Ijumaa, 5 Agosti 2016

de 9

Gangstar noma
By: benchrys
9
......Jane unaundugu nae au ndo tabia  zenu za ajabu hapa skul, madam aliniuliza hili swali hadi nikajifikiria hivi madam hadi anauliza swali kama hili kawaza nini ila sikuwa na chaguo ilinibidi nimjibu tuu. Hapana madam sina uhusiano nae wowote isipokuwa tuu.... Enhee kitu gani madam alidakia kabla sijamalizia hapo na mimi akili yangu iligutuka ikajibadili fasta mana niazimia kuwa nitamweleza kwanini tupo jirani ila alipodakia nikamjibu shotcut kuwa ndo mana nilikwambia kwenye meseji kuwa nitakueleza shuleni na wewe shuleni hujaja mimi ningekuelezaje haya panga siku nyingine ya kukutana ili nikueleze, madam akajibu wewe mimi kukuamini inaeza kuwa ngumu kidogo maana naona wewe ni kama janja moja hatari so kunidanganya hutaona kama kitu kigumu sana kwako..Ahaa nawewe usiponiamini powa tuu mana mnaona kama sisi tulizaliwa tunadanganya mimi nimekwambia panga wakati wa kukueleza hupangi unanipa tuu hali ya kujiona mimi ni mwongo so nikikueleza utaamini kipi sasa kama mapema hivi hutaki kuniamini halafu umeagizwa na mwalimu wa nidhamu au ni uamuzi wako tuu..Hili swali lilimfanya madam atulie kidogo hadi nikahisi kakata simu ile
Hallo,hallo,hallo nilisema hivo mara tatu bila kuitikiwa nikatoa simu sikioni ili niangalie kama tayari ishakata nilipoangalia nikagundua kuwa bado ipo hewani tuu nikairudisha tena sikioni,,, madam alivuta pumzi kwa nguvu kwa nguvu kama mtu aliyewekewa kisu shingoni kisha kikatolewa tena kwamba amenusurika kifo Kisha akaendelea kuongea ivi ben kumbe ambavo mimi najiona sikuamini kumbe na wewe huni amini pia ivi....Kabla hajamalizia kuongea nikadakia kuwaamini nyie ni ngumu sana lakini mbona hujajibu swali la, nilirudia tena kuuliza lile swali la mwanzo halafu nikauliza samani lakini au unashuguli nyingi ndo maana ukaweka simu na kuitulizia kisha ukavuta pumzi kuonyesha umechoka? naona ni bora ungefanya kwanza kazi ndipo unitafute au unaonaje,, madam akanijibu baadae sitakuwa na dakika for sure but i think we will chat au unasemaje madam alisema hivo nikamwambia kwa leo sina kifurushi chochote wala salio kwahiyo itakuwa ni ngumu kuchat, niliongea hivo huku nikijua kabisa kuwa nadanganya kisha akaniuliza halaf ben mbona whatsapp sikuoni na wakati unasimu yenye uwezo wa kuwa na vitu hivyo vyote nikamjibu kwamba siwezi kujiunga na pia hata nijiunga walimu nyie ni lazima muanze kuninyanyasa mana sijui mnaroho gani nyie hadi sometime siwasomi yani hapana wewe jiunge mwalimu atakae kujadili tuu nitajua mimi cha kujibu.........Hadi hapa tulipofikia kwa haya maongezi kati yangu na madam nilikuwa tuu najiuliza mbona huyu madam leo simsomi dakika 37 anaongea tuu na mwanafunzi wake inamaana hawamtafuti watu kwenye simu yake au nlikuwa nikijadili hayo Wakati tukiendelea kuongea nimwambia sorry naomba nikabadili kwanza nguo za shule akaitikia akasema sawa ben ila ntakutumia vocha ili ujiunge whatsapp sawa ee baadae mpendwa eee! ilinichukua mda kidogo kujibu yale maneno kwa uvivu nikamwambia ok kwaheli nayeye akaitikia kwa sauti kama mtu mwenye dalili ya kulia hivi sawa benii badaee....
    Hivi ben ulikuwa unaongea na nani tunapiga simu ipo bize tuu karibia saa sasa mda wote huo mtu unaongea tuu duh watoto wa sikuhizi ni shida tupu sijui mnamatatizo yaani hadi kazi iliyotakiwa tuifanye pamoja tumesha maliza sawa boss wetu..Samahani tuu nilikuwa naongea na mwalimu tuu akawaananipa maelekezo na ndio mana tumeongea mda mrefu. Nilimjibu hiyo mama baada ya kuniuliza na kunambia vile kisha nikauliza hakuna kazi nyingine ya kwangu niimalizie.. Nimekwambia tushamaliza
****Duuuuuuh we ben huyu madam linda na wewe inakuaje tena anakutaka nini.. Halaf naomi tuheshimiane sawa maneno gan hayo sasa ananitaka kwani mi msosi au ni ajira ambapo atahitaji salary kutoka kwangu kwanza kwanini uniulize swali kama hili. wakati Huo yeye alikuwa kashika simu yangu, ok umesema kwanini nimekuuliza hivi chukua hichi kidude vaa sikioni halaf ningojee mda huo nilikuwa nimevaa prova kama wenyewe mnasemaga kwahiyo kile kidude nilkivaa yeye akiwa kashika simu yangu sijui alifanya nini nikaanza kusikia yale maongezi niliyokuwa nikiongea na madam kwanza nilishituka nikamuuliza hichi ni kinini akanijibu inaitwa bluetooth, na haya maongezi yameingiaje humu akanijibu mbona yapo kwenye simu yako sijataka niweke sauti juu wasije wakasikia na wengine hapa halaf iwe noma kwako ben. Nikasema inamaana simu yangu inarekodi mnapoongea au akanijibu ndio hivo duuuuuh huu kumbe upuuzi wa hali ya juu aisee
    Tukiwa tunaendelea kuongea na naomi iliingia meseji, ben meseji yako hii bhana ee ifungue tuu kwani kunatatizo! akaifungua kisha akataka kucheka kwa ngumu akatulia baada ya kusikia mlango ndani unafunguliwa alikuwa ni baba anatoka sebuleni mana mda huo wote sisi tulikaa kwenye msingi wa nyumba yetu nyinyi mnaitaga kiti ilikurahisisha lugha....Naona mnabadilishana mawazo safi sana hivo ndio inafaa sio kila mtu anaishi nyumbani hapa kipekeake tuu. Aliongea hivo baba kisha akauliza kwa naomi 'naomi nawewe unasimu au? hapana baba sina pole naona ben anasumbua tuu ngoja niwape wote unapenda ipi akajibu hata ikiwa kama ya hii ya ben ntafurahi tuu, baba akajibu ok safi baba alionekana ni mtu mwenye furaha ile jion. Ben mi natoka mara moja sasa hivi narudi hata geti msifunge.. Haikupita mda akarudi akiwa na box la simu aina samsung garaxy kama ambayo mimi naitumia akasema ben jee utafurahi naomi akiwa na simu kama yako nikamjibu nimefurahi ndiyo baba wote tulinyanyuka na kumkumbatia baba baba akasema chukua utamchajia mwenzio unakumbka yako nlikwambia uchaji masaa mangapi ndio si ni masaa sita baba akasema kumbe unakumbuka safi sana.....Itaendeleaaaaaaa

Jumatano, 3 Agosti 2016

De 8

Gangstar noma
By: benchrys
8
....ngongongo, ngongongo oya fungua mlango vipi wewe,, aah bhana ee nimelala mimi sitaki kusumbuana naomba uondoke. Mlango wangu ulikuwa ukigongwa kwakuwa nilikuwa sihitaji usumbufu sikuufungua ili isije ikatokea na kesho nichelewe shule kama ilivokuwa hii siku.......
  Wengine wakiwa sebuleni pale ule usiku,, kumbe ben nae ni mwoga daah yaan ameenda kulala mapema eti kisa kesho asije chelewa kama leo ila sio mbaya asafishe hata jina lake kuwa amewahi kulala,
Asafishe jina wapi ben akili yake inamtosha yeye pekeake tuu wengine hata hamuiwezi ni bora mkamwacha tu ila habari ya kusafisha jina hilo swala gumu mana utampa heko leo halafu kesho lisha haribu. Walikuwa wakijadili hayo pale sebuleni wakati nipo chumbani kwangu waliongea wakawa wamesitisha ile mada
'hivi mimi mwenzeni ule mda tumetaka kuvamiwa ilionekana ben kama kuna mtu alikuwa akichati nae na kumpatia plani zile zote na ndio maana polisi wakapata urahisi katika kuwakamata wale majambazi mi hapa mpaka sahizi ninajiuliza ni nani rafiki yake anaejua plani zile za kushujaa mana yeye anadai rafiki yake ni joel tuu huyo joel kajifunza wapi hizo njia,,,lilikuwa ni swali ambali liliulizwa na mama ambapo lilifanya pale wote waliokuwa wamekaa wali hukuchukulie uzito kwa namna fulani licha ya kuwa hawakupata majibu yaliyosahihi..
Au atakuwa na rafiki yake tofauti na joel ambae ashawahi kuvamiwa ndio akatumia hio njia kuwakamata
**** ben nikiwa nimelala nikawa naota wale wote waliokamatwa washarudi nyumbani kwetu kwa lengo lipi sijui wamatokaje? Na kama waneachiliwa ni kwa misingi ipi""" oya wewe dogo nadhani ndiye uliyefanya mpango hadi tumedakwa alivoongea tuu akachomoa kitu fulani kama kiboko hivi kutaka abitandike nacho ila ananyanyua juu na kutaka kushusha mwilini mwangu ben nilijizingusha mithili ya paka aliyedondoshwa kutoka juu anakaeibia kufika chini kisha kwa haraka  ikapokonya ila fimbo yeye baada ya kuona vile akatikisa kichwa na kusema kwahiyo leo unataka kujitia wewe ni mkorea ambae mwili wake ni kama puto subiri ngoja nikuonyoshe we si ninja ee hapo akachomoa kisu akawa ananisogelea lengo anichome na kile kisu duu kikweli ben nilikuwa nina nguvu hadi mimi nilijishangaa kuona napambana na watu  kama  ni mpiganaji wa vita uwanjani, aliposogea na kisu nikazunguka kama upepo ghafla akahikuta ashapokinywa kile kisu halafu nimemwekea yeye kooni hapo ndipo akaanza kutetemeka na kuomba msamaha,,
Tafadhali naomba usiniue!!! alisema mana nilimtaiti kana kwamba akitikisika tu basi ncha ya kisu itakuwa ishazama kwenye shingo yake..ok unasema nisikuue labda nitake kujua huyo unaemtafuta kibaya alichokufanyia wewe ni nini
Hakukuku    ku na kibahya alichonifanyia sasa.
Sasa tatizo lako wewe kwake ni nini? Hapana nisamehe sitamuwinda tena......nilimwachilia akaondoka spidi kali kama mwizi kaiona chochoro ambayo haina mtu.
Nikiwa nimekaa nikaona kundi la vijana linakuja wakiwa na mapanga fulani yaliyo nolewa hadi yanang'aa nikajua hili ni kundi la yule jamaa tu sio watu wengine nikaingia ndani haraka na kuulock mlango kisha nikachukua manati na golori na kupandisha kwenye mlango wa dharura ambao upo juu ya dari na kuvuta kipande cha bati ili nitoke nje,, nilipotoka nilienda mbali kidogo nikashika golori na kuweka kwenye manati ile na kumkadiria mmoja wao sehemu ya mgongo katikati ilipompiga akabaki anagaragara kama mtoto chini wote wakaona hii ishakuwa shida wakaondoka na mimi nilitumia njia ile ile kurudi ndani na kuhifadhi manati kisha nikafungua mlango wangu baada ya hapo nikaona haina haja ya kukaa nje nikaenda sebuleni nikiwa nimekaa simu yangu ilianza kuita..
**** dah kumbe nilikuwa katika ndoto nasimu ndio iliyoniamsha hadi nimeshituka na ndoto iliisha kwa staili hiyo usiku huu niliuona kama ni mfupi kwangu mana kulala nlichelewa halafu ndoto niliyoiota sio ya kufariji hata kidogo...
    Ilipofika asubuhi niliamka kama kawaida na kumkuta naomi alishaamka ameandaa hadi kifungua kinywa.
Habari za athubui naomi nilimsalimia hivo. Powa nzuri tuu leo umeamka na kithembe au hahaha acha hizo nani anakithembe bhana mbona nimeongea vidhuri tyu au nakosea kutamka maneno.....nilikuwa nikifanya makusudi kuongea vile....hapana hujajosea, sasa mbona unasema nina kithembe mi sio fani yangu kuwa na kithembe.... Hahaha nawe acha utani kuwa mtu ambae fani ya kuwa na kithembe kunywaga chai uwahi skuli tuu....haya powa ngoja nikanawe kwanza kisha ndio ninywe chai.
    Woah!!!!!! Uko vizuri chai hii kutafuno kama isingenibidi niwabakizie wengine walai ningeifuta tuu maana tame enhee..... Ok basi powa mi naenda shule bhana badae nikiwa nataka kuondoka.. We ben,   naam ivii.... Au basi ntakuuliza badae tuu saizi nenda shule. Niliondoka kuelekea shuleni nilipofika kitu cha kwanza niliipata namba yangu halafu nakaanza kupepesa macho kumtafuta madam linda mahali alipo sikumwona ikabidi niulize kwa wenzangu kama wamemwona..... Aaaaaa ben ee acha utani madam mineno asubuhi yote hii unamtaka wa nini kama alikupa homework unaeza kumpelekea hata badae, niliwasikiliza hivohivo kisha nikasitisha lile ziezi la kumtafuta mda wa kuingia darasani ulifika ila bado sikumwona nikaanza kujiuliza inamaana leo hajaja anaumwa au maana hata taarifa sijapata na wakati ananamba yangu ila siyo shida sana, hali ilikuwa hivo hadi ulipofika mda wa kurudi nyumbani nikiwa naniandaa kuondoka akaja godson mpambe na mbea wa darasa letu
    Ehee FASEBOOK nambie unataka ukatoe taarifa gani tena mana leo umenifata mimi hapa sio bure tu haya nambie.. Duh kumbe god lile jina ambalo nilimwita hakulipenda akasema. Ben kudadeki nakuheshimu sana nani ni facebook hapa haha eti nani facebook we kazi yako sikutoa taarifa tuu kama facebook ukicomplain powa haya nipe shida yako god akajitia kuleta kiburi akaondoka kwa hasira anapoondoka nikamtupia tena  oya shauri yako sikuhizi hadi mwanamke mwenyewe hatubembelezi sembese wewe boya nani akubembeleze tembea p****y wewe
    Nikaendelea na safari ya kwenda home siku niliiona kama ya ajabu mana hata joel sikuongea nae hadi naondoka kurudi nyumbani nilipofika nyumbani kabla ya vyote nilitaka kuchukua simu na kutafuta madam ila nilipoichukua ndio nikagundua nilitafutwa vya kutosha kulikuwa na missed call 12 message 15... Nikishakula nitazisoma zote sio saizi nikaingia ndani nilibadili nguo na kurudi ili nile nikiwa naendelea kula simu yangu ilikuwa ikiita nikainyanyua ndipo niligundua alikuwa ni madam nikaipokea.... Shik.... Mambo ben. Nilikuwa nikitaka kusalimia shikamoo nikatulizwa na salamu yake ambayo ilikuwa na ujazo wa namna yake... Halafu akaendelea kuongea ben, ndio mimi ben unasemaje. Halaf ben usinijibu hivo mimi mwalimu wako sawa, sawa niliitikia kisha yeye akaendelea nilikuwa nataka nikuulize hivi........ Itandeleaaaaaaaaaaaaaa

benchrys.blogspot.com

Jumatatu, 1 Agosti 2016

De 7

Gangstar noma
By: benchrys
7
...baada ya kupiga picha nilihisi kama yule jamaa anadalili za kugeuka hapo na mimi nikatuna lengo nisigundulike kitu ambacho nimekifanya mana laiti angejua kuna nimempiga ile picha basi ingekuwa hatari kama sio hata mtaani pasingetosha maana hakuna mtu m baya yeyote ambae anapenda siri zake zivuje na vitu kama hiyo miguu ya kuku aka pisto hatakama unamiliki inatakiwa asione mtu yeyote kwa maana hiyo yeye ni kwamba alikuwa kafanya kosa kuiweka vibaya hadi sisi tuliiona, Hapo akawa tayari ameshatoka hadi nje ya geti la nyumba yetu hapo na sisi tukawa kidogo tupo sawa mana wasiwasi ilikuwa kama @kigeuka haraka na kutufyatulia hizo risasi....
  Tukaendelee na mambo mengine mana hii ni mida ya kula giza hili tayari lisha ingia. Alisema mama tukiwa pale nje nakuanza kuondoka ndipo na mimi nikaelekea sebuleni hadi pale nilipoiweka simu yangu nikaangalie ile meseji ambayo sikuimalizia kusoma lakini cha kushangaza nilipofika pale nilipo iweka simu yangu sikuikuta kwa haraka nikahisi au Naomi kaichikua!!! Kama kaichukua anafanya nayo nini simu yangu. Ni baadhi ya maswali niliyo jiuliza bila jibu "Naomiiiiii upo wapi" hee we ben kuna tatzo au alisema hivo mama baada nimemuita naomi kwa sauti ya juu sana nahisi sauti ilisikika hadi nyumba ya tatu maana nilijivuta sana kuita hilo jina.. Hapana mama hamna tatizo ila nilitaka tuu nimwulize simu kama yupo nayo nikiwa naendelea kuongea naomi nae alikuwa akija huku kashika simu mkononi kidogo nimwuulize ulikuwa kufanya nayo nini ila kabla sijauliza yeye alianza kuongea kwamba ulipoitwa na mama nilichungulia kupitia dirisha nikamwona yule kaka nikajisemea lazima niwe na ushahidi hata wa picha lakini kuwafata hapo nje ikawa ngumu lakini nilipoangalia kwenye kiti ndipo nikaiona simu yako sikujali ulikuwa unafanya nayo nini nikaichukua na kuingia kwenye camera ili nimpige picha huyo mkaka aliyekuw hapo nje samahani kama nimekuudhi ben.. Na mimi baada kusikia kuwa alichukua ili apige picha nikasema ok basi kama lilikuwa ndio lengo lako powa hamna tatizo nione hizo picha ulizo piga au hujapiga. Naomi akajibu picha nimechukua moja tuu ila nimechukua video iangalie hiyo hapo, akanikabidhi simu ndipo nikaangalia ile video aliyochukua 'kumbe unaakili safi sana gud' nikajikuta nampongeza tuu. Mda wote huo mama nae alikuwa akicheki kinachojiri nae alipoangalia akasema kumbe sisi tungeacha tu
(Usiogope mimi ni mwalimu wako linda na nilikuwa nakuomba kesho unapotoka shule wanafunzi wakitawanyishwa tukutane ofisini kwangu usianze kushangaa sana wala usijiulize wapi nimepata namba yako hayo yote niulize hiyo kesho, kingine sihitaji umshirikishe rafiki rafiki yako jane kuhusu hili Ombi nikutakie usiku mwema BEN)  <ni meseji ambayo nilianza kuisoma mama akaniita kumbe alikuwa ni madam linda sikujua namba yangu kaipata wapi ila alieleza kwamba kama kumwuliza niulize hiyo kesho siku ya ijumaa baada ya wanafunzi kutawanyika lakini nikahisi ni yule god Mwanaume kipele wa dasara letu nilipokuwa sijajua tabia yake nilimpa namba yangu ya simu maana aliniomba kwaajili ya mawasiliano..
   Mama na baba wakiwa sebuleni mimi nilikuwa nje sikutaka kukaa ndani kuepuka usumbufu ila nilipoulizwa nilidai kwamba mtandao wa internet humu ndani unasumbua lakini baada dakika kadhaa nikahisi kama kuna mtu amebifwata nje nilkokuwa nikageuka mwili mzima kuangalia nilimwona naomi akiwa anasogea nilipo nikajifanya kama sijamwona hapo akaita kwa sauti ya chini ben nnaswali naomba kuuliza, niulize sawa mbona upo nje mda huu unaumwa au, hapana mimi siumwi, sa kama huumwi mi naona bora ukajumuike na sie wenzio ndani twende,,,,, aaah bhana ee we nenda nitakuja sasa hivi, ok ila nnaswali jingine ila utanisamehe, sio shida we uliza tuu. Sawa powa ivi wewe na madam linda mna...... Ile kabda hajamalizia kuuliza hili swali ambalo sikulielewa tulihisi kama kuna kishindo kizito pale getini halafu na punze za mchanga zilituangukia wote tuliingia ndani kwa spidi kama robot zimeagizwa kuua vile baba akauliza huko nje inakuaje mbona kama kuna vishindo navisikia alitaka kutoka nje nikamzuia baada ya mda zilisikika kama sauti za watu uwanjani duuh nikasema leo tumevamiwa hapo ndipo nilipohitaji msaada wa linda yule madam nilinyanyua simu na kureplay ile meseji kwamba sawa nimekuelewa ila naomba utume upige simu polisi waje hapa nyumbani tunavamiwa kisha nikaituma ilipopokelewa tuu simu yangu ilianza kuita bahati nzuri niliiwekea silent mode ilikuwa ikiita bila sauti sikuipokea bali nilikata na kutuma meseji kuwa usipige tafadhali hiyo meseji nayo ilipopokelewa ndipo akarudisha kwamba nimeshatoa taarifa nyie zimeni taa za nyumba nzima tena anzeni na taa za ndani nikafanya hivo wale waliokuwa nje yaani majambazi walianza kujibizana kuwa hawa jamaa mbona wanazima taa msimu wenyewe ndio huu cheki ilivokuwa giza mishen yetu itaharibika hapa mimi niliposikiliza zile sauti zao niliigundua kuwa na yule aliyekuja jioni nae yupo tena inaonyesha yeye alikuwa kiongozi wao mana alikuwa akiwaanlisha sana wenzake
Mda kidogo ikaingia tena meseji ya madam kuwa mkiona tuu polisi washaingia washeni taa za nje tuu nikamjibu powa madam

*****nikiwa sehemu yenye switch ya taa za nje tu nikaona licha ni kwa umbali sana kama taa kwenye usawa wa geti mara sauti mpo chini ya ulinzi hapohapo mlipo Atakaekimbia ndio amekwisha. Ilikuwa ni sauti ya askari mmoja na mimi nilipojua kuwa polisi wamefika nikawasha taa za nje zote mda mchache wale majambazi wakawa wameshafungwa pingu wote kwa pamoja. Mimi nikajisemea afadhali saizi ndio kwanza nikalale mana hapa roho ilikuwa juu juu.. Hapo gari la polisi kwa jina la TENGA huku wanaita hivo sijui kwingine mnasemaje lilikuwa tayari lisha ondoka na wale majambaz....
   We ben aliita mama jina langu, naam mama umesema unaenda kulala?? Ndio mimi naenda kulala, unaenda kulala! Leo umekula wapi mwenzetu. Haaa hivi kumbe sijala nilisahau kuwa sijala kweli mimi ni jinga looooh!! hapo ikawa kazi moja kutafuta pot ilinijue msiso ulikonikiuona niukomeshe kwanini nimeusahau ingali nautaka bado kabla sijauona wakasema na nyama umalize nikawajibu mlijuaje thijui..nikawa nishaliona pot lenye chakula na mboga nikagundua hapa ni wali na nyama ya ng'ombe furaha yangu yote ndipo ilipoisha mana hii nyama siitumii
   We mbona mboga umeacha au imechacha, amna haijachacha, saa kwanini huli au haijaiva niliona ananizubaisha tu nilimwambia ngoje nishibe nilikatazwa kuongea ninapokula sorry naomi aha powa
   Nilipomaliza kula sikutaka kuongea na mtu yeyote niliishika simu na kutuma meseji kwa madam linda kwaajili ya kumshukuru kwa msaada wake kisha nikaingia kulala ili niitafute siku ya kesho nikiwa nimelala......itaendeleaaaaaaa

benchrys.blogspot.com