Jumamosi, 23 Julai 2016

nguzo ya duniA

���������� ������ ������������

-Tumia dakika chache kufanya uamuzi na siku nyingi kufanya utafiti.Wanaume wengi wanaongoza kwa kuhonga huwa na mkono mfupi wa kuhudumia familia zao pamoja na kuwajali wazazi wao.
Ni kazi rahisi kumkuta mwanaume anakunywa pombe bar ya Tsh 200,000/siku mmoja na mama yake mzazi ana pair mbili za kitenge bila kusahau wazazi hawana uwezo hata wa kununua Kg ya nyama,ila ni kazi rahisi sana kumpangia mwanamke kimada chumba na kumnunulia gari kimada wakati ada ya mwanao hauwezi kulipia.
Nitajie mtu anayemtolea Mungu fungu la kumi ambaye hana mafanikio katika maisha yake ? Nionyeshe kijana yeyote ambaye huwatumia wazazi wake pesa za matumizi ya nyumbani ambaye hajastawi katika maisha bora na yenye tija ?Kila palipo na baraka ya wazazi pana hazina ya mafanikio daima.
Jitahidi mara nyingi kuwapa wazazi faraja ili wakunenee maneno yenye baraka na hazina ya furaha yako katika maisha yako.Manung'uniko huleta laana katika maisha ya mwandamu na maneno ya baraka huleta mafanikio katika maisha .Ni wakati sahihi wa kuwapa faraja wazazi wetu kwa upendo na asilimia chache ya tukipatacho ili maisha yetu yawe na baraka.
Mama unaweza ukamtumia doti mbili za khanga na akakuombea dua na baraka kwa mwenyezi Mungu ila unaweza kumnunulia kimada wako IPhone 6 na akakuomba tena umnunulie na airtime pamoja na Brazilian Wig,sababu wamejaa laana na ndio wanaovunja ndoa za watu kila uchwao.
Kama upo kwenye ndoa basi hakikisha unapata baraka toka kwa mwanamke bora ambaye ni mkeo sababu yeye ndio kila kitu katika maisha yako kisha unapata baraka za wazazi sababu ndio nguzo bora ya maisha yako.
One of the greatest titles in the world is parent, and one of the biggest blessings in the world is to have parents to call mom and dad. #LoveIs___My____Religious
Credits: benchrys.blogspot.com

de 4

Gangstar noma
By: benchrys
4
...Usishtuke sana bro vipi wewe kumbe mwoga hivo
mbona jana nilikuona bonge la shujaa moja ambae naweza kumfananisha hata na johnsina mana ulifanya kazi ngumu tena inayohitaji akili mana ungecheza vibaya tu basi na wewe ungeunganishwa kwenye kibano, aliongea maneno hayo Naomi baada ya mimi kutoa mshituko mkali nilipoona mlangoni kwangu kuna mazaga mengi ya usafi mana nikijicheki bado nina akili zangu za usiku kiukweli nilishituka hadi nikafunga mlango wangu tena na kutaka kuludi kulala dahh kweli akili za usiku hazifai ila ambacho niliona so ni pale aliponipa dongo kuwa mimi ni mwoga hivo sikulipenda lile neno basi ndio hivo nikatulia tu....Muda huo wazazi walikuwa bado hawaamka ama kweli jana tulichelewa kulala nilijisemea kwenye nafsi yangu....
   Ben vipi mbona huu muda bado upo hapa nyumbani inakuwaje au shule ndio imefunga tena kwako tuu mana leo nashangaa kukuona hapa nyumbani,,, mbona hunijibu ivi sinime taja kwamaana naongea na wewe hizo ni zarau au. Haya yalikuwa ni maneno ya mama baada ya kuamka na kunikuta bado  mimi nipo pale nyumbani ilikuwa ni saa tatu kasoro na muda kuingia darasani na kuanza vipindi ni saa 8:00 kwa hiyo nilikuwa tayari nishachelewa tayari mama akasema shule lazima uende na wala huwezi shinda hapa kajiandae haraka'
   Dah leo mwanetu umechelewa kiNoma au ndo ushaanza na majukumu huko home kwenu saa tatu ndio unafika skuli kama ushadata we sema...Joel aliongea maneno ambapo nae kwakuwa nilizinguana nae jana halafu tena leo ananipa maneno ya kashfa namna hii sikumjibu kitu chochote ila baada ya muda kidogo nilikaa na kuwaza kuwa haya maisha tuu "no one is perfect" nikajikuta tuu nikitamka hilo neno la kimombo pekeyangu ndipo nikajizindua kama nilikuwa katika maeneo mengine kabisa na pale darasani mana toka nyumbani ni kama nimeharakishwa mkiki mkiki hapo ndipo nikajinyanyua na kumjibu joel,,,,,dah mwanangu we acha tuu usione nimechewa hivi leo kuja skuli mi jana ilikuwa ni majanga tuu. Joel akadakia kuna nini tena kilikupata joh langu mana ulipofika hata hukunicall au hukuwa na bando mzeiya. Awee niachie kashfa hizo bhana kisa nini mpaka nisiwe na bando et sema jana nimeupa faida mtandao tuu....yaani nilipofika darasani zikawa ni stori tuu nikasahau kuwa mwenzangu alikuwa darasani toka muda mrefu na mimi ndio kwanza hata kipindi kimoja sijahudhuria mi nikaendelea na stori,, unajua nini mwanangu ile jana pale nilipoachana wewe siuliona nimeondoka kama chizi hivi pale mshua alipiga simu ya kuniita home lakini napita kona hivi nikasikia sauti ya dada akipiga kelele za kuomba msaada sikuwa na noma kwenda kupiga chabo nikaona boya moja sijui lilikuwa linataka kupiga mtungo au mi nikaokota mawe na kulipiga nayo lilipotua chini tuu nikamnyakua yule dada na kuanza kusepa kabla haijawa noma;; nilikuwa nikimwelezea hivyo jamaa yangu joel. Joel , dah kweli ulikutana na zali ila bora kama ulimwokoa na bora kama ulienda nae homu kwa usalama wenu..Ndio tulifika hadi homu licha ya kuwa barabarani ilikuwa jau bado mana kulikuwa na boya lingine linatukimbiza ila nalo nililidhibiti kwa jiwe moja tuu likatokomea ila kufika homu ilikuwa fresh
    Ben samahani nina swali nataka nikuulize samahani lakini kama hutojali...nilipoona jina langu limetajwa kuwa kuna swali isitoshe ni sauti ya kike roho yangu ikanipa majibu bila hata kusikia swali lenyewe, moyoni nikajisemea kudadeki wenye mapepo ya unafiki nao washaanza sasa ngoja nimsikilize halafu aniharibie siku yangu hapo ndipo atanijua vizuri hata kama sipendagi bifu na watu...Ok wewe unataka kuuliza swali gani na wakati unajua mimi hata kipindi kimoja hapa sijakipata bado nyie mshasoma ndo mana mnatuletea sisi wengine mambi ajabu ajabu hapa nakupa dakika mbili tuu uliza hilo swali ila isiwe ni swali la masomo mana nitaamsha mapepo yangu...Niliongea maneno hayo  baada ya kuona sura ya m baya wangu ndiye mwenye shida ya kuuliza lile swali alikuwa ni msichana kwa jina la Jane ambae nilikuwa sihitaji kuongea nae hata kwa bahati mbaya hata pale nikubali kuongea nae kwa sababu Joel jamaa yangu aliniambia nimpunguzie jazba na nimsikilize tuu kilichofanya huyu dada nimchukie ni siku moja nikiwa darasani kichwa changu hiyo siku sijui kilitembelewa na wadudu gani maana kilikuwa kinaniuma tena sana katika orodha ya watu wasumbufu ikaonekana na mimi ni mmoja wao licha ya kuwa nilkuwa mgonjwa lakini nilipokea adhabu ambayo walisema wanafidia kwa wanaosumbua siku zote adhabu ilikuwa ni kubwa tena ni viboko pamoja na kazi za nje nilifanya hadi natamani kulia mana hata huyo mwalimu nilipojaribu kumwambia kuwa mimi naumwa hakuweza kunielewa hata kidogo ilkuwa ni kama siku ya kunikomesha shule nilijihisi kama bora niwambie wanifukuzishe shule mana huu  ni utumwa sitaweza kuuvumilia hata dini yetu inasema samehe 7x70 niliona kama hawajui lolote ila basi kamakawaida mimi ni mtu wa kujifariji daily nilifanya ile adhabu hadk namaliza lakini kwa kinyongo sana......
***Nimesikia hapo na rafiki yako mnasema kwamba kuna mtu ulimwoKoa jana nilitaka kujua anaitwa nani kama uliuliza hata jina lake mana mimi nyumbani nina dada yangu jana hajarudi na tumejitahidi kumtafuta ila hatujafanikiwa kumpata hata yaliyo mkuta hatujui mana alikuwa akienda kutafuta mahitaji kwaajili ya usiku, naomba unitajie jina tuu licha ya kuwa najua kuwa inanichukia toka kipindi lakini na mimi sikuwa mimi nadhani ni utoto nao unachangia samahani ben.aliongea maneno hayo jane tena msikitiko mkubwa nilipata roho ya kumsamehe lakini roho na mdomo vilikuwa ni vitu viwili tofauti kabisa maana moyo ulitoa majibu mazuri ila katika kuyafikisha kwa mhusika ikawa ni vingine kabisa,,,kwahiyo ukiwa na shida kubwa ndio unakumbuka kuwa kuna mtu ulishawahi kumkosea huo utoto unaosema ulichangia mchango wake ulifikia sh. ngapi mana mi hata sikuusikia huo mchango, nilimjibu hivyo jane kwasababu nikikumbuka adhabu ile ya siku ile laiti angekuwa yeye angeweza zimia lakini mwanaume nilikomaa. Hivi unafahamu kwamba ile siku nilkuwa naumwa sana nilimuuliza hivo ila jane hakujibu zaidi ya sorry ben forgive me, sikuwa na mengi nikaamua nimsamehe tuu ila sikumwambia kuwa nishakusamehe yeye akawa analia tuu analiwa huku kajiziba uso wake na kitambaa na zile sauti za fyuu zikisikika nadhani alikuwa akilia. Hapo mimi si najua kama ni dada yake yupo home hakuna kinachoharibika, nikauliza wee jane ilibakiza supu ndo unamalizia au mana nasikia tuh fyuu nahisi pale nilimkatisha hata hamu ya kuendelea kusimama pale jirani na mimi kwa kuuliza lile swali ambalo kiukweli lilikuwa na la kitahila na ni lama udhi tena yaliyo kithiri..
    jamani humu dasani kuna ugomvi au inakuaje nahitaji kujua nambieni kinacho endelea humu mana naona jane pale analia inakuwaje?! wanadarasa wote walibaki kimya wasijibu lolote lakini kidogo nikasikia sauti ikisema jane kabla wewe hujaingia alikuwa kasimama na benchrys labda ungemuuliza huyo ben anaweza kuwa na majibu..Hapohapo nikamwangalia jane nae alikuwa akiniangalia na kutoa ishara ya kuwa nisiseme lolote tuliyokuwa tukiongea nikaona huu sasa utakuwa msala mwingine mana mi gari linalo tembeza nyota yangu nahisi bovu ndio mana kila siku kwangu ni majanga tuu.....Inaonesha nyie mshaanza upuuzi tangulieni ofisini kwangu pale wewe ben na mwenzio jane kisha......Itaendelea

benchrys1996@gmail.com
&
benchrys.blogspot.com

Alhamisi, 21 Julai 2016

de 3

Gangstar noma
By: benchrys
3
Kufungua mlango hakuona kitu chochote hukubkulikuwa na kelele na fujo nyingi za kugonga mlango kama kuna ugomvi au mgambo kaibiwa na ameshaona adui yake nyumba ndio hii hapa,, ivi huu ni uchawi au mambo gani ya kujienjoy namna hii au macho na masikio yangu ni mabovu alisema hivo baba kisha akatugeukia sisi akasema hivi jamani simmesikia makelele sasa hivi hapa za makelele ya mtu kugonga hapa lakini nafungua hakuna mtu...Mi nikasema baba pengine umetazama vibaya mana hata mimi nilikuwa na wasiwasi mana zile fujo za kugonga nakajua hapa ndani hapata kalika ila siyo shida sana tufunge mlango tuendelee....Mama akasema hivi hukuwa umeanza kuelezea hata kidogo, baba akafunga mlango akaludi kukaa na mimi nikaendelea kuhadithia baada ya hapo baba akageuka kwa yule dada akamwambia pole sana bint,,, yule dada akajibu asante nashukuru pia namshukuru na mwanao ila huko nyumbani najua watakuwa wanawasiwasi kuhusu mimi niko wapi hadi mda huu, yule dada aliposema vile baba akadakia akasema sio mbaya sana ni bora upo hapa salama kuliko ungekuwa huko ambako wangekuharibu tuu...Akawa amejaribu kumtoa katika mawazo yale bint alipoonyesha katuliza akili ya ndipo na mimi nikajikakamua kuuliza hivi jina lako nani? kiukweli niliona nimejitahidi mana mimi katika mda au kipindi hicho nilikuwa mzito sana kunyanyua mdomo na kumwuliza swali licha ya kuwa nilikuwa ni mtu wa makundi ambayo mara nyingi ni ya kubishana. Naitwa Naomi chesko ok mana ndio tumetoka mbali ila sikufanikiwa kukuuliza niliongea maneno hayo baada ya yeye kutaja jina lake.. Ila kilicho nishangaza ni pale nilipoona ametaja jina langu'' ivi we ben mbona nasikia unachelewa sana kurudi nyumbani.......
    Jaman huu mda wa kulala ben siunajua kesho inabidi uwahi shuleni au imesahau alisema baba. Kwa upande wangu nliona kama kanirahisishia kujibu lile swali lililo ulizwa na naomi kweli baba ila unakumbuka ulinipigia simu iliniwahi hapa nyumbani lakini katika harakati za kurudi ndio nimekutana na hili zogo hujaniambia kulikuwa na nini' nilijitia mfuatiliaji kidogo ni kweli tangu narudi baba hajanambia kwanini waliniita mda ule tena akiwa kama anajazba fulani
Aha Basi kulikuwa na kakazi fulani kadogo ila mbona kwa kuchelewa kwako tumeshafanya,,,, naomi kwa kisikia vile akasema nambeni mnisamehe Kwa kumchelewesha kuja kufanya hiyo kazi mana mimi ndio nimekuwa kikwazo kwa hilo tatizo. Mimi mawazo kichwani yakaanza kupembua kama mwanasaikolojia hivi 'wenyewe wanasema mi sifahamu sana' inamaana huyu dada anaigiza au ndio mkarimu na mnyenyekevu hivi dah unaweza ukaaibika hapa bora nikalale tuu tuinane kesho, hayo ni maneno nilikuwa nikijisemea mimi mwenyewe katika kichwa changu nyie mnasema kimoyomoyo lugha hizi bhana,, basi nikawaambia jamani mi naenda kupumzika hapa nimechoka sana bora nikapumzike tuu. Baba akadakia ila leo kama mazoezi umefanya na ushukuru tulishaandaa maji ya kuoga. Baba kusema vile naomi akacheka alishindwa kujizuia. Haa na mimi nikaona hatakama nimeaga lazima nijue huyu kacheka nini
   Naomi: niliita hivo akaitikia abee ben siumesema unaenda kulala wewe. Ndio naenda kulala ila...... Kabla sijamaliza kuongea mama nae akasema wee ole wako na kesho tujisumbue kukuamsha huku saizi hapa unazugazuga kwenda kulala. Hapa naomi alitamani acheke ila akajishinda kwa kuzuia mdomo wake na kitambaa alichokuwa nacho basi na mimi ndio nikagundua huyu ananicheka mimi tuu, licha ya kuwa mama alivosema kamoyo kangu hakakupenda nikaona sasa naona uzalendo unanishinda, sasa nnamachaguo mawili nikalale huku sijui anachekea kitu gani au nikomae hadi niulize.. Kichwa hapo kilipata kazi ya kuchafua lipi litakua jema ili nilale kwa amani na usingizi wanfu uwe safii. Baada kufikilia ndio nikajikakamua tena na kuuliza we naomi naona unacheka nini au umekumbuka tulivokuwa tunakimbia ukanifananisha na vile vitom na jerry acha mambo yako bhana
Nikweli baba alivosema leo umefanya mazoezi ndio nikakumbuka hadi ulivompiga yule jamaa na jiwe! hapo hadi mimi mwenyewe nikajikuta eti naanza kucheka huku nilisema kwamba naenda kulala
    Acha hizo usiku mwema kwaheli jaman nikawa nasukuma mlango wangu ili niingie kulala naomi akasema kumbuka kuomba ben na sisi sote utuombee, nikajibu kuhusu hilo hata msijali hapo ndipo nikaingia chumbani kwa nikaanza kujiuliza ivi nani kaniruhusu kuanza utani na wadada kama hivi.. Mda si mwingi sana nikawa nishapitiwa na usingizi kama unavojua mambo kama haya ni emegenc tuu mara haukwambii fumba macho ulale ila mwenyewe utajikuta ushalala
***Naomi hiki ndicho chumba ambacho utalala utatusamehe hatupo vizuri maisha yetu hiyo ilikuwa ni sauti ya mama alikuwa akimwonesha naomi chumba cha kulala nashukuru sana niwatakie usiku mwema wenye amani naomi alisema kama ishara ya kumuaga mama.....
***Ivi we dogo kwanini unapenda uonekane kama wewe ndio bonge gentlemen hapa unajua tunauwezo wa kukugeuza hata kitoweo ok yule dem umesepa nae umempeleka wapi nahitaji nausiposema hapa hapa naanza na kukung'oa meno kama unabisha sema unabisha au kaa kimya tuu nakupa dakika tano kuwe kumesha sambazwa majibu ya maswali hayo kwenye masikio yangu nakungoja wewe mwenyewe dakika moja tayari ishaisha kama upo braza ee uliangalia vibaya mi sijaondoka na demu wako mbona tunaoneana hivo kama angu. Sijakaa vizuri nilipokea zinga la kofi hadi nikajikuta nimepiga magoti kama dakika tatu ivi,, hapo ndipo akili yangu ikawa imerudi jamaa yule akasema nadhani muda umekwisha tayari ok nambie umempeleka wapi huyo demu. Sikutoa jibu lolote lile akasema wewe unaona mimi ni kanumba au ray nipo kwenye muvi naigiza sasa ngoja akatoa kamba mfukoni akanifunga kwenye nondo ya dirisha kisha akasema ningoje nakuja mpuuzi wewe. Aliporudi alirudi na koleo na nyundo moyo ukaanza kunienda mbio kisha akatoa kisu mfukoni akakiburuza ukutani kikawa kinatoa kama moto hivi, Ok chansi ya mwisho sema mimi kimya tuu nilibaki. Nikiwa bado sijafunguliwa nilipigwa ngumi ya tumbo kidogo niteme utumbo nje nilipiga kelele mamaaaaa nakufaaa......
***Kumbe nilikuwa naota nilishituka asubuhi kuna jua kwa umbali nikajua wazi nimechelewa shuleni, nikajivuta kiuvivu ili nitoke nje duh nilipofungua mlango tuu.........Itaendelea

benchrys1996@gmail.com
&
benchrys.blogspot.com

Jumatano, 20 Julai 2016

de 2

Gangstar noma
by: benchrys
2
Haraka  tugeuke bana mbona huku ndio mateso tupu cheki sasa dah mbona tunafukuzwa hku nyuma angalia, aliongea yule dada huku akiwa kama anahuzunika kutokana na kuhisi kama atadhulika zaidi mana mbele kuna jamaa ambae ni anatisha mana amejazia mimi nikijicheki dah yani sina hata ubavu wenyewe wanasema kimbaombao basi akili yangu ikajipiga haraka namna ya kujitetea kuangalia chini kama kawaida nikakutana na jiwe moja ambalo nililiona kwangu litanifaa kwa kujitetea basi nikainama fasta na kuliokota lile jiwe yule jamaa alipoona nimeshaokota jiwe akagutuka na kugeuza safari yake ya kutukimbiza basi safari ikaanza upya mbio hadi nilipofika nyumbani nikiwa na yule dada wote tukiwa tunahema kama mbwa anatamani nyama..
    nyie vipi tena mbona tunashituana tu hapa kuna nini huko mlikotoka mana hata siwaelewi hata kidogo mnahemeana tu kama manini sijui, hayo yalikuwa ni maneno ya mama yeye ndio alituona tukiwa tunaingia pale kwa fujo kama tunakimbizwa na mbwa mwenye kichaa. Basi nikasema mama huko tulikotoka ni shida tupu huyu unaemwona hapa simjui nadhani hata yeye hanijui ila twende hata sebuleni tukae kisha niwaelezee vizuri, mama akasema huo muda mnaokuwa mnatoa hiyo habari yenu nadhani utakuwa mda wangu wa kupika mana nadhani mnajua saizi ni saa ngapi mda huo ilikuwa ni kama saa kumi na mbili na nusu simu yangu ilikuwa ikionyesha hivo, ndio hivo na kukimbia kote ila simu yangu nilikuwa makini nayo kama unavojua nipo tayari nisahau vingine ila sio simu na ndo mana hata wanaosahau kuweka alarm wakilala sio kwamba hawajui umuhimu wa kuwahi kuamka ila kujali tuu kitu hicho..Basi mama akaanza kazi ya kupika chakula muda ukafika tukaanza ila yule dada akawa kama anaogopa hivi nadhani hiyo yote ilikuwa kwasababu ni mgeni pale..Usiogope jisikie upo kwenu dada yangu,,,

****yule jamaa ambae alikuwa anataka kumfanyia unyama yule bint muda ukawa umefika kuzinduka akawa anajinyoosha ....Aaaaaamu aaha shit kudadeki nipo wapi hapa kuna mzee alikuwa anapita maeneo hayo akacheka sana
Dah bangi sijui za wapi hizi mtuu unashituka sahizi kuwa ulilala tena eneo kama hili dah
Kijana habari yako, huyo mzee alimsalimia kwa kibaunsa hicho hakujibiwa''' kijana habari za saizi nakusalimia, yule jamaa akamwangalia halafu akaguna wazee wengine bhana utalazimishaje salamu kwangu kama lazima siinatakiwa nikusalimie mwenyewe aha... Ok salamu sio lazima sana ulikuwa unatakaje mana naona salamu nyingi sana ndio nakusikiliza sema,,jamaa alisema hivo kwa hasira sana hadi yule mzee akaina hapa yaweza kuwa majanga mengine bure...Ok sikuwa na shida yoyote ila nilikuwa nakusalimia tuu hakuna lolote lile kwaheli mwanangu mzee aliondoka pale kwa wasiwasi mkubwa maana asije akapata majanga bure maana ilikuwa mda wa jion hakuna atakae msaidia

****tukiwa nyumbani tulikuwa tushamaliza tayari ukawa ndio mda wa baba na mama kuanza kusikiliza jambo ambalo ndio lilitupata ila mimi nikawa bado najiuliza yule dada kwao inaezekana watakuwa wana mtafuta ila nikajisemea sio shida sana angekuwa mtoto labda ndio ingekuwa ni tatizo kubwa, hapo nikaanza kuelezea jambo lililo tupata mara mlango wa pale ukagongwa tena kwa fujo..Fungua mlangoooooooo nasema funguaaa mlango nasema wote mle ndani tulikuwa kimya kama tumelowa maji hivi, baba akasimama na kufungua mlango lakini baada ya kufungua mlango......Itaendelea

benchrys1996@gmail.com
&
benchrys.blogspot.com

Jumapili, 17 Julai 2016

de 1

NGangster noma
Mwandishi: benchrys
1
Nikiwa na umri wa miaka 14 nilikuwa ni mtu ambae hata siku moja huwezi nikuta nyumbani hata kwa bahati mbaya hali ambayo iliwakwaza sana wazazi wangu kila siku wakawa wananisihi nijalibu kupunguza uzururaji kwa maana nilikuwa bado ni mwanafunzi wa sekondari katika shule moja iliyoko njombe mkoa mpya kwa sasa, kiukweli sikuweza kuwa muelewa kwa haraka kama inavo takiwa kwa binadam ambae anaitwa mtu mwenye nidhamu na uelewa. Jaman hivi mtoto kaenda wapi tena saivi wakati huu ndio mda wake wa kuludi kibaya tulicho mwekea tayari hakipo inaonyeshA dhahili kwamba asharudi ila ndio haonekani na alikoenda hata sijamwoma, dah huyu hili badae litakuwa tatizo tena kubwa sana tuu.. Hayo yalikuwa ni majibizano kati ya baba na mama ilikuwa ni mida ya saa tisa mchana, hiyo siku nilipofika nyumbani nilikuwa haraka sio kidogo nikabadili nguo kisha nikafakamia chakula na kuondoka hali iliyowafanya wao hata mmoja wao asinione hata nilipofika wala mda gani nimekula na kuondoka ndio maana wakawa wanaulizana mahali ambapo nimeenda.
   Dah mwanetu upo quick ni kinoma dah ushafika hizi engo tayari dah we noma au leo unataka uwahi kurudi home nini mana daily we mchelewaji, hayo yalikuwa ni maneno ya jamaa yangu joel. Usijali basi tuu mtu ukiShaamua kitu inabidi ujitahid kujisukuma ww mwenyewe nilimjibu hivyo
Basi powa joh langu njoo gheto mi nazama ndani
Powa sio kesi mdau wangu ila na we inabidi uwefasta kidogo co uchelewa teina
Aaaah wewe kitakacho nichelewesha ni nini sasa. Yalikuwa ni majibizano kati yangu na rafiki angu joel.   
    Dah kasimu kangu safari hii kazito hadi kananiboa yani dah, nilisema maneno hayo wakati joel anakula mana mi nlishakuwa full toka naindoka nyumbani.........Alipomaliza kula tukaanza safari ya kuelekea kituo cha internet kwa computer(internet cafe) njiani tulipiga stori nyingi za uongo na ukweli tukiwa karibu na kituo hicho tukakutana na god huyo alikuwa ni moja ya wanafunzi ambao tulikuwa darasa moja tatizo lake ni moja yeye hata mwalimu ashinde anafundisha anaweza kuondoka hajaelewa kitu chochote lakini ni mtu mwenye dharau kwa wanafunzi wenzake halafu ni wakujipendekeza kwa walimu aonekane yeye ndio mtu ambae ni bora kuliko wengine wote, kikweli hata nilipomwona sikutamani hata kumsalimia maana mi nlikuwa mtu ambae siwapendi sana wanafunzi au watu ambao ni vipele iwe mtani au shuleni. Oya ben mwanangu hata kama unamdisi huyo jamaa msalimie tuu huo anaofanya ni utahila wa mda mfupi anavunga we ngoja hapa tupo form two na sidhani kama kweli hadi mwakani tutakuwa wote darasa moja au kidato kimoja, maneno hayo aliyaongea jamaa yangu baada ya kugundua dhahiri kuwa namchukia sana huyo god kipele wa darasa hata kama ni wakiume.
    ngrrrrrrrrrrrrrrr........Ulikuwa ni mlio wa simu yangu aina ya samsung ambayo nilipewa na mjomba nilipofaulu kwenda kudato cha kwanza kwaajili alifurahishwa sana.
     Hallow ivi we mtoto umeenda wapi sisi huku tunakutafuta na hamna anaejua kuwa umeenda wapi acha kutusumbua hebu rudi haraka sana hapa vichwa vyetu vinawaza mambo mengi sana sio kwamba tunawaza kuhusu wewe tuu nakupa dakika kumi na tano nadhani zinakutosha sana kufanya mambo yako na kurejea hapa,,, Ilikuwa ni sauti ya baba baada ya kupiga simu inaonekana alikuwa na hasira sana na ndio maana hajataka hata salamu yangu, aliongea vile na kukata simu. Nikaona isiwe taabu acha tuu niende nyumbani mana kama ni siku nishaharibiwa na huyu god bora nsingekutana nae tu
Oya ben vp mbona kama huyo jamaa yako kashakuvuruga kabisa acha upuuzi bhana hebu twen zetu huko, aliongea hayo maneno joel ila kwangu sikuona kama yanamaana nikamwamba ee bhana ee minaenda zangu home nimepewa dakika tano tuu hapa niwe nishafika nyumbani we unataka niharibiwe siku yangu kama hivi hadi usiku nao niharibiwe vp wewe mzazi ni mzazi bana tofauti na wewe. Maneno haya inaonyesha kama yalimuudhi sana jamaa yangu joel ila nikaona sio kesi sana kama kashamaindi acha amaindi..Kwa hiyo mi kesho ndo kuonana tena bye nilimuaga na kuondoka lile eneo huku nikiwa mbiombio hadi watu baadhi walioniona wakabaki kunishangaa maana haikuwa kawaida yangu kukimbia au kijichosha kwa mazoezi.Jamaa yangu mmoja akanitania oya unawahi uwanjani au mbona upo mwendo hivo sikujibu niliachana nae na kuendelea kukimbia.....

***
Jamani nyie mbona waonezi niacheni bhana uwiiuu vibakaaaaa jaman naomba msada jaman msaada, we tulia tena usije tuletea zari hapa nishakwambia kimya"ilikuwa ni sauti ya bint mmoja akijaribu kuomba msaada huku akifokewa na sauti za kiume ambao inaonekana kabisa ni watu ambao wanaroho mbaya na si watu wema. Nikatulia kidogo akili yangu ikaniagiza okota hata tofali au jiwe kisha nenda huko ambako sauti ya msaada inatokea basi na mimi moyO wa kuwa mtiifu ukaja nikaokota mawe matatu ambayo yanaweza kuwa silaha yangu au msaada kabisa kwa bint huyo, nilipookota nikaenda katika ile chocho ndipo nikamwona huyo jamaa na bint wakiendelea kubishana nika kamata jiwe moja vizuri na kumpga nalo yule jamaa alipigeuka haraka nikashika jiwe la pili nikampiga nalo kichwani palepale akaanguka chini nikamwita yule bint na kuondoka nae huku tukiwa tunakimbia ili hata yule jamaa akiamka  asimwone mtu eneo lile tukakimbia na kupita kona fulani nikasikia sauti ya kimbea na unoko kabisa 'kantangazeeeeeeeee leo naona kuna wamefumwa ila kwa kudumisha upendo wamesepa wote shushuu' nilikariri tuu sura yake na kundelea kukimbia lakini nikiwa naendelea kumbia ghafla bin vuu nikaona.....Itaendelea

benchrys1996@gmail.com

Na
:benchrys.blogspot.com

.......