana ilikuwa ni ngeni machoni kwangu lakini niliipokea hivohivo, baada ya kuipokea zilisikika tuu sauti za makelele ya watu kibao.
Aaah msinizingue shit,. Kasha nikakata simu na kuanza kuondoka mdogo mdogo kuelekea kule nyumbani ambapo nilipanga____-

Katika uchochoro mmoja ivi kulikuwa na kikundi cha watu ambao walikuwa na mazungumzo yao :-
Aaaah kichaa waangu ivi huyo ngeni ni mtoto wa kahaba gani anae weza kuingilia tuu mitaa ya watu kiholela hivo
Ddduh man hata mimi sijampata hata jina lake ila acha tukamcheki mamake zake huyu, lazima niondoke na kiwiliwili chake nikaange homu kama kitimoto mana kitambo saaana
(kumbe walikuwa ni wavuta bangi ambapo katika hawa wavuta bangi na bashir alikuwa ni mmoja wao) baada ya kuongea saaana walijipanga kwa kuchukua silaha zao kama mapanga, nyembe, makwanja, wengine fimbo kama unavojua wavuta bangi wakisha panga kuleta vurugu. Baada ya hapo wakaanza safari na kiongozi wao alikuwa ni bashir ambae alishika jambia kama silaha yake

____- bon_ wakati naingia tuu pale nyumbani mdada alinifuata akijitambulisha huku hajaulizwa
Kakaangu mimi naitwa amina, mwenyeji wa hapa hapa samahani sijui wewe unaitwa nani mana kama majirani ni vyema kufahamiana vizuri
Niliona kama ananipotezea tuu mda wangu nikataka niondoke ili niingie ndani,. Jamani kaka angu acha dharau naongea na wewe.
Ahaaaa mawazo yapo mbali sana hapa umesemaje kwani, nilimuuliza kama sijasikia vile
Ilimpa wakati mgumu sana kuanza kuongea tena lakini akajikaza hivohivo, nimesema hivi-----kabla hajaongea simu yangu ilianza kuita tena, sikupoteza mda nikaipokea bila hata kuangalia ni nani ambae alikuwa anapiga kisha nikasikia sauti tokea upande wa pili nakuhitaji uje hapa nyumbani sasa hivi tena bila kuchelewa
Nilijua dhahiri kuwa hii ni sauti ya yule mzee kwenye jumba lile ambako nilipelekwa baada ya kutekwa. Niligundua kwakuwa nafahamu kuwa simu ninayo itumia ilikuwa ni ya mwanae aliiacha baada ya kwenda shuleni

Niliposikia amesema vile hata sikujibu chochote nikakata simu ile.
Enhee ulikuwa unasemaje nilimuuliza amina lakini hakujibu chochote na kuondoka spidi huku akiingia ndani kwake. Kumbe kile kikundi cha mateja tayari kilikuwa kishafika pale

Boya lenyewe ndio lipo wapi au umetuenjoi tuu hapa bashir onyesha fasta bhana ninahamu ya damu///aliongea teja mmoja kwa bashir ili bashir aonyeshe huyo aliye mpiga ni nani huo muda wote nilikuwa nimesimama tuu huku nikiwaangalia
Bashir nae hakusita kwa kutumia jambia lake akanyoosha kuelekea kwangu kwa maana mimi ndio mhusika wa tukio hili.
Yule teja kwa kimbelembele akajileta huku kashika upanga wake mkononi na kusema kijana piga simu ya kuaga kuwa wewe wakuandalie tuu kaburi kwa maana saiz wewe unaenda kuwa kitoweo changu nakupa dakika moja inatosha. Baada ya hapo akatoka kipisi cha karatasi ambacho ndani yake kuna bangi alikiwasha na kuvuta kisha akampa mwenzake ili nae apige pafu
Kisha akanigeukia tena./ muda umeisha kisha akanyanyua panga lake lakini anashusha tuu panga lilipigwa teke na kwenda kutua juu ya bati za nyumba ile kisha nikampiga makofi kama naadhibu mtoto. Baada ya hapo nilimpa ngumi ambayo ilimrudisha nyuma kidogo nikaongea na teke la tumbo alipepesuka na kwenda kuwasukuma wenzake kule walikosimama. Kudadeki zenu kwahiyo mmejituma kuja kufanya ujinga kama huo hapa eti. Nilikuwa naongea huku nikiwafuata waliko, nao kwakuwa walikuwa na silaha wakajiaminisha na kunyanyua silaha zao. Mmoja akajifanya kuleta shobo za kuwa wa kwanza kunipiga alipewa zawadi ya ngumi ya taya akaanguka chini huku akiwa kashika tu mdomo kwakuwa alikuwa ameshika fimbo niliinyanyua na kuanza kuwachezeshea muda wa dakika tano tuu ulitosha kuwakalisha wote chini. Nilipomaliza nilijaribu kupapasa macho yangu ili nimwone, lakini jitihada zangu hazikufanikiwa, sikumwona na wale mateja waliondoka na kupotelea wapi sijui

-------baba ivi simu yangu niliiweka humu ndani lakini siioni iko wapi maana nimetafuta sana na sijaiona (aliuliza mtoto wa mzee yule ambae waliniteka) e bwana wewe unalia na simu ya laki tano mimi niliibiwa milioni saba unaona kama unahaki ya kulia? Na kibaya simu yenyewe inapatika hebu ngoja nipige tena. Alinyanyua simu na kutafuta ile namba tena ili apige lakini haikuwa inapatikana
Kama ni line nilishasajili nyingine kuepusha usumbufu usiwepo kabisa kisha nikaifuta kila data zikiwemo account zake zote

Kama unavoona namba saizi haipatikani (aliongea baba ake)
Basi itabidi ninunue nyingine kesho, kwanini usiende sasa hivi nikupe hela kabisa, sawa nipe tuu naenda hata saizi. Basi mzee alisimama na kwenda ndani kisha akatoka na kitita cha hela kikiwa kimefunga na lababend (kama mnavosema) kisha kamkabidhi yule mwanae akanunulie simu, alipokea na kuondoka.

Katika duka moja tunamwona yule kijana wa mzee yule ameingia kununua simu mara akakumbana na dada Fulani na kuangusha simu ya yule dada ambapo simu ilianguka na kupasuka kioo lakini huyu dogo hata hakujari akapita na kuingia ndani. Lakini mhudumu kwakuwa aliona akamuuliza // wewe kaka mbona umeharibu simu ya yule dada lakini unajifanya kama huoni vile// ebwana ee wewe fuata kinachokuweka hapa huyo dada ndio kazi yako au unajifanya msamaria mwema wa kileo acha uboya nahitaji nokia lumia 850 hapo kama ipo.
Lakini yule mhudumu akakazania kwa kuendelea kuongea
//kakaangu acha dharau yule nae ni binadamu hujui saizi hapo tayari umemharibia hana mawasiliano tena?
Ivi wewe sista vipi mbona inaonekana hatuelewani kwahiyo simu inagharama gani ambazo wewe zinakupa uchungu namna hii, simu ipo haipo niambie niondoke aliongea kwa hasira sana yule dogo
// ok simu zipo nadhani gharama zake unazijua ni m ngapi
Wewe usijari kama hela ipo ya kutosha tuu nipe simu niiangalie nikiridhika nayo fwesh
./././mhudumu alitoa box moja la simu na kumkabidhi ili aweze kutazama. Dogo alilipokea kuangalia kisha akatoa kitita kizima cha hela zile na kumwambia hesabu zako nipe chenji zangu. Mhudumu. Alizipokea na kuhesabu huku akiwa na lengo la kumkomoa alihesabu zinazotakiwa kisha akahesabu za simu ya yule dada kisha akakamrudishia chench ambayo ilikuwa ni laki tisa na themanini na kumwandikia risiti.
Unaitwa nani mteja
Naitwa enock mlanje. Alijibu hivo kisha yule mhudumu akaandka jina kwenye risiti lakini kwenye kiasi cha hela akaandka in u$ dollah kisha akamkabidhi.
Karibu sana. Enock aliondoka kwa furaha asijue kuwa kaibiwa.,
Enock akiwa njiani kuna gari moja jeusi lilikuja na kusimama mbele yake kisha muda wa dakika tuu kadakwa na kuingizwa ndani ya gari lile ambayo ilienda kumwacha katika viunga vya posta. Enock alishuka ndani ya gari huku akiwa analia sana huku akiwaza gari lake alilokuja lipo mbali na kama simu bado ni mpya hawezi kutumia kufanya chochote ila akawaza aingie kwenye duka moja ili apate msaada-------itaendeleaaaaaa

Jumapili, 16 Oktoba 2016