Gangstar noma
By: benchrys
15
.........Ngrrrrr ngrrrrrr huo ulikuwa ni mlio wa simu yangu nilinyanyuka kiuvivu ili niweze kujua ni nan anapiga simu mda kama ule halafu ukizingatia namba ngeni.. Niliichukua simu yangu kisha nikaslide iliijipokee lakini nilipopokea hiyo simu sikuweza kutoa sauti yoyote wala kuongea chochote baada ya mda kidogo alianza yeye mwenyewe,,,,,, hallo ben vipi mbona sikiizi adimu sana hata huonekani yani upo wapi rafiki yangu....ilisikika vyema hiyo sauti masikioni mwangu nikaja kugundua kwamba huyu ni jane lakini kwanini atumie namba ngeni sikupata jibu lolote na sikuongea chochote hadi maongezi yanaisha mana nilijua lazima amesetiwa ili aulize ili ijukane niliko kitu ambacho mimi sikuwa tayari kukifanya, nilikata simu nikarudi kulala ila baada ya dakika chache iliingia meseji kwenye simu yangu nilinyanyuka tena kuifungua hapo ndipo ilikuwa ni namba ya jane imetuma meseji inayosomeka "duh nashukuru hujatoa jibu lolote mana mimi huku nimetekwa wakinibana nitaje uliyoko na sitaki unitajie kabisa kwaheli usiku mwema" baada ya kusoma hii meseji nilivuta pumzi ndefu ndio nikala ila kwakuwa walisha niharibia usingizi sikuona hata haja kulala maana macho mda huo yalikuwa magumu basi nilichokifanya nikwenda kuwasha computer ya mule chunbani ambamo nimewekwa ilikuwa ni computer aina ya dell yenye uwezo wa kujitosheleza kabisa cha kwanza nilingia internet kisha nikatafuta maps lengo ilikuwa ni kujaribu kutaka kuyasoma mazingira kupitia computer baada ya mda mfupi ilianza kunionyesha baadhi ya maeneo usiku ule sikulala nikawa tu na computer hadi ilipofika asubuhi.....
.......ilipofika asubuhi nilitoka nje lengo nikaangalie hata kulivo tu ila merry akanambia usitoke huko ben nilimuuliza kwanini tena akasema hebu tazama pale ukutani duuh hata sikuamini baada ya kuwaona baadhi ya watu ambao tuliwaona kwenye huku wakiwa na sura za kikatili kabisa nikamuuliza merry sasa tuna fanyaje hapa akasema wewe rudi kule ndani funua kapeti unaona mlango kisha jifiche huko chini tumbukiza na mabegi yote sawa...niliitikia sawa kisha nikafanya kama kadiri alivonambia.
****aaaah hakuna lolote hapa huyu mjinga hayupo ilieneo tumepoteza mafuta ya bure tu, oya vichaa wangu ee twenzetuni asituzingue bhana... Hayo yalikuwa na maneno ya wale majambazi,,,,, Kumbe walijua ile nyumba ni ya vyumba vitatu kumbe kuna vyumba vingine vya siri ndani na ndio ambako mimi nilijificha huo baada ya dakika chache merry aliingia kule na kusema haya saizi toka lakini usitoke nje mimi naenda kwenye shughuli zangu ila wewe hapo kinachokupasa nikukazia macho yako pale ukutani tuu mana hapo kila kitu cha nje lazima kionekane hapo....."""" hii nyumba ilijengwa kijanja sana ndio kitu nilichokuja kukigundua mana chumba nilichopangiwa hata uwe mchunguzi vipi huwezi gundua haraka kwamba huko ndani kuna chumba isitoshe huko ndani nako kuna chumba kingine cha chini niliupenda sana huu mfumo wa ujengaji....
****huko nyumbani leo walitembelewa na wageni ambao hawafahamiki machoni pao baba na mama aliwakaribisha vizuri kabisa wakapata kifungua kinywa pamoja kisha wakaanza kuongea
Baba: karibuni jaman ningeomba kwanza kuwafamu ninyi ni akina nan na shida yenu ni nini,
Mgeni: sisi ni walimu katika shule ya hapo mbele i mean anaposoma na mwanao ben.... Kabla hajamalizia kuongea yule mgeni baba akapachika swali jingine mnasema nyie ni walimu mbona hizi sura ni ngeni hata pale shuleni sijawahi kumuona hata Mmoja wenu mlifika lini??? Swali hilo lilimpa wakati mgumu yule mgeni aliyeanza kutoa maelezo... Mbona kama unaanza kuwa na wasiwasi ok nambia shida iliyowaleta yule mgeni alianza kujing'atang'ata... A aammm eee i po hivi mzee wangu kabla hajatoa maelezo yoyote baba akasema kwa amani naomba mpotee haraka,,, hawakuwa na jinsi iliwabidi tuu waondoke lakini wakiwa wanatoka kuna mmoja kati ya wale watatu aliangusha karatasi... Kumbe mama nae alikuwa nje aliiwahi kuokota akaingia nayo sebuleni lakini ile anaangalia ndipo aliweza kuona picha ya mwanae ben akajiuliza hawa ni watu wa namna gani kutembea na picha ya mwanangu.
Kumbe katika yale maongezi yaliyokuwa yakiendelea kati ya baba na wale wageni yalirekodiwa na naomi ambae alikuwa dirisha la nyuma ameweka simu yake kama paparazi...
Na hiki ndicho kitu ambacho mimi pamoja na baba tulimpenda sana huyu naomi kichwa chake kipo fasta sana kufikiria.....baada ya mambo yote kuisha kila mtu aliendelea na mishe zake dakika zilisogea masaa yalipita ikawa imeshafika jion meery nae alikuwa akitoka huko kwenye mgahawa wake,,,,_,,,,, lakini mimi nilikuwa nikijiuliza maswali hivi huu mgahawa ndio ulio msababishia hadi anajenga nyumba kama hii kiukweli sikupata jibu lolote maana ni kichwa mtu mmoja hakiwezi kutafuta majibu ya mtu mwingine
Merry alifika pale nyumbani akiwa ni mtu mwenye furaha sana tulipiga stori nyingi sana hadi ilipokuwa inkaribia mda wa kwenda kulala lakini tukiwa tumekaa mimi niling'aza macho yangu ukutani na merry pia aling'aza macho yake ukutani vilevile harafu akasema mabwege hawa ngoja niwape dawa yao alichukua kitu fulani kama kikokotoo au nyie mnaita calculator ya ni hivo kisha akabonyeza baadhi ya namba na kumalizia kwa kusema hii nyumbani ni yangu sikujenga ili mnitenbelee kilio chema.....baada ya kubonyeza ni kweli nilianza kusikia vilio kule nje kutoka kwa wale watu kisha akasema ben siumeona nnachofanya kiukweli hii nyumba sihitajigi mlinzi mana nao ni wezi tuu niliitikia vizuri baada ya hapo......itaendeleaaaaaaaa
benchrys.blogspot.com