Ijumaa, 14 Oktoba 2016
Alhamisi, 13 Oktoba 2016
Jumatatu, 10 Oktoba 2016
Who am i
WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 13
Ilisikila sauti paaa!!! Kisha vika fuatiwa na vilio vya watu
Songa>>>>
Kila mtu pale tulipokuwa tumesimama alitawanyika na isieleweke kaenda wapi, na mimi isionekane zube sana nikaondoka na kuelekea kule ambako imesikika ile sauti nilijivuta hadi kufika kule ambapo niliweza kuona vijana watatu ambao wamejaza vifua kama breast za wanawake (sitaki swali) wakiwa wamesimama wakitoa kichapo ambapo mmoja kati ya wale alikuwa amehika bomba moja ambalo kwa mda huo lilikuwa likitoa moshi, nilijaribu kulitafsiri lile bomba lakini sikupata jibu lolote lile zaidi ya kujua labda atatumia kumpiga mtu ila bado nikabaki na swali kwanini litoe moshi halafu amelishika kwa raha kabisa, hili jambo sikulielewa kabisa nikajikuta nikisogea hadi mbele ili niwezekujionea mwenyewe vizuri kabisa.
NANI MWINGINE ANAE TAKA ALETE UBISHI JUU YETU SISI, KILA SIKU TUNAWAAMBIA HUU MTAA LAZIMA UWE NA HESHIMA JUU YETU SISI THREE SOJAZ SAWA HILI KUNDI LICHUKULIENI KAMA NDIO RAHISI WENU. SASA NAMMALIZIA NA HUYU BOYA ALIYEBAKI.
Baada ya kuongea vile alimdaka dada mmoja ambae muda wote nilimwona amekaa kiwoga woga sana,. Baada ya kumdaka yule dada alikuwa analeta ubishi aliokea kofi moja ambalo kwakutazama tuu lilikuwa ni zito sana hata mwingine ungepigwa lazima uombe maji ya kunywa. Hichi kitendo kilinikwaza sana na nilishindwa kabisa kujizuia nika paza na mimi sauti
;;;;;oya bro huyo dada kakosa nini hadi umpe adhabu kama hiyo hivi huoni kama huo ni unyama unaomtendea huyo,. Baada ya mimi kuongea vile akanijibu
;;kwa hiyo ulikuwa unaamuaje sasa au unataka uje kuwajibika wewe, no mind kama unataka nipo tayari kumwachia huyu Malaya aende halafu ubadiri siunajiweza
;;;;;kudadeki kwahiyo akili yako wewe ni kunyanyasa wanawake tuu si ndio ok sio shida sasa basi., kama wewe unajiita mwanaume unae taka uheshimike kila mtaa mi nipo tayari kukushushia hiyo heshima fara wewe.
;;hahahaha we mbuzi ivi unanibipu nadhani umeona uwe ray kwa kutafuta kiki ya kubishana na mimi? Si nakuuliza we toto la kahaba
;;;;;;toto la kahaba ndio lenye akili ya kishost kama wewe huku ni boy acha nyodo njoo tuonyeshane sio maneno mengi maan hayajengi vipi
Baada ya mimi kuongea vile alimwachia yule dada kwa kumrusha huko kisha akawa ananifuata akiwa kafura, watu wote katika hili eneo walianza kusogea pembeni ili washuhudia ni nini kitaendelea hapa wale ambao wao kazi yao ni upambe kama kawaida walianza
Bro akujui huyo dadeq zake anaona sisi tunaeheshimu kama ni malofa hivi hebu mwoneshe tuu boya huyo
Nae kwakuona kapewa sifa akawa bichwa hiloooo alitoka spidi na kuja kujirusha ili atulie na teke kwenye kifua changu. Lakini kabla hajafika nilruka kavu kisha tukakutana juu kwa juu na kwakuwa hakuwa na stamina ya kutosha akatulia mgongo chini.
Hapo hata kelele zilianza kupungua kutoka kwa wale wapambe. Lakini bado alionyesha ubishi alinyanyuka na kutaka asogee na ngumi aliporusha mkono niliudaka na kuuzungusha hapo ilisikika tuu sauti ya kaaaa kwenye mwili kisha kikafuata kilio kama mtoto, huku mwanzo alikuwa akiongea bezz zito tena la kujiamin kana kwamba yeye ndie general ya majeshi.
Baada ya pale nikataka kuondoka nikijua tayari nishamkomboa yule ambae hta kitendo ambacho alitaka kufanyiwa sidhani kama ni kizuri
Niliangalia mahali pa kutokea nikawa nimeweza kuona upenye fulan niliufuata lakini kabla sijatoka nilirudishwa pale katikati nateke zito kisha ikasikika sauti HAHAHAHAHAH WE UNATAKA KUUTAWALA MTAA AMBAO UNAWENYEWE KAMA UMEPIGA HUYU MMOJA BASI SISI TUTAANGAMIZA PAMOJA NA FAMILIA YAKO YOTE
Nikiwa bado nipo pale chini nikaona watu wakija pale na mapanga hapahapo gafla nikanyanyuka na kusimama kama mtu ambae ametoka katika usingizi na ameota ndoto ya kutisha sana
Wale wote wenye mapanga wakaanza kunifuata. Wakati huo nikiwa nawaza sina hata silaha, lakini nikakumbuka kuwa kuna njia ya kuwafanyia mauzauza kisha kila kitu kinakuwa fresh. Wakati ule wapo jirani ilikuwa kama CD ya kichawi inatazamwa.,., nilidank juu sana waliokuwa chini waliona kama cheche tuu zinawaangukia, mara mtu nikatua tena chini nikiwa sio mimi tena. Safari hii nilikuw na nguo za kininja zenye rangi ya nyeusi na nyekundu hapo ndio watu wote walibaki tuu wameshika midomo yao kuonyesha hawaamin walichokiona wenye smart phone nao ulikuwa ndio mda wao wa kuanza kushoot video maana wamezoea ninja assasin kwenye tv tuu lakini leo wanaona live kwa macho yao
Baada ya kutua chini pale nilichomoa upanga wangu nikiwa sina lengo la kumwacha hata mmoja kati ya wale wenye mapanga zoezi lililofuata hapo ni kichapo tuu kila aliejitahidi kunivizia na panga lake hakuna alicho ambulia zaidi yakufyekwa au kuvunjwa kiungo mojawapo
Waliokuwa wanaangalia kuna jamaa mmoja ambae ndie aliye nipiga lile teke la kunirudisha pale katikati huyu ndio sikutaka hata time nae aliposogea tuu nilidank na kutua kichwani kwake huku nikimshindilia kiwiko cha mkono ambacho kina ujazo wa aina yake kisha nikaruka na kumbetua kabla haja tua chini nilimwongeza teke ambalo lilimpeleka juu sana anapotua chini nikamtegea kisu nae akatua juu yake (kama mwoga fumba macho)
Waliokuwa pembeni wale washabiki baadhi yao walianza kuondoka taratibu huku wakirudi makwao na baadhi wakificha sura zao
Nilipomaliza zoezi lile kulikuwa na ukuta jirani hapohapo. Upanga wangu ukiwa mkononi niliutumia kuandika YOU HAV E TO KNOW (WHO AM I) kisha nikapotelea katika maeneo ambayo hata ungekuwa makini kiasi gan ungeondoka chenga huelewi chochote.
Dakika chache mbele nikaja kuonekana tena katika kijiwe fulani cha kushona viatu
Daaah ivi kumbe hata Tz kuna maninja
Daah mwanangu ivi yale yalikuwa mauzauza au ni kitu gan maan ilikuwa kama muvi.
Halaf nakumbuk kama umerekodi hiv lile tukio
Aaaah kweli halaf ckucheki ngoja nicheki saa hizi hapa
Alitoa simu katika mfuko wake wa suruali ilikuwa ni tecno h6 nadhani aliyotumia kushoot video ile
Basi watu wapale walijisogeza kuiangalia huku na mimi nikiwa ni mojawapo kati ya waliokuja kuitazama. Aliiwasha hii video ikaonyesha tuu pale ambapo walikuwa wanaongea kisha nikaruka juu sana kwa kudanki kuendelea ilikuwa ina scratch tuu
>>>>aaaaaah mwanangu hapo umeharibu uhondo wote duhh
Sasa kama memory yako inavirus siungeacha tuu kutuonesha shit smart phon nzima memory inavirus unazingua bhana
.,.,watu walichukia sana kile kitendo cha simu kustak kuonyesha ile video huku wao walikuwa na hamu nayo ile mbaya
Lakini mimi huo mda wote nikawa najiuliza inamaana hawanijui au sura sio yangu huku na kule ni tofauti. Maana hapa ningepata maswali kibao kuhusu uwezo huu lakini sikujua kuna nini hadi wanisahau wakati tulikuwa wote muda si mrefu kabla ya tukio. Nikiwa bado simu yangu ilianza kuita kuitazama ni nani-----itaendeleaaaaa
Who am i
WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 12
Baada ya hapo walitoa silaha na kuanza kuifuata ile gari____
Songa nayo
------wale wanajeshi waliasogelea hadi jirani ya lile gari kubwa ambalo lilikuwa na walinzi ndani. Lakini walishangaa kuona kimya kimetanda sana katika gari hili ila kwakuwa ni wanajeshi wakajipa moyo na kuingia katika gari lile ndani wakiwa na imani lazima watamuona mtu ambae anawaletea mauzauza hapa
Oya kinju mbona hakuna kitu humu ndani, ngoja niwashe hata tochi ili nione./ baada ya hapo aliwasha tochi yake ambayo ilikuwa na mwanhamkali sana lakin hakuweza kumwona mtu mle ndani zaidi aliona tayari mlango wa upande mwingine nao upo wazi.
Kwa kuona hivo akajua walinzi wanawaogopa, alipaza sauti
JITOKEZENI TUMEKUJA NA BOSS WENU KUWENI NA AMAN HATUPO KUWADHURU NYIE. HEBU NJOONI TU. Alipoongea vile ndipo akaanza kujitokeza mlinzi mmoja hadi mwingine hadi wakafika idadi kamili inayotakiwa ambapo bamboo kwa mda huo hatazamiki hata kidogo usoni kaumia hadi huruma kama ungemuona huwezi kumwangalia mara mbili
Walijaza mafuta katika lile gari na kutaka kuanza safari ya kurudi nyumbani lakini kila walipojaribu kupiga starter hakuna kulichojibu.
Mwanajeshi mmoja alishuka chini na kuangalia huku akiwa na tochi yake lakini hakuona tatizo lolote. Wakabadilisha mawazo labda wote wapande gari la boss wao ambalo amekujanalo,. Walikubaliana na hilo wazo kisha wote wakaondoka na kulifuata lile gari kisha wakapanda na mwanajeshi mmoja akakaa siti dereva kuonesha kwamba yeye ndie wa kuendesha aliweka funguo na kunyonga hakuna hata mwanga uliotoka ilionyesha dhahiri kwamba hili gari halina betri kwa mda huu. Ila kwa kujiaminisha alishuka na kuangalia, na kweli beri kwenye gari tayari ilikuwa imesha chomolewa
Mwanajeshi huyu alifura kiasi kwamba akasema huyo anaemchezea akili laiti akionekana hana kichwa
)()( kudadeki nitapeleka mtu kuzimu mimi, tafadhali wewe kilaza hebu jitokeze mwenyewe kabla sijaanza kukusaka)()( aliongea mwanajeshi yule kama mwenda wazimu lakini hakuna aliyemjibu hata kwa hewa tuu
Masaa yalisonga mbele bila kukawia, toka saa tatu mda walio kuja huku hadi sasa tunaangalia saa ni saa saba na robo na hakuna magari yanayoweza yakapita haya maeneo mda kama huu, mwanajehi baada ya kuchanganya akili akaona huu upuzi hakuna wa kulala hapa porin.
Alinyanyua simu yake na kuandika namba fulani kisha akazipiga
-_-_-__-yaa ndio mkuu, tupo eneo la mawenzi sijui huu mtaa wanaita, yaa ndio njoo, au tuma watu, ndio, ok sawa simu ikakatwa
Baada ya dakika chache kuna magar yapatayo manne yalitinga katika hili eneo, kisha wanajeshi wakashuka wasio na idadi na kuanza kuingia katika pori hili huku wakikata baadhi ya miti ambapo wakati huo wote nilikuwa nikiwaangalia tuu, na baada ya muda mfupi tuu walimaliza maeneo yote yakawa wazi. Nikaona isiwe shida kama nilipambana na yule kiumbe nikamshinda nitashindwaje na hutu tuumtu twa kawaida.
Baadaya hapo nilichumpa toka pale niliposimama na kutokezea katika kaeneo ambako kalikuwa wazi ambapo ni barabarani.
Wanajeshi wote walishituka na kugeuka. Ile wanaangalia nyuma yao waliona ninja akiwa na maski fulani ya rangi kama silver ilingaa kutokana na kuwa walikuwa na tochi za mwanga mkali usiku ule.
Kwa kuwa walikuwa wengi sana walijivuta kwa mshikamano hadi pale ambapo mimi nipo huku wakiwa na iman ni lazima wanikalishe tuu.
(hebu kaa hapo hapo upo chini ya ulinzi) ilisikika sauti ya mwanajeshi mmoja ikiniamrisha ninyooshe mikono juu eti nimesalenda kwao.., kimoyomoyo nikasema sio masharti ya ninja hayo kunyoosha mikono juu. Kisha nikawageukia kuwatazama.
Silaha zao zoote zilikuwa zikiniangalia mimi kuashiria kwamba siwezikufanya kitu chochote kile ili kujinusuru, lakini nikaiona njia moja ya tuu ambayo ilikuwa ni kuwapiga changa.
Baadaya kugeuka nilichuchumaa chini
Wanajeshi wakiwa wananitazama pale nilipochuchumaa ulitokea mwanga mkali na mlio kama wa bomu,. Kufumba na kufumbua mwanaume nlishapotea mda mrefu sana. Ule usiku walitafuta lile eneo lote lakini hawakuona mtu yeyote yule. Baada ya hapo waliamua kuondoka wote katika lile eneo na kurudi makwao.
Safari ilikita moja kwa moja hadi nyumban kwa boss na kuwaacha pale pamoja na walinzi wake. Walimchukua boss kwa kusaidiana kisha wakamweka sebuleni. Huku wakimwamsha kwa fujo na kwa bahati nzuri walifanikiwa kumwamsha hadi aliamka, kisha walimfanyia utaratibu wote na baada ya dakika chache wote waliingia kulala hadi asubuhi
_____________________________
Ilipofika asubuhi boss aliamka na kuwasha tv apate angalau taarifa ya habari
Habari ya kwanza kusikika
)))))asubuhi hii katika mtaa wa mawnzi kuna magari mawili yameonekana yakiwa yamewakamoto, tukio hili inaonekana limefanywa usiku wa kuamkia leo na mhusika bado hajajulikana mpaka sasa, jeshi la polisi bado linaendelea na uchunguzi zaidi juu ya tukio hilo(((((
Boss baadaya kusikia habari ile palepale alizimia. Mhudumu mmoja ambae alikuwa anapita kwa aajili ya maandaliz ya chai ndio aliyekuwa wa kwanza kuona lile tukio, aliwaita walinzi ili ikiwezekana wamfikishe hospital akapewe huduma.
Walinzi walipofika pale waliita gari na kumpeleka kituo cha afya na sio katika hospital kubwa kitedo ambacho kilimshangaza yule mhudumu, alipata shauku ya kuataka kuuliza lakini aliushinda mdomo wake-----
Asubuhi tunaamka katika nyumba ambayo na bon amepanga,.
Kuna wadada wawili walikuwa wamekaa wakiotea jua wakiwa wamekaa kizembe kabisa.
======ivi shoga mbona huyu kaka haamki hadi sasa hivi
==nyooo ko wewe umejikalisha kimitego hivo ili umpate,.
===sasa hayo yametoka wapi sasa ndio jibu la swali langu au
=yametoka wapi mdomoni au we unatolea mata***ni, hebu nitokee hapa fyuuu
== powa natoka ila hadi nimwone
=Dadeki na hatoki huyo hujui anamwogopa bashir tena na wewe enheeee sijui>>
Katika hii nyumba hawa wadada wawili sijui ni wanalaana au vipi maana wao ni maneno tuu mda wote lazima watupiane
*******tukiwa mbali kidogo na huu mtaa tunamwona bon akiwa na vijana kama wanne hivi ambao walikuwa ni boda boda na mmoja yupo tuu sijui anafanya kazi gani.
.oya broo mishe gan unapiga kitaa hiki
Daa bado sijapata mishe maana bado ni mgeni
. daah pole ila sio shida_____kabla hajamaliza kuongea ilisikika sauti paaaa!!!
Kisha vikafuatiwa na vilio vya watu baada ya -----itaendeleaaaaaa
Who am i
WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 11
---------ilikuwa ikionyesha dhahiri kwamba kuna polisi tayari washaingia pale ndani na taarifa wamepata wapi hakuna aliyeweza kujua baadhi ya watu ambao walikuwa bado hawaja ingia ndani walishikwa na kuwekwa ndani ya gari ambalo linafahamika kama tenga. Kisha afande mmoja akasogeza gari jirani kabisa na uwanja, na kuanza kufungua milango ya kila mmoja.
Usiku huu ilikuwa ni fujo tuu katika hii nyumba
Baada ya dakika kumi na tano walikuwa tayari wameshakusanya wapangaji wote na kuwapakia kwenye tenga
Aisee hapa kuna chumba kimoja naona kama bado hatuja pita(aliongea afande mmoja kumwambia hivo mwenzie)
Ok nichumba kipi hicho kipara
Chumba cha mwisho kwenye karibia na kona. Ahaa we nyoronyoro nenda kagonge fasta (alimwamulisha afande mwenzie)
Yule afande ambae alionekana ni mwembamba sana hadi wanamwita nyoronyoro aliondoka ili akaangalie katika kile chumba na amchukue na aliyeko ndani waende kituoni
Ngo ngo ngo fungua mlango (kimya) nasema fungua mlango,.,. aliongea kwa ukali lakini hakuna sauti ambayo iliitikia wala mlango haukufunguliwa alichokifanya kuulazimisha kufungua akafanikiwa. Lakini ile anaingia tuu ndani alibamizwa na mlango hadi akajikuta anarudi tena nje. Hadi hapo hakuwa na hamu tena ya kuendelea kufuatilia hili swala la kutaka kujua aliyeko humu ndani, aliondoka na kurudi hadi kule kwa wenzake.
Oya kimbao mbona unarudi bila abiria inakuwaje au umeshakula hongo hukohuko.
-nianchie upuuzi hebu nenda kwanza wewe ivi unadhani wewe ulisahau kwa bahati mbaya kwenda katika kile chumba.
Unamanisha nini?
- nimesema nenda kamchukue aliyeko ndani. Baadaya kubishana sana yule ambae alikuwa kama ndio kiongozi alitoa uamuzi wa kwamba tuachane nae tuu.
Lakini wapangaji wengine nao wakapaza sauti zao
NYIE MAAFANDE NDIO HAMNA AKILI KWELI YAANI MHUSIKA MUMWACHE HALAFU TUCHUKULIWE SISI WENGINE AMBAO HATA HATUHUSIKI SASA HAPA HATOKI MTU, MTAKALO AMUA AMUENI TUU WOTE TUNASHUKA HU UJINGA SASA>
Baada ya kuongea vile alianza kushuka mmoja baada ya mwingine hadi gari likawa tupu. Maafande walijaribu kutumia ubabe lakini hakuna aliyyeweza kuwaridisha mle ndani. Walipoona wameshindwa waliamua kuondoka na bashir pekeyake na kwenda nae kituoni ili akawasaidie maelezo kwa kitu kilicho tokea.
Gari lilianza safari na kituo cha kwanza kilikuwa katika kituo cha afya ambacho hadi ule mda kilikuwa bado kipo wazi, na kumpa huduma ya kwanza bashir ili waendelee na safari yao. Baadaya kufika kituoni bashir alifikishwa na kupelekwa mahali maalumu kwaajili ya maelezo. Lakini alipofika tuu polisi mmoja ambae alikuwa ni wa kike akajisemea asante mungu KAMA HILI JAMBAZI LEO LIMELETWA
Hongereni kwa kazi nzuri maafande maana huyu alikuwa ni msumbufu sana. Kisha akapelekwa katika chumba kingine bila kuulizwa chochote
_______upande wa walinzi kule barabarani_______
Oya nyie jamaa hapa naona boss leo ni kama hana msaada hivi, mnashauri tufanyaje sasa tutembee kwa mguu au jee.
Kudadeki acha ujinga hata kama ramani tunayo umajua huu mtaani wa akina nani wewe kama utatembea kwa mguu safar njema bamboo sawa sisi hatuna noma hata kwenye gari tutalala tu
Duuuh ila nae anazingua sa siapokee simu tu tuelewe tunafanyaje-----wakiwa wanaendelea kujadiliana mara simu ya bamboo ilianza kuita, alipoitazama alifurahi baada ya kuona namba ya boss ndio iliyokuwa ikipiga simu kwa muda ule, aliipokea
_-_-_yaah boss, ee ndio, enhee, sawa ok, lakini mbona hakuna m-pesa hili eneo, ya ni bora uje nayo tu, ok asante, sawa tutakungoja tuu, asante. Kisha simu ilikatwa.
Bamboo alifurahi, na wenzake kidogo furaha yao ilirudi maana walikuwa wakiwaza watalaleje hapa polini na isitoshe sio wenyeji. Lakini waliposikia boss anakuja ili waondoke walishukuru sana kisha wakaingia kwenye gari na kuanza kumngoja ili atokee wajaze mafuta kwenye gari safari ya kurudi nyumbani ianze.
Walikaa kwa mda kama wa nusu saa wakaona boss hatokei bamboo akataka anyanyue simu ili ampigie tena boss. Lakini gafla akaona simu yake imepokonywa sikioni mwake, kwaakili yake alijua labda ni utani waliojizoesha na wenzake ndio wamechukua simu. Alimgeukia mwenzake ili amwambie aache utani wa kijinga lakini akajikuta akipokea makofi tuu
Bamboo alianza kuona maruweruwe. Wakiwa bado hawaelewi chochote mara wakaona kama mbele yao kuna taa zinawaka na kuzima huku zikiwa fuata wote wakajificha chini ya viti vya gari lile ili ule mwanga usiwamulike. Lakini mauzauza hayakupungua mara wakahisi kama wanamwagiwa maji kwenye migongo yao tena maji ya barid kama barafu kitendo kilichomfanya kila mmoja wao kunyanyuka ili ajipukute hayo maji. Kitendo cha kunyanyuka tuu kioo cha mbele cha gari lile kilipasuliwa.
Wote wakabaki wameduwaa tuu mara wakaona mtu ananyukia mbele ya gari lile
Bamboo alishika usukani ili aanze kuendesha amharibu huyo aliyekuwa ananyanyukia mbele ya kioo. Lakini gari haikuwaka. =.alisahau kama mafuta yalikuwa yameisha na ndio walikuwa wanamngoja boss awaletee mafuta
/////kweli bahati mbaya haina mwenyewe na kifo cha nyani miti yote huteleza/////
Bamboo baada ya kuona vile akaamua kujitosa na kuchumpa pale dirishani kwenye kioo cha mbele ya gari ambacho kilipasuliwa, lakini kabla ya kutoka nje alirudishwa na teke ambalo lilimpeleka hadi siti ya nyuma kabisa huku akitulia mgongo. Bamboo alilalamika sana kuilaani hii kazi ambayo alipewa na boss wake leo..,,,/; kwa mbaali wakaweza kuona mwanga wa gari inakuja katika lile eneo
______)kwenye hili gari tunaona boss wa akina bamboo akiwa na wanajeshi wawili ambao wameshiba sana(_______
Aisee mkubwa gari lako ndio lile au
Yaah ni lenyewe vipi kwani
Mbona naona kioo cha mbele kama kimevunjwa vile (alikuwa ni mwanajeshi mmoja ambae alikuwa katika lile gari na boss wa bamboo)
Ngoja tusogee jirani kwanza
_-_-gari lilifika hadi pale kwenye gari ambalo lipo na walinzi. Wanajeshi wale walikuwa wa kwanza kushuka ambapo mmoja alizunguka ili amfungulie mlango boss, mlango ulifunguliwa na boss akawa anashuka kwa maringo sana ili akajue nini kinaendelea kwa walinzi wake. Lakini alipotoa kichwa tuu na kushusha mguu mmoja hapohapo alianguka chini wanajeshi hawa walipata wakati mgumu sana maana hawajui ni presha ya boss au kitu gani, walimnyanyua ili wajue cha kufanya.
Baada ya kumnyanyua mwanajeshi mmoja aliingia nae tena katika gari huku mwanajeshi mwenzake akifungua buti na kutoa madumu mawili ya mafuta ili akajaze katika lile gari lililochukua walinzi ili waondoke kukamilishakile ambacho kimewaleta
Huyu polisi ambae alikuwa na boss baada ya kumwangalia vizuri aligundua kuwa boss amedwingwa sindano ya usingizi. Alimwita mwenzie, akaja
Aisee hapa inaonekana pana hatari hebu tumwache boss tuacheki hicho kinyago kinacho tuchezea(baada ya hapo walitoa silaha zao na kuanza kufuata gari------itaendeleaaaaa
Who am i
WHO AM I (mimi ni nani)
Benchrys
No. 10
-----yule aliingia ndan na kuwasha tochi katika simu yake ili aangalie hela mahali ambapo anaziweka kila siku, lakini alishangaa kuona hakuna kitu chochote zaidi zimebaki tuu zile nguo ambazo zilikuwa jirani na ile sehemu ya kuhifadhia hela zake.
Hadi hapo mzee alichanganyikiwa kabisa asiamini kama kweli hela zake hazipo pia akabaki anajiuliza ni nani aliyefanikiwa kuingia hadi ndani ya kile chumba chake na kuondoka na pesa zake.
Licha ya kujiuliza maswali hayo yote lakini hakupata jibu ila akajipa moyo wa kuendelea tuu kutafuta pengine ataziona, ukiangalia umeme haupo katika hii nyumba ndio kitu kilicho mfanya ajipe moyo upya wa kuendelea kutafuta pengine ameangalia kwa pupa hadi hajaona kitu chochote.
Alitafuta hela zile kwa mda wa nusu saa lakini hakuziona, baadaya hapo akatoka na kukaa sebuleni huku kukiwa ni giza ila simu yake ndio iliyokuwa inamwongoza huu mda wote.
Upande wa walinzi nao walingoja sana hadi baadae wakakata tamaa kabisa, bamboo kama kawaida akanyanyua simu yake na kutafuta namba ya boss na kupiga,
Mzee akiwa nyumban amekaa pale kwenye sofa lake mara akasikia simu ayke inaita tena akanyanyua tena ili aone ni nani anae mpigia, alipoona ni mlinzi wake bamboo hata hakuhangaika kuipokea ile simu mana alishajua hawa shida ni mafuta na sio kitu kingine.
;;;kwakweli usiku huu ulikuwa ni mbaya sana ambao hata wasingeweza kuusahau hata mara ,moja
;;;IVI HAWA NAO WAPUUZI INAMAANA HAKUNA HATA GARI MOJA LINALOPITA KATIKA HIO NJIA MBONA WANATAKA WANIFANYE KUCHANGANYIKIWA HAPA SHIT;;;;
aliongea boss alipokuwa amekaa pale sebuleni baada ya simu kutoka kwa mlinzi wake bamboo kukatika
mzee akiwa amekaa tena simu yake ikaita tena
ya ndio nimekutafuta sijui ulikuwa wapi kijana wangu,
aah sawa mimi hapa nina tatizo kama hutojali sijui kama unaweza kuja hata sasa hivi hapa nyumbani, ok nitshukuru sana kijana wangu nakutegemea usiniangushe kwakweli, aaaaah ok, ok, nashukuru sana(simu ikakatwa)
baadaya muda kuna alipiga hodi mzee alikaribisha ili aingie ndani
daaaah mzee hapa naona shida yenyewe hata huna haja ya kuniambia inajieleza yenyewe aisee pole sana, ngoja nikutatulie haraka. Kijana aliingia kwa maneno mengi sana ambayo mzee hata hakupata chansi ya kuongea. Akabaki ametulia tuu kumngoja tuu kijana huyu akamilishe hii kazi ndipo waongee zaidi.- baadaya dakika chache umeme uliwaka ambapo mzee alifurahi sana akamfuata huyu kijana na kumwambia----; yaaah hebu njoo ukae kwanza mana hapa sikujua kabisa ntafanyaje hapa
sawa mzee wangu hizi kazi za tuu kwetu kama hela ipo
aaaah we usijari pesa sio tatizo sana, ehee niambie unahitaji sh ngapi mana umenisaidia sana
-----mzee alifurahi huku akihitaji aambiwe kiasi cha pesa ya kulipa kwa kurekebishiwa umeme wake katika nyumba kijana nae kwaajili ndio kazi yake hakuzubaa akamwambia
++mzee hapa kwakuwa umeniita usikukama huu utanipa elfu hamsini tuulikitokea tatizo niite tena.
Mzee akamwambia hebu ningoje hapohapo kwanza nakuja. Kisha akasimama na kuelekea ndani ili akafuate pesa amlipe huyu kijana
Baadaya kufika ndani ndipo alijua kuwa simu yake haikumdanganya kuwa ndani kwenye briefcase yake hakuna pesa yoyote
Kidogo azimie lakini watu wakubwa tena mapedeshee kama hawa hawawi na akiba ndogo akaenda kufungua begi fulan hivi kubwa kiasi
Ile anafungua tuu lilichanika begi lote huku vitita vya pesa vikidondoka chini akahesabia kiasi kama cha laki mbili na kuondoka nacho
Alirudi tena sebuleni na kumkabidhi yule kijana zile pesa na kumwambia asante mara kadhaa
Tukirudi kwa ben na bashir hii nyumba huu usiku zilikuwa ni kelele tuu
Wakati huo bashir alikuwa anatoa damu puani hadi mdomoni huku akiwa hana hata nguvu za kusimama tena
Kama kawaida wadada na maneno yao
Hahahaaaaaaaaaaaaaa babu uuu leo yamekupata unajifanyaga kidume sana kwa wenzio leo kajamaa kadogo kadogo kama hako kamekukalisha boya wewe
;;;;;mh amina tulia bhana kelele hadi unaboa ujue hapa atakuwa anakariri wanaomletea shobo shauri zako
Ohoooooo tena achunge akitaka kunipiga tuu nipo tayari nikaolelwe na huyu mgeni hata kama sijamfahamu. Wenzie baadaya kusikia hivyo walicheka sana huku wakimwambia shauri zako
Bashir baada ya kumwonesha na kumfunza adabu, nilijua wazi kwamba yule mwanamke wake labda atamsaidia kumwondoa pale lakini mke wake mwenyewe ndio kwanza alikuwa anapiga tuu stori na wenzake
;;;;; enheee shoga imekuwaje hadi shemeji yetu inakuwa hivi tena, aliuliza hili swali dada mmoja ambae walimtaja ni qeen.
Aaah shoga wewe acha tuu huyu mgeni si akaja kugonga na kuuliza wapi ambapo anaweza kupa msosi usikuu huu ili ale akalale bashir kama kawa na nyodo zake akajibu pumba lakini mimi nikaona sio vyema nikamwelekeza mahali ambapo anaweza kwenda na kula, huyu mkaka aliondoka, huku nyuma sasa bashir amenimaindi vibaya na kujisemea akirudi huyo boya wako nawachinja wote. Mimi sikuwa na la kusema
Basi huyu mkaka aliporudi akawa amekuja kutoa shukran bashir siakajifanya kumpandishia mimi nimewasilikiza wamebishana hadi wakasema watoke nje ili waoneshane, mambo ndiokama unavoona saizi hivi mtu tayari chini_-_--___-
Huu ni uboya ivi we unadhani mimi nikamtoe pale huku mimi mwenyewe kila siku napata shida tuu za kupokea kichapo bila sababu yoyote leo na yeye aonje bhana
(aliongea maneno yale mke wa bashir ambapo alikuwa amekaa na wenzake katika gogo ambalo lipo kwenye moja ya ukuta wa nyumba ile na baadaya mda wapangaji karibia wote waliondoka na kurudi ndani kwao huku mdada anaeenda kwa jina la Asha akisema kesho lazima awe redio ya mtaa kutangaza kuwa bashir jana usiku alipigwa kama mtoto na mgeni ambae ameingia jana hiyohiyo kwenye nyumba hii) lakini wenzake wakasema shauri yako na mwenzio amina nyie inaonekana mnataka kumbip bashir atamalizia hasira zake kwenu jifanyeni hamjamfahamu tu. Moja wao aliongea maneno yale na kuingia ndani kwake na mimi baada ya kuona kama adabu tayari nimeshamfunza nilinyanyuka na kuingia chumbani kwangu ili nilale na kesho nianze kazi ya kulipa visasi kwa wale ambao wanahusika na kututeketezea familia zetu bila sababu yoyote ile.
Niliingia ndani kwangu na sikutaka hata mmoja ajue nimeondokaje hadi kuingia ndan
Hii sikunililala kwa tahadhali sana, maana najua kabisa hii nchi yetu ya Tanzania wambea hawapungui.. unaweza sema kitu kitabaki siri kumbe kuna watu washapiga simu hadi kituo cha polisi ili kukuchomesha wewe ambae sio mwenza
Nilipoingia ndani nikachukua ile karatasi ambayo nilikabidhiwa na mama ili niipitie nijue ni nini ambacho kipo ndani yake
Nilisoma kwa mda wa dakika kama tano, mara nikasikia sauti kutoka nje wote mpo chini ya ulinzi hakuna mtu kutoka nje------itaendeleaaaaaaaa
Who am i
WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 09
---------sasa siungejenga nyumba yako mwenyewe (huku msonyo ukisikika)
Kiufupi haya maneno maneno yalimuingia sana huyu jamaa. Akajisemea ivi leo hii mimi basher ndo naambiwa upumbavu huu na mwanamke hizi dharau au kitu gani.
Baada aya kuongea hayo akamgeukia tena ile kwa spidi kama amechomwa na sindano au mwiba. Hali hii ilionyesha kabisa kwamba anahasira sana kwa jinsi alivokuwa. Ndipo ikasikika sauti samahani bashir nisamehe
Pumbavu ivi unapata wapi ujasiri kama huo eti mimwanaume mingine, kwahiyo huyo mgeni wewe atakusaidia nini wewe. Sasa namngoja arudi ili niwaonyeshe wote kuwa bashir ni mwanaume wa shoka.
Na kweli baada ya kuongea vile akakaa kwenye kochi fulani ambalo lilikuwapo mule ndani akimaanisha kwamba ananingoja mimi ili nirudi chumbani kwangu yeye anifuate
______kwa bon_____
-- baada ya kufuata yale maelekezo ambayo nilipewa na mke wa huyu jirani yangu nilienda mojamoja kwa moja hadi lile eneo na kuagiza kitu ambacho nilikuwa nakihitaji kwa wakati ule.
Nikiwa nimetulia nangoja mama ntilie aje aniletee chakula mara nikasikia kelele nje, watu wengi wa mle ndani walitoka ili wakashangae lakini mimi hata sikuwa na habari maana nilienda kwa shida ya kula na kula na sio mambo mengine. Ile nimekaa nangoja, niliona mda unazidi kuenda tuu lakini siletewi chakula changu nikasimama ili niangalie mahali ambapo yupo lakini sikuona chochote. Lakini baada ya dakika chache nikmwona nae akiingia toka nje. Kwa maana nae alienda kuangalia tukio lililo kuwepo kule nje. Niliboreka lakini basi hakuna namna yoyote ile maana mimi ndio mwenye shida. Ilinipasa kungoja tuu
Baada ya dakika chache ndio chakula kiletwa. Nilikula kwa fujo sana mda wa dakika moja nikawa tayar nimeshamaliza nikalipa hela na kuondoka nikienda nyumbani.
Nilifika nyumbani lakini kabla ya kwenda ndani nikapitia kuwashukuru kwa malekezo
Ngo, ngo, ngo
Yaa nani unagonga, aliuliza hivo bashir
- aaah ni mimi jirani yako hapa
Ok powa ingia tuu
- asante. Kisha nikaingia hadi ndani.
Nimekuja sina mengi ila nawashukuru tuu kwa msaada wenu nimefanikiwa kupaona asante. Kwaheli mimi naenda kwangu
Oya dogo ngoja kwani (alisema hivo bashir na mimi nikasimama tena kwa heshima zote)
IVI UNAJUA MASHARTI YA UNAPOENDA KUPANGA NYUMBA HIZI UNATAKIWA KUWAJE (aliuliza hili swali bashir lakini sikujua namaanisha nini)
Bro swali lako linamaana gan mbona kama sikusomi
--ahaa hunisomi utanisoma tuu subiri baadaya muda
Kudadeki usjitie kidume kwa wageni huku hujui mimi ni nani hata siku moja bado sijamaliza tena naomba tuelewane hapa sijaja kwaajili yako na kama ni hela ya pango hujanilipia kwahiyo fanya yako na mimi nifanye yangu sawa bro heshima ni kitu cha sana naona unaelekea hatutakuwa sawa hata kidogo(nilimwambia hivo nae akanijibu)
Powa ila mazingira ya watu hata sikumoja usijitie unajua sana, tena kama mimi ukinizingua nakumwaga ubongo kabisa bila hata kukuangalia usoni unasura ya kupastor au ki gangster sawa mdogo wetu
(niliona huyu anataka kunipanda kichwani tena hata heshima hana)
Sawa sio shida sana tuache maneno mengi kama madem wakitaa chenu twende njee saizi ili tukajue ni nani zaid na ni nani boga lililooza kabisa.
Bashir kichwani akajisemea leo ndio pa kuchukua ujiko kwa haka kaboya kengine ivi hakanijui nini ngoja kwani.
Alipojisemea hivo alimama na kunifuata hadi pale nilipokuwa na kusema sawa hebu twende. We jogoo la shamba huwezi kunitishia maisha yangu kama hukuchunguza kabla ya kuja kupanga hapa ndio utafahamu vyema huyubashir ni nani
Wakati huo wote yule mwanamke wake alikuwa akitusikiliza na kutuangalia bila kuongea kitu chochote kile
Mimi na bashir tulisimama na kutoka hadi nje ambapo kulikuw ana uwanja katikati ya ile nyumba.
Bashir alikuwa na maneno mengi sana hadi na baadhi ya wapangaji wengine walitoka ili wajue kuna nini hadi bashir anapigamakelele ya namna hii.
Kwa macho yangu nikawa nashuhudia milango ikifunguliwa na baadhi ambao walizima taa zao wakawa wanaziwasha ili waweze kushuhudia ni nini ambacho kinaendelea usiku huu
/////shoga angu leo kama siokuna timbwili hapa ngoja tulicheki atakae bondwa kama kawa kesho ntakuwa gazeti kitaa kizima yani.
Sema wee shoga nakuaminia kama ni ukiwembe tuu unajua
Acha zako mbona hata wewe uko hivo unakumbuka ile ulipozusha kuwa umenifumania.
Aaaah kausha bhana usije ukanikosesha mtanange huu bure////// ni wasichana wawili ambao majina yao hayajafahamika bado
Baada ya wapangaji kutoka pale bashir akaona huu ndio wakati wake wa kuonyesha uanaume wake maana wapangaji wote walikuwa wakimfahamu_______
______kwa baba______
Baba akiwa ametulia nyumbani amesha maliza taratibu zote mara simu yake ikawa inaita
Ngrrrrrrr x5
Naam haloo
Ndio mkubwa vipi ile mipango imekaa vizuri
Mipango gani
Mzee usifanye umesahau
Aisee hebu nikumbushe kwani wewe ni nani (simu ilikatwa na maongezi yaliishia hapo)
Baba hadi hapo hakuwa ameelewa ni nani aliyepiga simu kwa wkati ule na kuongea habari za mipango imekaa vizuri alizima tv na kuingia kulala
__________________________________
Tukirudi kwa yule mzee kwenye lile jumba tunamwona mzee ambae ni boss ndo anafahamika hivo
Yupo uwanjani anazunguka tuu peke yake huku nyumba ikiwa haina umeme na mafundi wote wapo bize kwa wakati ule.
Akiwa anaendelea kuzunguka mle ndani kama yeye ndie mlinzi mara simu yake ilianza kuita alipoangalia ilikuwa ni namba ya mlinzi wake mmoja bamboo jina lilisomeka hivo kwenye simu,. Ila mzee hakupokea maana aliona watakuwa wanampotezea tuu mda asijue wanataka kumwambia kitu gani,
Simu iliita hadi ina kata bila kuweza kupokelewa, lakini bamboo hakukata tamaa alipiga tena simu safari hii iliita hadi inakaribia kukata ndio ikapokelewa.
Samahani boss gari mafuta yametuishia na hatukutembea na akiba yoyote sijui kama unaweza agiza mtu aje atuletee huku tuko hapa barabarani.;;.;.; bamboo aliongea bila nukta maana alijua lazima huyu boss atakata tuu simu ile na kutofanya chochote kile.
Boss alijibu hebu ngoja kama dakika tano hivi natoa majibu, kisha simu ilikatwa nae akaingia tena ndani ili------itaendeleaaaaaaaaI