Ijumaa, 4 Novemba 2016

Asmet cav tz

Asmet cav tz new video song... Hellow click neno download ili kuipakua na kuitazama

>>>>Download

Ijumaa, 21 Oktoba 2016

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 19

Tuliposhia>>>>

---baada ya kuingia kwa mganga bila hata hodi ghafla nikabadilika na kuwa kuwa ninja, niliweza kujiona kupitia kioo ambacho kilikuwa mbele yangu
Kiukweli nilikuwa natisha sana hadi mwenyewe nilijiogopa usoni hata kipande kidogo changozi hakikuwa kinaonekana ila kulikuwa na maski ambapo inangaa sana huku kwenye alama za macho kukiwa na vitobo vitatu kwa kial jicho ambapo kila kitobo kilionekana kinatoa kama miale ya rangi tofauti kijani, nyekundu na nyeupe
Ilikuwa nikigeukia upande huu tuu unawaka mwale tofauti hii hali hata mimi mwenyewe sikuweza kuielewa ila nilijali mimi ni nini kimenileta

Wakati huo mganga nae alikuwa anapiga piga kama kangoma fulani ambako kamepakwa baadhi ya rangi. Alipiga kwa mda fulani huku akiwa anaongea na baadhi ya maneno ambayo baadhiniliyasikia na mengine hata sikuweza kuyasikia na kuyaelewa lakini niligundua kuwa huyu hizi nyimbo zake ni za kushangilia kitu fulani lakin bado sikujua anakishagilia anachokishangilia ni nini
Baada ya hapo alikitupa kile kingoma chake kidogo mbali kidogo ambapo mimi nilipoangalia niliona kama ni ukuta lakini cha ajabu kilekingoma kilipitiliza na kitua upande wa pili na kwa gafla tuu pakawa na uwanja mkubwa sana

Kwa akili yangu nilishajua kwamba kuwa wadudu lazima anatumia kupiganishia kitu ambacho kinataka kushindana na yeye na ndio maana anafanya huu uchawi ili ajihadhali mapema na kitakacho tokea hapa
Baada ya hapo nikiwa nimesimama mara nikweza kuona mnyama wa ajabu sana ambae hata sikuwahi kufikilia kama ipo siku nitaweza kumwona katika macho yangu

Mnyama kwa kumwangalia alikuwa na meno yasiyopungua kama mia mbili ikiwezekana ni zaidi hata ya hayo
Alitoa sauti ambayo ilisababisha hadi tetemeko kubwa sana katika uwanja ule baada ya hapo akaanza kun fuata kwa mwendo wa maringo
Na mimi kwa haraka hata sikulaza damu niliuchomoa upanga wangu huku kwa mbali nikimwona mganga anacheka huku ameshika kitu fulani mithili ya mkia wa ngombe na kuuzungusha kwa satili ambayo yeye aliijua zaidi
Mara yule kiumbe alijizungusha baada ya kumwona upande wake wa nyuma alikuwa na mkia wenye unene kama gogo la nguzo ule mkia ulikuwa ukija kulikuwa na upepo ukivuma kam kuna ndege aina ya helkopta ipo upande wa juu yangu akili yangu iliweza kugundua kwamba huu unatakiwa unitandike
Ule mkia ukiwa jiran niliruka juu ili kuukwepa ambapo ukaenda kugonga nguzo moja ambayo ilikuwa jiran na uwanja ule na baada ya hapo ile ilivunjika na kudondoka chini hii ni kuonyesha ule mkia uzito wake na nguvu zake ni hatari tupu

___upande wa pili baba tayari alikuwa amesha rud kutoka kazini kwake jioni akafika na kuanza taratibu zake huku akiita boniiiiiiiiiiiiiiiii, boniiiiii uko wapi mbona sikuoni

Na baadaya kuona kimya aliamua kuchukua simu yake na kunipigia iliita kwa mda mrefu sana kisha akapokea majibu
MTEJA UNAEMPIGIA HAPOKE_____
Hakutaka kusikiliza sana akakaa simu na kisha akaendelea kufanya mambo yake mengine, kwa wakati huo ilikuwa ni saa kumi na mbili za jion
Baada ya kufanya kila kitu kilicho kuwa katika ratiba zake
Ulikuwa mda kamili wa yeye kula ili aweze kulala au kujisomea vitabu vyake
Muda wote huo alikuwa ni mtu mwenye mawazo sana. Kuhusu mwanae bon ameenda wapi hadi mda huu aliangaliaa saa yake ilimwonesha ni saa mbili karibia na nusu ila akahisi labda nitakuwa nimeenda kwa joel kwa maana ndio mahali ambako mara nyingi napenda sana kwenda kutokana na kwamba tulikuwa na urafiki wa kitambo sana
Baba alikuwa kisha akafunga safari ya kwenda kwa akina joel, lakini akakumbuka kuwa pale nje palikuwa na vifaa vya utengenezaji wa barabara, aliamua kuzungukia ili akaangalie kama wameishia wapi katika hiyo kazi yao ya kufanya uwekezaji kwenye nyumba ya mtu.
Baada ya kufika kule nyuma ya nyumba yake aliona hakuna kitu chochote
Alicheka sana huku akijisemea MLIJUA KUNA MAJINI NA BORA MMEONDOKA WENYEWE ASANTE MUNGU KWA UAMUZI ULIOUTOA.alifurahi sana  kisha ndio akashika njia ya kwenda kwa akina joel alitembea kwa mda mfupi tuu na baada ya dakika kama tano na sekunde tayari alikuwa tayari ameshatia mguu pale, ambapo alipokelewa na baba ake na joel
Ooooooh karibu baba bon
- ah asante nimekaribia kwema lakini
Hapa kwetu kwema kabisa sijui utokako
- nako nadhani kutakuwa ni kwema hivo hivo
Haya karibu ndani ila mbona umetembea pekeyako na bon umemwacha wapi tena
Baba baada ya kusikia hivi akajua kwamba mwanae bon na hapa hayupo hapo ndio mawazo yaliongezeka zaidi akazidi kujiuliza kichwani mwake maswali mengi zaidi na asipate jibu lolote, ila kwa safari hii alijifariji kuwa
Aaaah mawazo ya nini wakati sio mtoto mdogo___akiw anaendelea kufikiria bado baba joel akauliza tena lile swali lake +=bon umemwacha wapi pekeyake (

Hivi unavoniona nimekuja hapa huku nikijua kuwa bon nitamkuta hapa lakini kumbe na hapa hayupo tena

Duuuh hili tatizo sasa kwahiyo unaenda ktnagza au unaacha tuu(aliuliza baba joel
Safari hata sihangaiki kutangaza inamaana bon bado mtoto mdogo namna hiyo kila siku niwe namtangaza tuu si hata vituo badae vitanichoka maana vinaona kila siku matangazo yangu tuu kwenye redio tena kuhusu mtoto ambaye akili zake ziko sawa kabisa, huwezi jua ni kwanini ameondoka pengine akirudi atasema alikoenda hebu tusubilie tuu (aliongea baba

Kisha baba joel akajibu sawa kuonyesha amekubaliana na mwazo ya baba
Jamani majirani basi mimi niwakimbie au mnasemaje(alikuwa baba akiaga na kusimama lakini baba joel akasema ngoja nikusindikize hadi kwenu maana wewe upo wewe tuu kila siku
Sikumoja moja hahahahahahhaaaa. Walicheka pamoja kisha wakaanza safari ya kwenda nyumbani walifika hadi nyumbani ambapo baba joel alifika moja kwa moja pale kwenye meza ya baba ambayo anatumia kujisomea vitabu vyake,.
   Jirani naweza kuangalia chochote hapa au marufuku kugusa kitu
Ahaa kwenye hiyo meza wewe angalia tuu ikiwezekana kaa kabisa hadi kesho hadi utakapo ridhika kuangalia

Baba joel baadaya kuruhusiwa kuangalia chochote kadiri alivoomba alikaa na kuanza kupitia vitabu vile lakini akiwa anaendelea kutazama kuna karatasi fulani aliona maneno yanayoishia BY NON, kwa haraka akaliwahi na kutaka ajue kuna nini ndani yake alipofungua alikutana na ujumbe ambao ulimfanya amwite baba ili wasome pamoja. Waliusoma ila wakabaki wanajiuliza mama yake alimwona wapi

Tukirudi kwa mganga tunamwona bon amelala chini akiwa hana nguvu kisha-----itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 18

Tulipoishia>>>>>

Walimsogelea lakini ile kumgusa tuu walisikia kishindo kizito sana juu ya gari moja walilokuja nalo pale wote walishtuka na kuangaza macho ule upande ambao kimesikika kile kishindo, lakini hawakuweza kuona chochote mmoja waoa kachukua saa na kuangalia ni saa ngapi mda ilikuwa inaonyesha ni saa 9 na nusu usiku
  Mmmmh ila kuna watu hapa duniani wapo kwaajili ya kuwapa watu mateso ivi mwenzenu sijawahi kufikilia kuwa nitakuja kufanya kaza ya ulinzi lakini leo ndio mara yangu ya kwanza ivi wenzangu mmeonaje kuhusiana na hili swala la sisi kulala kama mapopo hivi huku tukilinda magari ya mtu bila malipo yoyote yale huu uboya.(alikuwa akiongea mwenzo mmoja)
    Aaaaah na wewe unangea nini bhana mimi nawaza kama yule jamaa akija tena hapa ambae ametupa kichapo itakuwaje mana saizi yenyewe mauza uza kibao mara vipite vivuli tuu kama hvi saiv kishindo sijui ni cha nini, shit huu uboya mi naamsha hata sasa hivi ambaye yupo tayari twenzetu
Baada ya kuongea vile alianza safari yale na kwa kuwa nyumbani kwao hakukuwa mbali sana wote waliungana na kuondoka lile eneo bila kumwacha hata mmoja wao

____ilifika asubuhi boss wao alikuja na kuanza kukagua kama waliweza kumwona baba lakini cha ajabu alifika na kuyaona tuu magari yake yakiwa pekeyake pale
Kwa mawzo yake alielewa kwambayawezekana wamelala ndani ya magari kwahiyo bado watakuwa hawajaamka
Akalifuata gari moja na kuchungulia kwenyekioo lakini hakuona kitu akafuata jingine nalo aliona ni hivo hivo. Hapo akajua kwamba hapa wala hakuna mtu alianza kuongea pekeyake
IVI HAWA WATOTO WA MTU GANI, WAMEKIMBIA NA KUACHA MAGARI YANGU HAPA HUKU NILIWAPA KAZI YA KUFANYA. SASA NTAMTAFUTA MMOJA BAADA YA MWINGINE.
Baadaya baadaya hapo alitoa simu mfukoni na kumpigia mtu mmoja
Yaa ndio mheshimiwa, aah ndio, sasa nilikuwa nahitaji mtu wa kuendesha scaveta kama watu watatu hivi nataka wakaniondolee sehemu moja hivi vyombo vyangu, ok sawa ukipata nambie, yaah hakuna tatizo kabisa, ok asante sana.
Baada ya hapo akashusha simu yake na kuingilia moja ya gari kisha akaondoka nalo

_____ilipofika mda wa kazi baba kama kawaida aliondoka na kwenda kazini kwake na kuniacha pale nyumbani
Na mimi nilipoangalai ratiba zangu nikagundua kwamba hii ni siku nzuri ya kwenda kumwangamiza yule mganga ambae ndio hufanya kazi  na akina babu na bibi ili kuwapoteza ndugu zetu
Nilichukua begi langu na kuweka baadhi ya vitu kisha nikachukua karatasi na kuandika maneno fulani kwa kalamu ambayo yalisomeka
SAMAHANI BABA NAJUA UTAJIULIZA SANA NIMEONDOKA NA KWENDA WAPI,. ILA UKWELI NI KWAMBA NIMEENDA MAHALI KWAAJILI YA KUTEKELEZA MAAGIZO AMBAYO NILIACHIWA NA MAMA MARA YA MWISHO KUONANA NAE,.. BY BON
Kisha nikaifunga na kuweka sebuleni kwenye meza yake ambayo mara nyingi hupeda kukaa na kujisomea vitabu vyake. Na baadaya hapo nikaondoka na kwenda katika duka moja ambalo lilikuwa linajishughulisha na kuuza pikipiki nilinunua pikipiki moja aina ya boxer nilipohakikisha kila kitu kipo sawa nianza safari yangu rasmi ya kwenda kwa mganga
Safari hii ilichukua masaa kama saba hadi kufika maeneo ambayo nilikusudia lakini nikakumbuka kuwa mganga huyo anaishi jirani na mtaa wa mawen ambako niliacha vitu vyangu baada ya kuondoka na kwenda kwa baba.
Baada aya hapo niliamua kugeuza na kwenda pale lakini nikapitia ili kuapata baadhi ya mahitaji yangu, nilifanya hivo kisha nikaenda hadi pale nyumbani

Nilipofika niliwaona akina asha na mwenzake amina wakiwa wamekaa tu nje wanaotea jua la jion
Uso wa asha ulionyesha unafuraha sana lakini hawezi hata kusema anishingilie kwa maana hata jina langu hakuna anaelijua katika ile nyumba

Baadaya kufika niliapaki pikipiki yangu nje na kuingia ndani huku nikiwa na badhi ya mafurushiyangu niliyotoka kununua huko ila nikakumbuka hakuna jiko humu ndani nilitoka tena nje na kuchukua pikipiki yangu kisha nikaelekea kwenye maduka yanayohusika na kuuza majiko. Nilifanikiwa kuliona duka moja ambalo ndio walikuwa wamepanga majiko mengi sana nje pale, mwendo wa fasta tuu nilisimama na kufuata lile duka ili niulizie jiko lakini nikiwa ndio nafika mlangoni nyuma nilisikia mtu anapiga lesi kwenye pikipiki yangu. Akili yangu ilinituma kwamba hapa nitaibiwa halafu nishindwe kufanya kazi ambayo imenileta hadi huku.
Haphapo niligeuka na kurudi hadi kwenye pikipiki nae alipoona narudi kwakuwa kuondoka alisha chelewa akaamua kushuka akiwa nalengo anipige ili yeye apate kuondoka na pikipiki
Alifika kichwakichwa tuu na kunirishia ngumi asijue mi mtu wa namna gani
Ile maurusha tuu mkono niliudaka haraka na kuuvunja kisha nikamwacha pale akiwa na maumivu ya kuvunjwa mkono yani ilikuwa ni ndani ya nusu dakika tu tayari mtu ashaachiwa ukilema kisa wizi
Niligeuka na kurudi tena kwenye majiko kisha nikachagua jiko linalonifaa na kuchukua pikipikikisha nikaondoka na kurudi nyumbani ile nimekaa nyumbani mda kama wa saa tatu hivi nikawa sauti kutoka nje watu wanaongea
+++nilisikia anakaa  hapa tena nahisi ni humu ndani kama siyo ngoja kwanza tukagonge ili tuone kama kweli
Sema mwanangu inatakiwa tuingie kwa akili sana mana asije akawa ni mtu wa hatari mana ukifuatilia tangu anaingia tuu siku ya kwanza usiku ni mtu ambae hata hapendi ujinga ujinga na mtu licha ya kuwa anaonekana ni mpole sama kwa usoni.
Kudadeki acha uoga wewe inamaana tumetembea tuu bure mwenzetu amevunjwa mkono halafu tulifumbie tuu macho suala kama hili kwa upande wangu mimi sikubaliani hata kidogo yani ama zake ama zangu liwalo na lile.(walikuwa wakijibizana hivo wasijue kwambakila wanachoongea nimesha kisikia tayari
Baada ya hapo walifika hadi mlangoni kwangu na kuanza kugonga kwa fujo kweli
Ngongongongo
Nani unagonga (niliuliza kisha nikajibiwa
Binadamu..ok sawa kama wewe ni binadamu nahisi mimi ni binaugali au maji sawa kaa hapohapo kama mlinzi kama huwezi kujitambulisha sawa
Halafu acha uboya hebu fungua mlango vipi wewe utajuaje kama mimi ni balozi?
Sidhani kama balozi unauhuru wa kutoa majibu ya chooni kama hayo kwa usalama wako nakuomba tuu ondoka (niliwaambia hivo  badaya kuona kama wananiletea nyeusi tuu)
Na hapa haondoki mtu sasa hadi kieleweke tuu(walinijibu )
Poa ngojeni kwanza kitaeleweka tuu hata msijali nisubirini nyie si ndio wasumbufu wa nyumba za watu.>baada ya kuongea vile nilinyanyuka na kutokea dirishani kisha nikawazungukia hadi mlangoni na kuanza kuwafumua tuu makofi kama naadhibu mwanangu hivi. Baada ya kuona makofi tuu wamelizika waliamua kuondoka mbio na kurudi makwao

Baada ya hapo kwa kuwa nilishukuwa nimekula na kushiba safi kabisa nilichukua pikipiki tena na kuondoka hadi kwa mganga kisha nikapaki pikipiki mbali kidogo kisha nikaingia hadi ndani bila hata hodi------itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 17

Tulipoishia>>>>>

Baada ya mimi kutoweka pale ile gari ilisogea hadi jirani kabisa kisha akashuka yuke baba aliyeyejitambulisha kwa jina la mkuti kule ofisini kwa baba
JAMANI YULE KIJANA YUPO WAPI NAMHITAJI ILI NIKAMPELEKEE BABA AKE MAITI YA MWANAE MAANA ANANILETEA DHARAU AMBAZO HATA SIZIELEWI(laiti angejua jinsi alivokuwa anawaboa hawa wafanyakazi wake ambao aliwapa ile kazi hata asingethubutu kuongea yale ambayo anayaongea kutoka mdomoni mwake mda huu
Jamani hivi sinawauliza nyinyi au siongei na nyinyi mimi tayari nimeshakuwa chizi au. Licha ya yeye kuongea maneno mengi mfululizo lakini hakuna aliyeweza kunyanyua mdomo wake ili atoe angalau hata jibu maana wote pale walikuwa wanaugulia maumivu ambayo wameachiwa kama zawadi na bon a.k.a ninja halafu yeye anawaletea nyeusi. Mmoja uvumilivu ulimshinda akaamua kupwayuka tuu
<<<<mzee kama uliona kazi sio lazima sana kuifanya ni bora ungeniacha niendelee kusafisha tuu mitaro kule ulikonikuta sio kuanza kuagiziana watu ili watufanye vilema tena bila hata faida hata ya mia mbovu, sihitaji niongee sana cha kufanya nipe tuu changu kwa maana umenisumbua tuu na hakuna nilichokipata

Boss wao baada ya kumsikiliza sana akaona huyu tayari asahaanza kuwa kichaa au kachanganyikiwa na maisha hadi anapwayuka maneno kama haya.
Aisee nimekusikiliza sana lakini hata sijakuelewa kwa lolote labda saizi hapa naomba kujua unamaana gan kuongea maneno kama hayo ambayo unayaongea. Baada ya kuongea hivo akamgeukia mwingine lakini wote sura zao zilikuwa zimekunjamana mbaya hadi boss akaanza kujiuliza maswali inamaana hawa watu wameamua kumnunia, ila bado akajiuliza inamaana ile pesa aliyowapa haijatosha chochote au ndio mbongo huwaga hawezi kulizika akapepesa macho huku na kule ili amwone yule ambae alimkabidhi ile briefcase yenye hela za kuwapa wenzake lakini hakumwona, akaanza kutembea tembea kidogo kwa mbele aliweza kuna mtu amelala chini kama amekufa vile lakini aliposogea hadi jirani aliweza kugundua kuwa bado anahema akajaribu kumsogelea jirani nakumtikisa ili aone kama anaamka, kwanza akashtuka kuonandio yule ambaye alimkabidhi ile briefcase yenye pesa zile. Lakini akabaki na maswali inakuwaje hadi yupo katika hali hii. Alijaribu kumwamsha ili hata mawili tuu lakin hakuamka, hapo boss andio akajua kwamba huyu kazimia lakini bado hajajua ni kwasababu gani hadi amezimia pia akawa anajiuliza mbona na wale wengine wapo katika hali ile
Akiwa anaendelea kujiuliza akageuka nyuma kuangalia vifaa vyake kama vipo sahihi bado kwanza aliangalia lile gari ambalo walikuja nalo akaona vioo vya upande wote vina vumbi la hatari sana kana kwamba hata kama ndani kuna kitu huwezi kuchungulia na kuona chochote kidogo nae achanganyikiwe

_____bon_____
Muda wote baadaya kumaliza kazi ya kuwatuliza wale wafanyakazi wa mkuti niliingia ndani na kufungua ile briefcase kisha nikaanza kuhesabia pesa ambazo zilikuwa mle ndani ya brifcas nilihesabu huku masaa yakiendelea kwenda ila nikakumbuka baba sio mda mrefu sana anaweza akarudi sasa akifika hawa bado wapo hapa nje lazima waanze kumsumbua na mimi sitaki hata mtu mmoja ajue kuwa bon ni nani katika upande wa mkono, nilichokifanya ni kupiga simu kwa baba na kumwambia leo itabidi kidogo achelewe kurudi hapa nyumbani kisha nikamwelekeza ni kwanini namwambia hivo,,. Baba nae alinielewa kwa haraka kisha akakata simu nakuniambia atakapo kuwa anarudi atanambia kupitia simu kisha simu ikakatwa

Huku nje baada ya kukaa kwa mda mrefu kumbe ni kweli walikuwa wanamngoja baba ili wajue siri ya hili eneo kumbe hakuna siri yoyote ile isipokuwa tuu wameingia kwenye mikono mibaya na kujikuta wakikunjwa kama chapati inaandaliwa kunywewa na supu

Walikaa sana masaa yalienda hadi ikafika usiku wa saa nne hivi wakajisemea hapa hakuna mtu kutoka hadi tujue hatima ya huyu mzee
Ila mmoja waoa akasema>kinachomchelewe nini mbona sijawahi kuona mzee akiwa ananajaribu hata kunywa au kwenye sehemu za starehe sijawahi kumwona
    Ivi kuna binadamu ambaye unaweza ukakariri tabia yake kwa jumla we kaa hapo hadi arudi ili na sisi tupate chetu sawa chogo
  Kudadeki tutazinguana hata kama ni usiku tena maeneo ya watu nani chogo tabia kama una*****

Wewe nikaushie huko hasira nyingi halafu hujiwezi mamaza mengine bhna

Halafu nyie acheni uboya huo(kilisikika kibezi kikitokea upande mwingine wote waliogopa kumbe alikuwa ni mwenzao) nae baada ya kuona wameogopa na kutulia akacheka na kuwaambia mnajifanya mnachimbana kumbe wote manyoro tuu shit

____kwa bashir ___mda wa saa mbili kama nusu tunamwona bashir akiwa anatoka kwa asha wpangaji wenzake wakamwona kisha wakaanza kucheka baada ya kuona anajinyoosha kama alilala juzi vile na miayo mingi kweli ila aaaaaamh kama anataka kummeza mtu vile

Hahahahahaaaaaa bashir kichaa lao mbona upo hasso hivo vipi tena ulikuwa na mtanange au (alikuwa ni rafiki yake mmoja kwa jina la john
Licha ya kuongeleshwa hayo maneno mengi lakini bashir hata hakujibu chochote maana kwanza alikuwa akachoka sana isitoshe alikuwa na njaa sana mana toka azimishwe mchana hajaamka hadi saizi ndio anakurupuka
Alienda moja kwa moja hadi kwenye chumba akitegemea atamkuta mke wake lakini chaajabu aliona hata taa imezimwa kuonesha dhahiri kwamba humu ndani hakuna mtu kwa wakati huu. Aliingia ndani na kuwasha taa yake lakin bado hakuona mtu ila alishangazwa baada ya kuangaza mle ndani aligundua kuwa kuna baadhi ya mabegi hayapo mle ndani. Alianza kama kichaa au kapandwa na mapepo doriii, dorii hadi wapangaji wengine wakawa wanajiuiza inamaana dori bado yupo tuu
Kumbe mke wa bashir aliitwa dori na inaonyesha dori ameondoka kaenda wapi haieleweki
Bashir akabaki mdogo zaidi basi hakuwa na njia nyingine aliamua kuchukua pesa yake na kwenda kwa mama ntilie ili akapate chakula alale ili aione kesho

____bon__nikiwa nimekaa tuu mle ndani meseji iliingia kwenye simu yangu nilipotazama niligundua kuwa ni baba., nilinyata hadi kwenye geti kumbe nae alikuwa kabana kwenye maua ambayo yalikuwa jilani na geti nilipofungua tuu geti mara moja nae akaingia ndani kisha tukafunga geti tukala la kisha mimi nilienda kulala na kumwacha baba pale sebuleni
Na huku nje wale waliopanga kukutana na baba bado tuu walikuwa wakingoja huku wakiwa na imani kwamba bado hajarudi na ndani ya nyumba nipo mimi tuu pekeyangu

Wakiwa bado wanazunguka nyumba yetu mara wakahisi kama kuna kitu kimepita tena kasi hadi kinaacha upepo wote walistuka na kuwa makini sana ili kukiangalia kama kitapita tena lakini hakikupita tena.
Ni kama saa sita usiku yule aliyekabidhiwa hela na boss ndio alikuwa anazinduka akiwa na maumivu sana upande wake wa mgongo mana ndio ile ngumi ilikokita. Alianza kujinyoosha kwa kupiga kelele kama mtu anatapika vile na kulia humohumo hadi wale wenzake walishtuka ila wakagundua kuwa ni mwenzao ndio anaamka walimfata na kumshika, lakini ile kumgusa tu-----itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 16

Tulipoishia>>>>

Bashir baada ya kugonga mlango na kuona hafungiliwi aliamua kuusukuma kwa nguvu ili aingie ndani kumfunza adabu huyo asha ambae yeye mara nyingi ni mshabiki kipindi kama bashir akiwa kakutana na majanga hasa ikitokea amepigwa na mtu fulan
Bashir alitumia nguvu hadi alifanikiwa kufungua ulemlango lakini alipoingia ndani kabla hajaweza kuona chochote alipigwa na kitu kizito kichwani kwake kilicho mpelekea hali ya kuweweseka na kuanguka chini puuuuuu kama mzigo kisha asha akaanza kushangilia kuwa ameweza kujitetea na mbaya wake baada ya hapo asha alitimuka na kutoka nje hadi hadi kwa rafiki yake amina hata kama walipigana ila bado utani kwao ulikuwa ni wa damu kabisa
Shogaangu nifungulie mlango basi
Jiheshimu wewe umefumaniwa au inakuwaje mbona upo haraka hivo
Ahaa we acha tuu nifungulie kwani tuongee bhana,. Usinizingue hebu ngoja kwan nifanye yangu ndio nafungua kaa hapohapo kama mlinzi sawa., daha kwakuwa ni kwako nakaa ila usinzingue., asha hakuwa na namna nyingine zaidi ya kumngoja tuu amina amfungulie mlango wake

Mlango ulifunguliwa amina akaingia ndani huku akiwa kama hajiamini hivi,.. mana bada ya kuingia tuu ndani aliufunga mlango tena kwa ndani kisha akaanza kumwelezea

Ivi wewe leo unanini wadudu wako leo inaonekana umewapa maji ya moto haya niambie kinachokukimbiza namna hii nini
Shogaangu we acha tuu bashir alikuja akangonga mlango wangu sikufungua maaana nlishajua kabisa anataka anipe kipigo
Basi akalazimisha had amefungua___alieleza maelezo yote kisha wakacheka sana kwa maana asha alivofanya alionekana kama shujaa sana kwa kumkomoa bashir licha ya kuwa amezimia wao walishajua ataamka tuu.,>>>>

>>>>ilipofika asubuhi nyumbani mimi na baba tulifanya utaratibu wote kisha baba akaelekea kazini kwake hukuakiniacha tuu pale nyumbani sikukaa sana nikaondoka na kwenda kwa joel ambae nilipotezana kitambo kidogo
Ngo ngo ngo hodiiiii
Hodiiii wenye wenye nyumba
///mmmmh hii mbona kama sauti ya bon hivi ngoja nikacheki kwani,. Alikuwa akiongea vile joel mda ule yupo na babaake.
Joel alisimama na kuja hadi mlangoni ambapo hakuamini kukutana live na uso wa beni maaana ni miezi mingi sasa imepita tangu nipotee na kutangazwa kwenye baadhi ya vituo vya redio lakini bado sikupatikana
    Dahaa  babaaaaa ni bon kweli aisee daah nambie mwanangu mbona adimu sana ulipotelea wapi mana kitambo kinoma
Dah mdau mi nipo mbona sema mambo ya hapa na pale tuu ndiyo yanafanya hadi hatuonani nilimjibu vile huku nikijua kabisa hata weza kuridhika kabisa na hili jibu. Kisha akaendelea kuongea
Bon unazingua mishe za hapa na pale huku tangu skuli watu tulikutafuta kinoma mahafali yenyewe ulisepa hukuonekana, au ulipata mishe kabla hata hujapata cheti cha umeme?
Usijali ntakutonya tuu ngoja nikamcheki mshua si yupo humo ndani au
Yah yupo ndani((((tuliingia ndani huku tukiwa bado tunaongea mambo meng tuu kisha nikafika na kumsalimia baba yale lakini nae alionyesha anashauku ya kujua wapi ambako nilipotelea kwa mda wa karibia mwaka mzima sijaonekana hadi wananitafuta bila mafanikio,. Lakini wote niliwaambia ni stori ndefu sana

Tukiwa tunaendelea kupiga stori pale kwa akina joel mara gafla tuu nilipitiwa na usingizi na kuanza kuota nyumbani kuna greda na d6 yapo yanavunja nyumba. Hii ndoto ilinishtua sana hadi nikajikuta nikinyanyuka pale kwenye kiti huku nimechoka sana
We bon vipi mbona kama hatupo wote hapa unasinzia ndani ya dakika tano na kushituka kama ulilala jana vipi bhana kuna tatizo au(aliuliza hivi babaake wa joel lakini sikujibu kitu nikasimama na kuwaaga kuwa mi naenda wote hawakuweza kuelewa ni nini maana ya hili jambo lakini ukweli wote ulikuwa ndani ya moyo wangu
Samahani mambo yakiwa vizuri badae nakuja hata kukesha tuu ila kwa saizi naomba niende nyumbani. Sikuhitaji ruhusa nikafungua mlango na kuondoka ili nikaone nyumbani kupo katika hali gani. nilipiga hatua za haraka haraka sana kwa mda mfupi tuu tayari nikawa nimeshafika nyumbani.
Nilipofika nyumbani nilishangaa kuona kuna magari ya wide road yapo pale huku pembeni kuna greda moja na d6 moja kwa mbaaaali nikaona kile kigari cha kushindilia nacho kikija usawa wa pale nyumbani

Sikutaka kubaki kimya nikaamua kuuliza
ETI SAMAHANI HIVI VITU VINAELEKEA WAPI
Aliyekuwa jirani akanijibu vimesha fika
Nikamuuliza tena inamaana hii nyumba inavunjwa nae akanijibu ndio tuliagizwa na boss
Mara akaja mzee mmoja na briefcase kisha akamkabidhi mmoja wao na kuwaamuru kuwa huyu kijana mwangamizeni kwa haraka sana inavowezekana pale pale wote walinigeukia na huku wengine wakiwa na sepetu a.k.a spedi nyie mnaita na kuanza kunifuata nazo nikaona namna yakufanya hapa ni kukimbia tuu na sio njia nyingine
Baada ya kuona upenyo nilitoka spidi kali kama upepo wote pale walibaki tuu wakishangaa wasijue nimeenda wapi wakiwa wametulia bado wanafikiria nitakuwa nimeenda wapi ili wanifuate watimize kauli ya mkubwa wao
Mara ukaja upepo mkali sana eneo lote lilikuwa ni rangi ya vumbi tuu hii ni style ambayo niliisoma katika kile kitabu kidogo ambacho niliachiwa na mama ninapoagana nae mara ya mwisho kule kwenye lile jumba
Baada ya upepo kuvuma wengi walianza kujiziba usoni kuzuia vumbi
Hadi yule aliyepokea ile briefcase yenye hela alijisahau ile anageuka aangalie zile hela ile briefcase ndo kwanza akaona inazamia kwenye upande wa pili wa paa la nyumba hakuweza kuamini akataka apwayuke kwamba watu waingie mle ndani lakini kabla hajaongea chochote alitulizwa na ngumi yenye uzito kama tufe kisha akatua chini puu akiwa hana hata fahamu kitendo kile wengine nao walikiona baada ya hapo wakamwona ninja akiwa katokea upande ambao upepo ulikuwa umetokea hapohapo wote waklidamka na kuanza kusogelea silaha zao ambazo ni sepetu mapanga wenye spana walichukua spana zao na kujipanga ili wapambane nami sikakawia nilitoka na mwendo wa kasi huku nikiruka juu na kuzunguka nikaachia mateke kwa watu watatu mfululizo ambao walienda kuwasukuma na wenzao kama watatu tena. Baada ya hapo nikasimama kati ili mtanange uanze na hii siku nilishawapania wakijifanya wabishi sana nachinja mmoja wao ili uwafundishe na wengine.
Walianza kujongea huku wakizishika silaha zao kiufundi lakini mimi nilitoa tuu nyororo moja yenye goroli kibao na kuanza kucheza nayo, kila ambaye ilimpata alikuwa ni lazima akajifiche kwenye magari ya kazi niliwafunza wote hadi wote tayari wakawa wapo hoi kisha nikaongea kwa sauti fulani ya bezi la kulazimisha
      ONDOENI UCHAFU WENU TENA NISIWAONE KABISA KATIKA HILI ENEO kisha nilimshika mmoja na kumrusha kule
Katika hawa wote hakuna aliyeweza kugundua kama ni mimi mtoto wa MPL ndio ambaye nimefanya hivi maana wote waliamini mimi nilikimbia mapema kabla ya zari kumbe niliwapangilia.
Wakiwa wanaanda magari yao ili waondoke wakampe taarifa boss wao, mara waliona kwa mbali kuna gari linakuja, kwakuwa hata mimi hilo gari sikulitambua sikupoteza mda nilichumpa juu sana na kupotelea kusiko eleweka lakini ndio ilikuwa ndo njia ya mimi kuondoka pale------itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 15

Tulipoishia>>>>

------baada ya kuingia duka lililokuwa jiran nae aliweza kujieleza ili apatiwe msaada wa kupata simu ili apige nyumbani
Nani akuamini wewe na wakati unajua kabisa umeniona pale duka la simu ukanipiga kibega tena kwa maksudi na yule dada anakuambia ila ukajifanya unaleta maringo kana kwamba hela zako ndio zinazosumbua sana watu wote (aliongea vile yule dada ambaea alikuwa katika m pesa fulani kule mjini

Dadaangu nisamehe na mimi ni binadamu tuu kama ni simu nitalipa tuu ila naomba msaada huo nisaidie
Yaani hapa enock alikuwa mdogo ghafla tuu mana yeye hakuweza kuriri sura ya mtu ambae amemharibia simu yake. Baada ya kuomboleza sana ndio alipewa msaada wa kuongea na simu alimpigia baba ake nyumbani na kumwambia amevamiwa na kuporwa hela zote lakini simu tuu ndio imeachwa, kwakuwa alikuwa ni mtoto wa pekee kwa huyu mzee mda huohuo tuu ziliingia hela mpesa kwa namba ya yule dada kisha wakaitoa, enock alishukuru sana kwakuwa alisaidiwa, baada ya kuhesabu hela ambazo alikuwa akihitaji alichukuwa kiasi kama cha laki tano na kumkabidhi huyu dada ambae amemsaidia, kisha akasimamisha bodaboda ambayo alitaka imfikishe hadi eneo ambalo lilikuwa na gari yake, mambo yalipokamilika akapanda gari na kupitia sheli ili ajaze mafuta kisha akarudi nyumbani salama kabisa

_____kwa baba______
Wiki moja liliisha na wafanyakazi wote walikutana tena katika ofisi zao na kuendelea  na kazi zao kama kawaida. Ilipita muda kama wa mwezi mmoja hivi walitembelewa na baba mmoja ambae alijitambulisha kwa jina la Mkuti, akadai yeye ni mwekezaji hivo alikuwa anatafuta eneo ambalo ni zuri ili aweze kufanyia shughuli yake. Lakini katika mapendekezo yake akapendekeza eneo ambalo ni  karibia na nyumbani. Baba baada ya kusikia vile akamwambia kwa hilo eneo hata haitawezekana kabisa kwa sababu lile eneo ni dogo sana na pia lilishakuwa na mipango ambayo tayari imeshaanza kufanyiwa utekelezaji, kajaribu sehemu nyingine
Lakini yule mgeni kwa jina la mkuti akaonyesha kama hajaelewa kabisa kuhusu kuzuiliwa na maelezo hayo alichowajibu ni kwamba ataenda kuongea na watu wa serikali ili wamuangalizie kuhusu hilo eneo. Baada ya kuongea vile akaondoka hata hakuhitaji kuanza kukaa tena pale wasije wakaendelea kumzuia zaidi
Aliondoka na kwenda kutimiza kama alivoahidi pale kwenda kuongea na wakubwa ikiwezekana hata kwa hongo ili tuu apate anachokihitaji yeye. Baada ya kuongea nao walikubaliana vizuri kabisa kisha simu ikapigwa kwa baba kumpa zile taarifa za kukatwa kipande cha eneo lake, baba hakutaka kukubaliana nao kabisa lakini kwakuwa walisha kula hongo ya pesa ndefu wakaamua kutumia comand kwamba atake asitake ni lazima tuu eneo likatwe kisha simu ikakatwa hivo
Baba alibaki akijiuliza maswali mengi sana pale ofisini lakini hakupata jibu lolote akiwa ametulia simu yake ilianza kuita namba ngeni aliiangalia kwa kuwa alikuwa na mawazo sana akataka aikate lakini roho ikasita akaipokea
Akiwa amepokea akabaki ameduwaa asiamin kituanachokisikia kwenye simu ile,
Nini wewe bon uko wapi kwa sasa, ahaa basi njoo hadi ofisini kwangu kabisa, ya nipo ofisini ndiyo, ok nakungoja ukifika gonga tuu sekretari akakuleta hadi ndani
----duh bon kaondokaje kule tutajua tuu----

Baba akiwa amekaa ofisini kwake mara mlango ukagongwa
Yes karibu
Waooooooh alinyanyuka na kunikumbatia kwa furaha mana ni kama mwaka umeisha tangu tupotezane pale nyumbani. Ulikuwa ni mda wa furaha sana baba alisahau kama kunamtu ashamtibua mda si mrefu sana,
Baba aliondoka na mimi pale ofisini na kulekea nyumbani lakini tukiwa bado hatujafika nyumbani tupo njiani kuna gari lilikuja na kusimama mbele kisha akashuka jamaa mmoja ambae alionyesha sio mtu mwema hata kidogo. Alikuja hadi kwenye kioo cha gari ambalo sisi tupokisha akasema kwangu wewe dogo sogea kwanza namhitaji huyo  mzee kwanza ninashida nae. Lakini nikaleta ubishi kidogo kwa kumwuliza kwani kama unamfahamu  na unashidanae si bora ingamfata kwa busara tuu sio kumzuia hata asiende mbele,
Dogo acha shobo nimekwambia ninashida na huyo mzee wewe mbona shobo nyingi au wewe ndio powa shuka wewe basi ili nikupe shida yangu ambayo nahitaji huyu mzee aifanye.
Baada ya yeye kusema vile nikamwambia ok nashuka ili niikamilishe hiyo shida yako.

Niliufungua mlango wa gari na kushuka kwenye gari nae akanivutia hadi mbele ya gari ya gari lake baada ya kufika kule akasema sasa nakupa dawa ya shobo zako we siunajitia mwehu sana eeee sasa ngoja, baada ya kusema vile alikunja ngumi huku akijiandaa kunipiga tumboni, nikawa namwangalia tuu bila kuchelewa akanipiga ngumi ya kwanza ya tumbo lakini sikushtuka akapiga ya pili sikushtuka bado alitaka kupiga ya tatu niliudaka mkono wake na kuunyonga ikasikika tuu sauti (koooo) kilichofuatia hapo ni kilio. Nami sikupoteza mda nikarudi kwenye gari kisha nikarudisha nyuma kidogo na kuipisha ile gari yake hadi tunafika nyumbani. Tulifika na kufanya taratibu zote kisha tukala na kulala_____

_____katika ile nyumba ambayo anakaa bashir kulikuwa na mabishano makubwa sana ambapo bashir alikuwa kazongwa na wpangaji wote huku wakimpa vipondo tuu
   Dadeq zako kwa hiyo saizi umeamua uache zile bangi zako na huyu jamaa ungeendelea kuleta shobo zako za kike angekuua wewe eti street fighter jiite hvohvo na saizi.
kantangazeeeeee kweli kila mbabe na mbabe wake. Bashir umepoa kama unasubiri upulize pola, aliongea vile asha kisha amina akamdakia ivi wewe asha mbona na wewe shobo  nyingi kama umejigundua unashombo wakikunyonyoa tu kilio kama umekutana na popobawa, lione kwan
afu wewe shoga au bashir unakuwaga na promise nae mana kila siku ilaonekana kama unajisikia mbaya mno nikiongelea kumhusu kuwa wazi tuu manfongo wewe..
hheheee shoga tena unikome nini.
Hujasikia au ndo mideko. Ushuzi kweli wewe
Amina na asha walisimama na kushikana ilionyesha kwamba kila mmoja ameshindwa kuvumilia yale maneno waliyokuwa wakipeana. Hapakukalika kabisa katika hii nyumba kama kawaida ya wadada wanapopigana matusi ya nguoni ni kawaida timbwili lilitembea kwa mda wa dakika kumi kila mmoja akawa ameenda ndani kwake kwa hasira sana.
Bashir akiwa ameenda kwenye chumba cha bon akakuta mlango upo wazi alijaribu kugonga lakini hakuna aliye jibu wala kufungua mlango. Kwakuwa alikuwa na hasira sana na bon alifungua kwa tahadhali sana na kuingia ndani ambapo aliona kuna vitu vichache tuu mle ndani ilikuwa ni kitanda, godoro na mablanket na shuka zaidi ya hapo hakuna akajisemea leo huyu lazima ajute humu naondoka na kila kitu siachi hata kimoja.
Baada ya kuongea vile akagusa kitanda kwenye kona ili akikague kama kipo vizuri lakini anagusa tuu alipigwa na shoti ya umeme,kumbe ulikuwa ni mtego tuu umewekwa kwa yeyote atayefanya anataka kuingia mle ndani na kuondoka na kitu, bashir kuona vile alikata tamaa tena ya kutaka  kujua zaidi akashika mlango kwa umakini akauvuta na kutoka nje, anapotoka mlango ulirudi kwa kasi sana na kumbonda hadi alienda kutulia kichwa.
HAHAHAHAHAHAHA. HAHAHA BASHIR VIPI TENA., kumbe kile kitendo kuna jamaa walikaa nje pale walikishuhudia vizuri kabisa bila chenga. Baada ya hapo bashir aliondoka kwa lengo akamfunze adabu asha ambae anamdomo sana. Alifika hadi mlangoni kwa asha na kugonga baada ya kuona hafunguliwi alisukuma mlango kwa nguvu kisha------itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I (mimi ni nani)
Benchrys
No. 14

Tulipoishia>>>>

-----simu ilianza kuita nikaitazama ni nani lakini sikuweza kujua namba kwa maana ilikuwa ni ngeni machoni kwangu lakini niliipokea hivohivo, baada ya kuipokea zilisikika tuu sauti za makelele ya watu kibao.
Aaah msinizingue shit,. Kasha nikakata simu na kuanza kuondoka mdogo mdogo kuelekea kule nyumbani ambapo nilipanga____-

Katika uchochoro mmoja ivi kulikuwa na kikundi cha watu ambao walikuwa na mazungumzo yao :-
Aaaah kichaa waangu ivi huyo ngeni ni mtoto wa kahaba gani anae weza kuingilia tuu mitaa ya watu kiholela hivo
Ddduh man hata mimi sijampata hata jina lake ila acha tukamcheki mamake zake huyu, lazima niondoke na kiwiliwili chake nikaange homu kama kitimoto mana kitambo saaana
(kumbe walikuwa ni wavuta bangi ambapo katika hawa wavuta bangi na bashir alikuwa ni mmoja wao) baada ya kuongea saaana walijipanga kwa kuchukua silaha zao kama mapanga, nyembe, makwanja, wengine fimbo kama unavojua wavuta bangi wakisha panga kuleta vurugu. Baada ya hapo wakaanza safari na kiongozi wao alikuwa ni bashir ambae alishika jambia kama silaha yake

____- bon_ wakati naingia tuu pale nyumbani mdada alinifuata akijitambulisha huku hajaulizwa
Kakaangu mimi naitwa amina, mwenyeji wa hapa hapa samahani sijui wewe unaitwa nani mana kama majirani ni vyema kufahamiana vizuri
Niliona kama ananipotezea tuu mda wangu nikataka niondoke ili niingie ndani,. Jamani kaka angu acha dharau naongea na wewe.
Ahaaaa mawazo yapo mbali sana hapa umesemaje kwani, nilimuuliza kama sijasikia vile
Ilimpa wakati mgumu sana kuanza kuongea tena lakini akajikaza hivohivo, nimesema hivi-----kabla hajaongea simu yangu ilianza kuita tena, sikupoteza mda nikaipokea bila hata kuangalia ni nani ambae alikuwa anapiga kisha nikasikia sauti tokea upande wa pili nakuhitaji uje hapa nyumbani sasa hivi tena bila kuchelewa
Nilijua dhahiri kuwa hii ni sauti ya yule mzee kwenye jumba lile ambako nilipelekwa baada ya kutekwa. Niligundua kwakuwa nafahamu kuwa simu ninayo itumia ilikuwa ni ya mwanae aliiacha baada ya kwenda shuleni

Niliposikia amesema vile hata sikujibu chochote nikakata simu ile.
Enhee ulikuwa unasemaje nilimuuliza amina lakini hakujibu chochote na kuondoka spidi huku akiingia ndani kwake. Kumbe kile kikundi cha mateja tayari kilikuwa kishafika pale

Boya lenyewe ndio lipo wapi au umetuenjoi tuu hapa bashir onyesha fasta bhana ninahamu ya damu///aliongea teja mmoja kwa bashir ili bashir aonyeshe huyo aliye mpiga ni nani huo muda wote nilikuwa nimesimama tuu huku nikiwaangalia
Bashir nae hakusita kwa kutumia jambia lake akanyoosha kuelekea kwangu kwa maana mimi ndio mhusika wa tukio hili.
Yule teja kwa kimbelembele akajileta huku kashika upanga wake mkononi na kusema kijana piga simu ya kuaga kuwa wewe wakuandalie tuu kaburi kwa maana saiz wewe unaenda kuwa kitoweo changu nakupa dakika moja inatosha. Baada ya hapo akatoka kipisi cha karatasi ambacho ndani yake kuna bangi alikiwasha na kuvuta kisha akampa mwenzake ili nae apige pafu
Kisha akanigeukia tena./ muda umeisha kisha akanyanyua panga lake lakini anashusha tuu panga lilipigwa teke na kwenda kutua juu ya bati za nyumba ile kisha nikampiga makofi kama naadhibu mtoto. Baada ya hapo nilimpa ngumi ambayo ilimrudisha nyuma kidogo nikaongea na teke la tumbo alipepesuka na kwenda kuwasukuma wenzake kule walikosimama. Kudadeki zenu kwahiyo mmejituma kuja kufanya ujinga kama huo hapa eti. Nilikuwa naongea huku nikiwafuata waliko, nao kwakuwa walikuwa na silaha wakajiaminisha na kunyanyua silaha zao. Mmoja akajifanya kuleta shobo za kuwa wa kwanza kunipiga alipewa zawadi ya ngumi ya taya akaanguka chini huku akiwa kashika tu mdomo kwakuwa alikuwa ameshika fimbo niliinyanyua na kuanza kuwachezeshea muda wa dakika tano tuu ulitosha kuwakalisha wote chini. Nilipomaliza nilijaribu kupapasa macho yangu ili nimwone, lakini jitihada zangu hazikufanikiwa, sikumwona na wale mateja waliondoka na kupotelea wapi sijui

-------baba ivi simu yangu niliiweka humu ndani lakini siioni iko wapi maana nimetafuta sana na sijaiona (aliuliza mtoto wa mzee yule ambae waliniteka) e bwana wewe unalia na simu ya laki tano mimi niliibiwa milioni saba unaona kama unahaki ya kulia? Na kibaya simu yenyewe inapatika hebu ngoja nipige tena. Alinyanyua simu na kutafuta ile namba tena ili apige lakini haikuwa inapatikana
Kama ni line nilishasajili nyingine kuepusha usumbufu usiwepo kabisa kisha nikaifuta kila data zikiwemo account zake zote

Kama unavoona namba saizi haipatikani (aliongea baba ake)
Basi itabidi ninunue nyingine kesho, kwanini usiende sasa hivi nikupe hela kabisa, sawa nipe tuu naenda hata saizi. Basi mzee alisimama na kwenda ndani kisha akatoka na kitita cha hela kikiwa kimefunga na lababend (kama mnavosema) kisha kamkabidhi yule mwanae akanunulie simu, alipokea na kuondoka.

Katika duka moja tunamwona yule kijana wa mzee yule ameingia kununua simu mara akakumbana na dada Fulani na kuangusha simu ya yule dada ambapo simu ilianguka na kupasuka kioo lakini huyu dogo hata hakujari akapita na kuingia ndani. Lakini mhudumu kwakuwa aliona akamuuliza // wewe kaka mbona umeharibu simu ya yule dada lakini unajifanya kama huoni vile// ebwana ee wewe fuata kinachokuweka hapa huyo dada ndio kazi yako au unajifanya msamaria mwema wa kileo acha uboya nahitaji nokia lumia 850 hapo kama ipo.
Lakini yule mhudumu akakazania kwa kuendelea kuongea
//kakaangu acha dharau yule nae ni binadamu hujui saizi hapo tayari umemharibia hana mawasiliano tena?
Ivi wewe sista vipi mbona inaonekana hatuelewani kwahiyo simu inagharama gani ambazo wewe zinakupa uchungu namna hii, simu ipo haipo niambie niondoke aliongea kwa hasira sana yule dogo
// ok simu zipo nadhani gharama zake unazijua ni m ngapi
Wewe usijari kama hela ipo ya kutosha tuu nipe simu niiangalie nikiridhika nayo fwesh
./././mhudumu alitoa box moja la simu na kumkabidhi ili aweze kutazama. Dogo alilipokea kuangalia kisha akatoa kitita kizima cha hela zile na kumwambia hesabu zako nipe chenji zangu. Mhudumu. Alizipokea na kuhesabu huku akiwa na lengo la kumkomoa alihesabu zinazotakiwa kisha akahesabu za simu ya yule dada kisha akakamrudishia chench ambayo ilikuwa ni laki tisa na themanini na kumwandikia risiti.
Unaitwa nani mteja
Naitwa enock mlanje. Alijibu hivo kisha yule mhudumu akaandka jina kwenye risiti lakini kwenye kiasi cha hela akaandka in u$ dollah kisha akamkabidhi.
Karibu sana. Enock aliondoka kwa furaha asijue kuwa kaibiwa.,
Enock akiwa njiani kuna gari moja jeusi lilikuja na kusimama mbele yake kisha muda wa dakika tuu kadakwa na kuingizwa ndani ya gari lile ambayo ilienda kumwacha katika viunga vya posta. Enock alishuka ndani ya gari huku akiwa analia sana huku akiwaza gari lake alilokuja lipo mbali na kama simu bado ni mpya hawezi kutumia kufanya chochote ila akawaza aingie kwenye duka moja ili apate msaada-------itaendeleaaaaaa

Jumapili, 16 Oktoba 2016

Jumatatu, 10 Oktoba 2016

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 13

Ilisikila sauti paaa!!! Kisha vika fuatiwa na vilio vya watu

Songa>>>>

Kila mtu pale tulipokuwa tumesimama alitawanyika na isieleweke kaenda wapi, na mimi isionekane zube sana nikaondoka na kuelekea kule ambako imesikika ile sauti nilijivuta hadi kufika kule ambapo niliweza kuona vijana watatu ambao wamejaza vifua kama breast za wanawake (sitaki swali) wakiwa wamesimama wakitoa kichapo ambapo mmoja kati ya wale alikuwa amehika bomba moja ambalo kwa mda huo lilikuwa likitoa moshi, nilijaribu kulitafsiri lile bomba lakini sikupata jibu lolote lile zaidi ya kujua labda atatumia kumpiga mtu ila bado nikabaki na swali kwanini litoe moshi halafu amelishika kwa raha kabisa, hili jambo sikulielewa kabisa nikajikuta nikisogea hadi mbele ili niwezekujionea mwenyewe vizuri kabisa.

NANI MWINGINE ANAE TAKA ALETE UBISHI JUU YETU SISI, KILA SIKU TUNAWAAMBIA HUU MTAA LAZIMA UWE NA HESHIMA JUU YETU SISI THREE SOJAZ SAWA HILI KUNDI LICHUKULIENI KAMA NDIO RAHISI WENU. SASA NAMMALIZIA NA HUYU BOYA ALIYEBAKI.
Baada ya kuongea vile alimdaka dada mmoja ambae muda wote nilimwona amekaa kiwoga woga sana,. Baada ya kumdaka yule dada alikuwa analeta ubishi aliokea kofi moja ambalo kwakutazama tuu lilikuwa ni zito sana hata mwingine ungepigwa lazima uombe maji ya kunywa. Hichi kitendo kilinikwaza sana na nilishindwa kabisa kujizuia nika paza na mimi sauti
;;;;;oya bro huyo dada kakosa nini hadi umpe adhabu kama hiyo hivi huoni kama huo ni unyama unaomtendea huyo,. Baada ya mimi kuongea vile akanijibu
;;kwa hiyo ulikuwa unaamuaje sasa au unataka uje kuwajibika wewe, no mind kama unataka nipo tayari kumwachia huyu Malaya aende halafu ubadiri siunajiweza
;;;;;kudadeki kwahiyo akili yako wewe ni  kunyanyasa wanawake tuu si ndio ok sio shida sasa basi., kama wewe unajiita mwanaume unae taka uheshimike kila mtaa mi nipo tayari kukushushia hiyo heshima fara wewe.
;;hahahaha we mbuzi ivi unanibipu nadhani umeona uwe ray kwa kutafuta kiki ya kubishana na mimi? Si nakuuliza we toto la kahaba
;;;;;;toto la kahaba ndio lenye akili ya kishost kama wewe huku ni boy acha nyodo njoo tuonyeshane sio maneno mengi maan hayajengi vipi

Baada ya mimi kuongea vile alimwachia yule dada kwa kumrusha huko kisha akawa ananifuata akiwa kafura, watu wote katika hili eneo walianza kusogea pembeni ili washuhudia ni nini kitaendelea hapa wale ambao wao kazi yao ni upambe kama kawaida walianza
Bro akujui huyo dadeq zake anaona sisi tunaeheshimu kama ni malofa hivi hebu mwoneshe tuu boya huyo

Nae kwakuona kapewa sifa akawa bichwa hiloooo alitoka spidi na kuja kujirusha ili atulie na teke kwenye kifua changu. Lakini kabla hajafika nilruka kavu kisha tukakutana juu kwa juu na kwakuwa hakuwa na stamina ya kutosha akatulia mgongo chini.
Hapo hata kelele zilianza kupungua kutoka kwa wale wapambe. Lakini bado alionyesha ubishi alinyanyuka na kutaka asogee na ngumi aliporusha mkono niliudaka na kuuzungusha hapo ilisikika tuu sauti ya kaaaa kwenye mwili kisha kikafuata kilio kama mtoto, huku mwanzo alikuwa akiongea bezz zito tena la kujiamin kana kwamba yeye ndie general ya majeshi.
Baada ya pale nikataka kuondoka nikijua tayari nishamkomboa yule ambae hta kitendo ambacho alitaka kufanyiwa sidhani kama ni kizuri
Niliangalia mahali pa kutokea nikawa nimeweza kuona upenye fulan niliufuata lakini kabla sijatoka nilirudishwa pale katikati nateke zito kisha ikasikika sauti HAHAHAHAHAH WE UNATAKA KUUTAWALA MTAA AMBAO UNAWENYEWE KAMA UMEPIGA HUYU MMOJA BASI SISI TUTAANGAMIZA PAMOJA NA FAMILIA YAKO YOTE
Nikiwa bado nipo pale chini nikaona watu wakija pale na mapanga hapahapo gafla nikanyanyuka na kusimama kama mtu ambae ametoka katika usingizi na ameota ndoto ya kutisha sana

Wale wote wenye mapanga wakaanza kunifuata. Wakati huo nikiwa nawaza sina hata silaha, lakini nikakumbuka kuwa kuna njia ya kuwafanyia mauzauza kisha kila kitu kinakuwa fresh. Wakati ule wapo jirani ilikuwa kama CD ya kichawi inatazamwa.,., nilidank juu sana waliokuwa chini waliona kama cheche tuu zinawaangukia, mara mtu nikatua tena chini nikiwa sio mimi tena. Safari hii nilikuw na nguo za kininja zenye rangi ya nyeusi na nyekundu hapo ndio watu wote walibaki tuu wameshika midomo yao kuonyesha hawaamin walichokiona wenye smart phone nao ulikuwa ndio mda wao wa kuanza kushoot video maana wamezoea ninja assasin kwenye tv tuu lakini leo wanaona live kwa macho yao

Baada ya kutua chini pale nilichomoa upanga wangu nikiwa sina lengo la kumwacha hata mmoja kati ya wale wenye mapanga zoezi lililofuata hapo ni kichapo tuu kila aliejitahidi kunivizia na panga lake hakuna alicho ambulia zaidi yakufyekwa au kuvunjwa kiungo mojawapo
Waliokuwa wanaangalia kuna jamaa mmoja ambae ndie aliye nipiga lile teke la kunirudisha pale katikati huyu ndio sikutaka hata time nae aliposogea tuu nilidank na kutua kichwani kwake huku nikimshindilia kiwiko cha mkono ambacho kina ujazo wa aina yake kisha nikaruka na kumbetua kabla haja tua chini nilimwongeza teke ambalo lilimpeleka juu sana anapotua chini nikamtegea kisu nae akatua juu yake (kama mwoga fumba macho)
Waliokuwa pembeni wale washabiki baadhi yao walianza kuondoka taratibu huku wakirudi makwao na baadhi wakificha sura zao
Nilipomaliza zoezi lile kulikuwa na ukuta jirani hapohapo. Upanga wangu ukiwa mkononi niliutumia kuandika YOU HAV E TO KNOW (WHO AM I) kisha nikapotelea katika maeneo ambayo hata ungekuwa makini kiasi gan ungeondoka chenga huelewi chochote.
Dakika chache mbele nikaja kuonekana tena katika kijiwe fulani cha kushona viatu

Daaah ivi kumbe hata Tz kuna maninja
Daah mwanangu ivi yale yalikuwa mauzauza au ni kitu gan maan ilikuwa kama muvi.
Halaf nakumbuk kama umerekodi hiv lile tukio
Aaaah kweli halaf ckucheki ngoja nicheki saa hizi hapa

Alitoa simu katika mfuko wake wa suruali ilikuwa ni tecno h6 nadhani aliyotumia kushoot video ile
Basi watu wapale walijisogeza kuiangalia huku na mimi nikiwa ni mojawapo kati ya waliokuja kuitazama. Aliiwasha hii video ikaonyesha tuu pale ambapo walikuwa wanaongea kisha nikaruka juu sana kwa kudanki kuendelea ilikuwa ina scratch tuu
>>>>aaaaaah mwanangu hapo umeharibu uhondo wote duhh
Sasa kama memory yako inavirus siungeacha tuu kutuonesha shit smart phon nzima memory inavirus unazingua bhana
.,.,watu walichukia  sana kile kitendo cha simu kustak kuonyesha ile video huku wao walikuwa na hamu nayo ile mbaya

Lakini mimi huo mda wote nikawa najiuliza inamaana hawanijui au sura sio yangu huku na kule ni tofauti. Maana hapa ningepata maswali kibao kuhusu uwezo huu lakini sikujua kuna nini hadi wanisahau wakati tulikuwa wote muda si mrefu kabla ya tukio. Nikiwa bado simu yangu ilianza kuita kuitazama ni nani-----itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 12

Baada ya hapo walitoa silaha na kuanza kuifuata ile gari____

Songa nayo
------wale wanajeshi waliasogelea hadi jirani ya lile gari kubwa ambalo lilikuwa na walinzi ndani. Lakini walishangaa kuona kimya kimetanda sana katika gari hili ila kwakuwa ni wanajeshi wakajipa moyo na kuingia katika gari lile ndani wakiwa na imani lazima watamuona mtu ambae anawaletea mauzauza hapa

Oya kinju mbona hakuna kitu humu ndani, ngoja niwashe hata tochi ili nione./ baada ya hapo aliwasha tochi yake ambayo ilikuwa na mwanhamkali sana lakin hakuweza kumwona mtu mle ndani zaidi aliona tayari mlango wa upande mwingine nao upo wazi.
Kwa kuona hivo akajua walinzi wanawaogopa, alipaza sauti
JITOKEZENI TUMEKUJA NA BOSS WENU KUWENI NA AMAN HATUPO KUWADHURU NYIE. HEBU NJOONI TU. Alipoongea vile ndipo akaanza kujitokeza mlinzi mmoja hadi mwingine hadi wakafika idadi kamili inayotakiwa ambapo bamboo kwa mda huo hatazamiki hata kidogo usoni kaumia hadi huruma kama ungemuona huwezi kumwangalia mara mbili

Walijaza mafuta katika lile gari na kutaka kuanza safari ya kurudi nyumbani lakini kila walipojaribu kupiga starter hakuna kulichojibu.
Mwanajeshi mmoja alishuka chini na kuangalia huku akiwa na tochi yake lakini hakuona tatizo lolote. Wakabadilisha mawazo labda wote wapande gari la boss wao ambalo amekujanalo,. Walikubaliana na hilo wazo kisha wote wakaondoka na kulifuata lile gari kisha wakapanda na mwanajeshi mmoja akakaa siti dereva kuonesha kwamba yeye ndie wa kuendesha aliweka funguo na kunyonga hakuna hata mwanga uliotoka ilionyesha dhahiri kwamba hili gari halina betri kwa mda huu. Ila kwa kujiaminisha alishuka na kuangalia, na kweli beri kwenye gari tayari ilikuwa imesha chomolewa
Mwanajeshi huyu alifura kiasi kwamba akasema huyo anaemchezea akili laiti akionekana hana kichwa

)()( kudadeki nitapeleka mtu kuzimu mimi, tafadhali wewe kilaza hebu jitokeze mwenyewe kabla sijaanza kukusaka)()( aliongea mwanajeshi yule kama mwenda wazimu lakini hakuna aliyemjibu hata kwa hewa tuu
Masaa yalisonga mbele bila kukawia, toka saa tatu mda walio kuja huku hadi sasa tunaangalia saa ni saa saba na robo na hakuna magari yanayoweza yakapita haya maeneo mda kama huu, mwanajehi baada ya kuchanganya akili akaona huu upuzi hakuna wa kulala hapa porin.
Alinyanyua simu yake na kuandika namba fulani kisha akazipiga
-_-_-__-yaa ndio mkuu, tupo eneo la mawenzi sijui huu mtaa wanaita, yaa ndio njoo, au tuma watu, ndio, ok sawa simu ikakatwa

Baada ya dakika chache kuna magar yapatayo manne yalitinga katika hili eneo, kisha wanajeshi wakashuka wasio na idadi na kuanza kuingia katika pori hili huku wakikata baadhi ya miti ambapo wakati huo wote nilikuwa nikiwaangalia tuu, na baada ya muda mfupi tuu walimaliza maeneo yote yakawa wazi. Nikaona isiwe shida kama nilipambana na yule kiumbe nikamshinda nitashindwaje na hutu tuumtu twa kawaida.
Baadaya hapo nilichumpa toka pale niliposimama na kutokezea katika kaeneo ambako kalikuwa wazi ambapo ni barabarani.
Wanajeshi wote walishituka na kugeuka. Ile wanaangalia nyuma yao waliona ninja akiwa na maski fulani ya rangi kama silver ilingaa kutokana na kuwa walikuwa na tochi za mwanga mkali usiku ule.

Kwa kuwa walikuwa wengi sana walijivuta kwa mshikamano hadi pale ambapo mimi nipo huku wakiwa na iman ni lazima wanikalishe tuu.
(hebu kaa hapo hapo upo chini ya ulinzi) ilisikika sauti ya mwanajeshi mmoja ikiniamrisha ninyooshe mikono juu eti nimesalenda kwao.., kimoyomoyo nikasema sio masharti ya ninja hayo kunyoosha mikono juu. Kisha nikawageukia kuwatazama.

Silaha zao zoote zilikuwa zikiniangalia mimi kuashiria kwamba siwezikufanya kitu chochote kile ili kujinusuru, lakini nikaiona njia moja ya tuu ambayo ilikuwa ni kuwapiga changa.

Baadaya kugeuka nilichuchumaa chini
Wanajeshi wakiwa wananitazama pale nilipochuchumaa ulitokea mwanga mkali na mlio kama wa bomu,. Kufumba na kufumbua mwanaume nlishapotea mda mrefu sana. Ule usiku walitafuta lile eneo lote lakini hawakuona mtu yeyote yule. Baada ya hapo waliamua kuondoka wote katika lile eneo na kurudi makwao.
Safari ilikita moja kwa moja hadi nyumban kwa boss na kuwaacha pale pamoja na walinzi wake. Walimchukua boss kwa kusaidiana kisha wakamweka sebuleni. Huku wakimwamsha kwa fujo na kwa bahati nzuri walifanikiwa kumwamsha hadi aliamka, kisha walimfanyia utaratibu wote na baada ya dakika chache wote waliingia kulala hadi asubuhi

_____________________________
Ilipofika asubuhi boss aliamka na kuwasha tv apate angalau taarifa ya habari
Habari ya kwanza kusikika
)))))asubuhi hii katika mtaa wa mawnzi kuna magari mawili yameonekana yakiwa yamewakamoto, tukio hili inaonekana limefanywa usiku wa kuamkia leo na mhusika bado hajajulikana mpaka sasa, jeshi la polisi bado linaendelea na uchunguzi zaidi juu ya tukio hilo(((((
Boss baadaya kusikia habari ile palepale alizimia. Mhudumu mmoja ambae alikuwa anapita kwa aajili ya maandaliz ya chai ndio aliyekuwa wa kwanza kuona lile tukio, aliwaita walinzi ili ikiwezekana wamfikishe hospital akapewe huduma.
Walinzi walipofika pale waliita gari na kumpeleka kituo cha afya na sio katika hospital kubwa kitedo ambacho kilimshangaza yule mhudumu, alipata shauku ya kuataka kuuliza lakini aliushinda mdomo wake-----

Asubuhi tunaamka katika nyumba ambayo na bon amepanga,.
Kuna wadada wawili walikuwa wamekaa wakiotea jua wakiwa wamekaa kizembe kabisa.
======ivi shoga mbona huyu kaka haamki hadi sasa hivi
==nyooo ko wewe umejikalisha kimitego hivo ili umpate,.
===sasa hayo yametoka wapi sasa ndio jibu la swali langu au
=yametoka wapi mdomoni au we unatolea mata***ni, hebu nitokee hapa fyuuu
== powa natoka ila hadi nimwone
=Dadeki na hatoki huyo hujui anamwogopa bashir tena na wewe enheeee sijui>>
Katika hii nyumba hawa wadada wawili sijui ni wanalaana au vipi maana wao ni maneno tuu mda wote lazima watupiane

*******tukiwa mbali kidogo na huu mtaa tunamwona bon akiwa na vijana kama wanne hivi ambao walikuwa ni boda boda na mmoja yupo tuu sijui anafanya kazi gani.
.oya broo mishe gan unapiga kitaa hiki
Daa bado sijapata mishe maana bado ni mgeni
. daah pole ila sio shida_____kabla hajamaliza kuongea ilisikika sauti paaaa!!!
Kisha vikafuatiwa na vilio vya watu baada ya -----itaendeleaaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 11

---------ilikuwa ikionyesha dhahiri kwamba kuna polisi tayari washaingia pale ndani na taarifa wamepata wapi hakuna aliyeweza kujua baadhi ya watu ambao walikuwa bado hawaja ingia ndani walishikwa na kuwekwa ndani ya gari ambalo linafahamika kama tenga. Kisha afande mmoja akasogeza gari jirani kabisa na uwanja, na kuanza kufungua milango ya kila mmoja.
Usiku huu ilikuwa ni fujo tuu katika hii nyumba
Baada ya dakika kumi na tano walikuwa tayari wameshakusanya wapangaji wote na kuwapakia kwenye tenga

Aisee hapa kuna chumba kimoja naona kama bado hatuja pita(aliongea afande mmoja kumwambia hivo mwenzie)
Ok nichumba kipi hicho kipara
Chumba cha mwisho kwenye karibia na kona. Ahaa we nyoronyoro nenda kagonge fasta (alimwamulisha afande mwenzie)
Yule afande ambae alionekana ni mwembamba sana hadi wanamwita nyoronyoro aliondoka ili akaangalie katika kile chumba na amchukue na aliyeko ndani waende kituoni

Ngo ngo ngo fungua mlango (kimya) nasema fungua mlango,.,. aliongea kwa ukali lakini hakuna sauti ambayo iliitikia wala mlango haukufunguliwa alichokifanya kuulazimisha kufungua akafanikiwa. Lakini ile anaingia tuu ndani alibamizwa na mlango hadi akajikuta anarudi tena nje. Hadi hapo hakuwa na hamu tena ya kuendelea kufuatilia hili swala la kutaka kujua aliyeko humu ndani, aliondoka na kurudi hadi kule kwa wenzake.

Oya kimbao mbona unarudi  bila abiria inakuwaje au umeshakula hongo hukohuko.
-nianchie upuuzi hebu nenda kwanza wewe ivi unadhani wewe ulisahau kwa bahati mbaya kwenda katika kile chumba.
Unamanisha nini?
- nimesema nenda kamchukue aliyeko ndani. Baadaya kubishana sana yule ambae alikuwa kama ndio kiongozi alitoa uamuzi wa kwamba tuachane nae tuu.
Lakini wapangaji wengine nao wakapaza sauti zao

NYIE MAAFANDE NDIO HAMNA AKILI KWELI YAANI MHUSIKA MUMWACHE HALAFU TUCHUKULIWE SISI WENGINE AMBAO HATA HATUHUSIKI SASA HAPA HATOKI MTU, MTAKALO AMUA AMUENI TUU WOTE TUNASHUKA HU UJINGA SASA>
Baada ya kuongea vile alianza kushuka mmoja baada ya mwingine hadi gari likawa tupu. Maafande walijaribu kutumia ubabe lakini hakuna aliyyeweza kuwaridisha mle ndani. Walipoona wameshindwa waliamua kuondoka na bashir pekeyake na kwenda nae kituoni ili akawasaidie maelezo kwa kitu kilicho tokea.
Gari lilianza safari na kituo cha kwanza kilikuwa katika kituo cha afya ambacho hadi ule mda kilikuwa bado kipo wazi, na kumpa huduma ya kwanza bashir ili waendelee na safari yao. Baadaya kufika kituoni bashir alifikishwa na kupelekwa mahali maalumu kwaajili ya maelezo. Lakini alipofika tuu polisi mmoja ambae alikuwa ni wa kike akajisemea asante mungu KAMA HILI JAMBAZI LEO LIMELETWA
Hongereni kwa kazi nzuri maafande maana huyu alikuwa ni msumbufu sana. Kisha akapelekwa katika chumba kingine bila kuulizwa chochote

_______upande wa walinzi kule barabarani_______

Oya nyie jamaa hapa naona boss leo ni kama hana msaada hivi, mnashauri tufanyaje sasa tutembee kwa mguu au jee.
Kudadeki acha ujinga hata kama ramani tunayo umajua huu mtaani wa akina nani wewe kama utatembea kwa mguu safar njema bamboo sawa sisi hatuna noma hata kwenye gari tutalala tu
Duuuh ila nae anazingua sa siapokee simu tu tuelewe tunafanyaje-----wakiwa wanaendelea kujadiliana mara simu ya bamboo ilianza kuita, alipoitazama alifurahi baada ya kuona namba ya boss ndio iliyokuwa ikipiga simu kwa muda ule, aliipokea
_-_-_yaah boss, ee  ndio, enhee, sawa ok, lakini mbona hakuna m-pesa hili eneo, ya ni bora uje nayo tu, ok asante, sawa tutakungoja tuu, asante. Kisha simu ilikatwa.
Bamboo alifurahi, na wenzake kidogo furaha yao ilirudi maana walikuwa wakiwaza watalaleje hapa polini na isitoshe sio wenyeji. Lakini waliposikia boss anakuja ili waondoke walishukuru sana kisha wakaingia kwenye gari na kuanza kumngoja ili atokee wajaze mafuta kwenye gari safari ya kurudi nyumbani ianze.
Walikaa kwa mda kama wa nusu saa wakaona boss hatokei bamboo akataka anyanyue simu ili ampigie tena boss. Lakini gafla akaona simu yake imepokonywa sikioni mwake, kwaakili yake alijua labda ni utani waliojizoesha na wenzake ndio wamechukua simu. Alimgeukia mwenzake ili amwambie aache utani wa kijinga lakini akajikuta akipokea makofi tuu
Bamboo alianza kuona maruweruwe. Wakiwa bado hawaelewi chochote mara wakaona kama mbele yao kuna taa zinawaka na kuzima huku zikiwa fuata wote wakajificha chini ya viti vya gari lile ili ule mwanga usiwamulike. Lakini mauzauza hayakupungua mara wakahisi kama wanamwagiwa maji kwenye migongo yao tena maji ya barid kama barafu kitendo kilichomfanya kila mmoja wao kunyanyuka ili ajipukute hayo maji. Kitendo cha kunyanyuka tuu kioo cha mbele cha gari lile kilipasuliwa.
Wote wakabaki wameduwaa tuu mara wakaona mtu ananyukia mbele ya gari lile
Bamboo alishika usukani ili aanze kuendesha amharibu huyo aliyekuwa ananyanyukia mbele ya kioo. Lakini gari haikuwaka. =.alisahau kama mafuta yalikuwa yameisha na ndio walikuwa wanamngoja boss awaletee mafuta
/////kweli bahati mbaya haina mwenyewe na kifo cha nyani miti yote huteleza/////

Bamboo baada ya kuona vile akaamua kujitosa na kuchumpa pale dirishani kwenye kioo cha mbele ya gari ambacho kilipasuliwa, lakini kabla ya kutoka nje alirudishwa na teke ambalo lilimpeleka hadi siti ya nyuma kabisa huku akitulia mgongo. Bamboo alilalamika sana kuilaani hii kazi ambayo alipewa na boss wake leo..,,,/; kwa mbaali wakaweza kuona mwanga wa gari inakuja katika lile eneo

______)kwenye hili gari tunaona boss wa akina bamboo akiwa na wanajeshi wawili ambao wameshiba sana(_______

Aisee mkubwa gari lako ndio lile au
Yaah ni lenyewe vipi kwani
Mbona naona kioo cha mbele kama kimevunjwa vile (alikuwa ni mwanajeshi mmoja ambae alikuwa katika lile gari na boss wa bamboo)

Ngoja tusogee jirani kwanza
_-_-gari lilifika hadi pale kwenye gari ambalo lipo na walinzi. Wanajeshi wale walikuwa wa kwanza kushuka ambapo mmoja alizunguka ili amfungulie mlango boss, mlango ulifunguliwa na boss akawa anashuka kwa maringo sana ili akajue nini kinaendelea kwa walinzi wake. Lakini alipotoa kichwa tuu na kushusha mguu mmoja hapohapo alianguka chini wanajeshi hawa walipata wakati mgumu sana maana hawajui ni presha ya boss au kitu gani, walimnyanyua ili wajue cha kufanya.
Baada ya kumnyanyua mwanajeshi mmoja aliingia nae tena katika gari huku mwanajeshi mwenzake akifungua buti na kutoa madumu mawili ya mafuta ili akajaze katika lile gari lililochukua walinzi ili waondoke kukamilishakile ambacho kimewaleta
Huyu polisi ambae alikuwa na boss baada ya kumwangalia vizuri aligundua kuwa boss amedwingwa sindano ya usingizi. Alimwita mwenzie, akaja
Aisee hapa inaonekana pana hatari hebu tumwache boss tuacheki hicho kinyago kinacho tuchezea(baada ya hapo walitoa silaha zao na kuanza kufuata gari------itaendeleaaaaa

Who am i

WHO AM I (mimi ni nani)
Benchrys
No. 10

-----yule aliingia ndan na kuwasha tochi katika simu yake ili aangalie hela mahali ambapo anaziweka kila siku, lakini alishangaa kuona hakuna kitu chochote zaidi zimebaki tuu zile nguo ambazo zilikuwa jirani na ile sehemu ya kuhifadhia hela zake.
Hadi hapo mzee alichanganyikiwa kabisa asiamini kama kweli hela zake hazipo pia akabaki anajiuliza ni nani aliyefanikiwa kuingia hadi ndani ya kile chumba chake na kuondoka na pesa zake.
Licha ya kujiuliza maswali hayo yote lakini hakupata jibu ila akajipa moyo wa kuendelea tuu kutafuta pengine ataziona, ukiangalia umeme haupo katika hii nyumba ndio kitu kilicho mfanya ajipe moyo upya wa kuendelea kutafuta pengine ameangalia kwa pupa hadi hajaona kitu chochote.
Alitafuta hela zile kwa mda wa nusu saa lakini hakuziona, baadaya hapo akatoka na kukaa sebuleni huku kukiwa ni giza ila simu yake ndio iliyokuwa inamwongoza huu mda wote.

Upande wa walinzi nao walingoja sana hadi baadae wakakata tamaa kabisa, bamboo kama kawaida akanyanyua simu yake na kutafuta namba ya boss na kupiga,
Mzee akiwa nyumban amekaa pale kwenye sofa lake mara akasikia simu ayke inaita tena akanyanyua tena ili aone ni nani anae mpigia, alipoona ni mlinzi wake bamboo hata hakuhangaika kuipokea ile simu mana alishajua hawa shida ni mafuta na sio kitu kingine.
;;;kwakweli usiku huu ulikuwa ni mbaya sana ambao hata wasingeweza kuusahau hata mara ,moja

;;;IVI HAWA NAO WAPUUZI INAMAANA HAKUNA HATA GARI MOJA LINALOPITA KATIKA HIO NJIA MBONA WANATAKA WANIFANYE KUCHANGANYIKIWA HAPA SHIT;;;;
aliongea boss alipokuwa amekaa pale sebuleni baada ya simu kutoka kwa mlinzi wake bamboo kukatika
mzee akiwa amekaa tena simu yake ikaita tena
ya ndio nimekutafuta sijui ulikuwa wapi kijana wangu,
aah sawa mimi hapa nina tatizo kama hutojali sijui kama unaweza kuja hata sasa hivi hapa nyumbani, ok nitshukuru sana kijana wangu nakutegemea usiniangushe kwakweli, aaaaah ok, ok, nashukuru sana(simu ikakatwa)
baadaya muda kuna alipiga hodi mzee alikaribisha ili aingie ndani
    daaaah mzee hapa naona shida yenyewe hata huna haja ya kuniambia inajieleza yenyewe aisee pole sana, ngoja nikutatulie haraka. Kijana aliingia kwa maneno mengi sana ambayo mzee hata hakupata chansi ya kuongea. Akabaki ametulia tuu kumngoja tuu kijana huyu akamilishe hii kazi ndipo waongee zaidi.- baadaya dakika chache umeme uliwaka ambapo mzee alifurahi sana akamfuata huyu kijana na kumwambia----; yaaah hebu njoo ukae kwanza mana hapa sikujua kabisa ntafanyaje hapa

sawa mzee wangu hizi kazi za tuu kwetu kama hela ipo
aaaah we usijari pesa sio tatizo sana, ehee niambie unahitaji sh ngapi mana umenisaidia sana
-----mzee alifurahi huku akihitaji aambiwe kiasi cha pesa ya kulipa kwa kurekebishiwa umeme wake katika nyumba kijana nae kwaajili ndio kazi yake hakuzubaa akamwambia
++mzee hapa kwakuwa umeniita usikukama huu utanipa elfu hamsini tuulikitokea tatizo niite tena.
Mzee akamwambia hebu ningoje hapohapo kwanza nakuja. Kisha akasimama na kuelekea ndani ili akafuate pesa amlipe huyu kijana
Baadaya kufika ndani ndipo alijua kuwa simu yake haikumdanganya kuwa ndani kwenye briefcase yake hakuna pesa yoyote
Kidogo azimie lakini watu wakubwa tena mapedeshee kama hawa hawawi na akiba ndogo akaenda kufungua begi fulan hivi kubwa kiasi
Ile anafungua tuu lilichanika begi lote huku vitita vya pesa vikidondoka chini akahesabia kiasi kama cha laki mbili na kuondoka nacho
Alirudi tena sebuleni na kumkabidhi yule kijana zile pesa na kumwambia asante mara kadhaa

Tukirudi kwa ben na bashir hii nyumba huu usiku zilikuwa ni kelele tuu
Wakati huo bashir alikuwa anatoa damu puani hadi mdomoni huku akiwa hana hata nguvu za kusimama tena

Kama kawaida wadada na maneno yao
Hahahaaaaaaaaaaaaaa babu uuu leo yamekupata unajifanyaga kidume sana kwa wenzio leo kajamaa kadogo kadogo kama hako kamekukalisha boya wewe
;;;;;mh amina tulia bhana kelele hadi unaboa ujue hapa atakuwa anakariri wanaomletea shobo shauri zako
Ohoooooo tena achunge akitaka kunipiga tuu nipo tayari nikaolelwe na huyu mgeni hata kama sijamfahamu. Wenzie baadaya kusikia hivyo walicheka sana huku wakimwambia shauri zako

Bashir baada ya kumwonesha na kumfunza adabu, nilijua wazi kwamba yule mwanamke wake labda atamsaidia kumwondoa pale lakini mke wake mwenyewe ndio kwanza alikuwa anapiga tuu stori na wenzake
;;;;; enheee shoga imekuwaje hadi shemeji yetu inakuwa hivi tena, aliuliza hili swali dada mmoja ambae walimtaja ni qeen.
Aaah shoga wewe acha tuu huyu mgeni si akaja kugonga na kuuliza wapi ambapo anaweza kupa msosi usikuu huu ili ale akalale bashir kama kawa na nyodo zake akajibu pumba lakini mimi nikaona sio vyema nikamwelekeza mahali ambapo anaweza kwenda na kula, huyu mkaka aliondoka, huku nyuma sasa bashir amenimaindi vibaya na kujisemea akirudi huyo boya wako nawachinja wote. Mimi sikuwa na la kusema
Basi huyu mkaka aliporudi akawa amekuja kutoa shukran bashir siakajifanya kumpandishia mimi nimewasilikiza wamebishana hadi wakasema watoke nje ili waoneshane, mambo ndiokama unavoona saizi hivi mtu tayari chini_-_--___-
Huu ni uboya ivi we unadhani mimi nikamtoe pale huku mimi mwenyewe kila siku napata shida tuu za kupokea kichapo bila sababu yoyote leo na yeye aonje bhana
(aliongea maneno yale mke wa bashir ambapo alikuwa amekaa na wenzake katika gogo ambalo lipo kwenye moja ya ukuta wa nyumba ile na baadaya mda wapangaji karibia wote waliondoka na kurudi ndani kwao huku mdada anaeenda kwa jina la Asha akisema kesho lazima awe redio ya mtaa kutangaza kuwa bashir jana usiku alipigwa kama mtoto na mgeni ambae ameingia jana hiyohiyo kwenye nyumba hii) lakini wenzake wakasema shauri yako na mwenzio amina nyie inaonekana mnataka kumbip bashir atamalizia hasira zake kwenu jifanyeni hamjamfahamu tu. Moja wao aliongea maneno yale na kuingia ndani kwake na mimi baada ya kuona kama adabu tayari nimeshamfunza nilinyanyuka na kuingia chumbani kwangu ili nilale na kesho nianze kazi ya kulipa visasi kwa wale ambao wanahusika na kututeketezea familia zetu bila sababu yoyote ile.

Niliingia ndani kwangu na sikutaka hata mmoja ajue nimeondokaje hadi kuingia ndan

Hii sikunililala  kwa tahadhali sana, maana najua kabisa hii nchi yetu ya Tanzania wambea hawapungui.. unaweza sema kitu kitabaki siri kumbe kuna watu washapiga simu hadi kituo cha polisi ili kukuchomesha wewe ambae sio mwenza

Nilipoingia ndani nikachukua ile karatasi ambayo nilikabidhiwa na mama ili niipitie nijue ni nini ambacho kipo ndani yake
Nilisoma kwa mda wa dakika kama tano, mara nikasikia sauti kutoka nje wote mpo chini ya ulinzi hakuna mtu kutoka nje------itaendeleaaaaaaaa

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 09

---------sasa siungejenga nyumba yako mwenyewe (huku msonyo ukisikika)
Kiufupi haya maneno maneno yalimuingia sana huyu jamaa. Akajisemea ivi leo hii mimi basher ndo naambiwa upumbavu huu na mwanamke hizi dharau au kitu gani.
    Baada aya kuongea hayo akamgeukia tena ile kwa spidi kama amechomwa na sindano au mwiba. Hali hii ilionyesha kabisa kwamba anahasira sana kwa jinsi alivokuwa. Ndipo ikasikika sauti samahani bashir nisamehe
Pumbavu ivi unapata wapi ujasiri kama huo eti mimwanaume mingine, kwahiyo huyo mgeni wewe atakusaidia nini wewe. Sasa namngoja arudi ili niwaonyeshe wote kuwa bashir ni mwanaume wa shoka.
Na kweli baada ya kuongea vile akakaa kwenye kochi fulani ambalo lilikuwapo mule ndani akimaanisha kwamba ananingoja mimi ili nirudi chumbani kwangu yeye anifuate

______kwa bon_____
-- baada ya kufuata yale maelekezo ambayo nilipewa na mke wa huyu jirani yangu nilienda mojamoja kwa moja hadi lile eneo na kuagiza kitu ambacho nilikuwa nakihitaji kwa wakati ule.
Nikiwa nimetulia nangoja mama ntilie aje aniletee chakula mara nikasikia kelele nje, watu wengi wa mle ndani walitoka ili wakashangae lakini mimi hata sikuwa na habari maana nilienda kwa shida ya kula na kula na sio mambo mengine. Ile nimekaa nangoja, niliona mda unazidi kuenda tuu lakini siletewi chakula changu nikasimama ili niangalie mahali ambapo yupo lakini sikuona chochote. Lakini baada ya dakika chache nikmwona nae akiingia toka nje. Kwa maana nae alienda kuangalia tukio lililo kuwepo kule nje. Niliboreka lakini basi hakuna namna yoyote ile maana mimi ndio mwenye shida. Ilinipasa kungoja tuu

Baada ya dakika chache ndio chakula kiletwa. Nilikula kwa fujo sana mda wa dakika moja nikawa tayar nimeshamaliza nikalipa hela na kuondoka nikienda nyumbani.
Nilifika nyumbani lakini kabla ya kwenda ndani nikapitia kuwashukuru kwa malekezo
Ngo, ngo, ngo
Yaa nani unagonga, aliuliza hivo bashir
- aaah ni mimi jirani yako hapa
Ok powa ingia tuu
- asante. Kisha nikaingia hadi ndani.

Nimekuja sina mengi ila nawashukuru tuu kwa msaada wenu nimefanikiwa kupaona asante. Kwaheli mimi naenda kwangu

Oya dogo ngoja kwani (alisema hivo bashir na mimi nikasimama tena kwa heshima zote)
IVI UNAJUA MASHARTI YA UNAPOENDA KUPANGA NYUMBA HIZI UNATAKIWA KUWAJE (aliuliza hili swali bashir lakini sikujua namaanisha nini)
Bro swali lako linamaana gan mbona kama sikusomi
--ahaa hunisomi utanisoma tuu subiri baadaya muda
Kudadeki usjitie kidume kwa wageni huku hujui mimi ni nani hata siku moja bado sijamaliza tena naomba tuelewane hapa sijaja kwaajili yako na kama ni hela ya pango hujanilipia kwahiyo fanya yako na mimi nifanye yangu sawa bro heshima ni kitu cha sana naona unaelekea hatutakuwa sawa hata kidogo(nilimwambia hivo nae akanijibu)
Powa ila mazingira ya watu hata sikumoja usijitie unajua sana, tena kama mimi ukinizingua nakumwaga ubongo kabisa bila hata kukuangalia usoni unasura ya kupastor au ki gangster sawa mdogo wetu
(niliona huyu anataka kunipanda kichwani tena hata heshima hana)
Sawa sio shida sana tuache maneno mengi kama madem wakitaa chenu twende njee saizi ili tukajue ni nani zaid na ni nani boga lililooza kabisa.

Bashir kichwani akajisemea leo ndio pa kuchukua ujiko kwa haka kaboya kengine ivi hakanijui nini ngoja kwani.
Alipojisemea hivo alimama na kunifuata hadi pale nilipokuwa na kusema sawa hebu twende. We jogoo la shamba huwezi kunitishia maisha yangu kama hukuchunguza kabla ya kuja kupanga hapa ndio utafahamu vyema huyubashir ni nani

Wakati huo wote yule mwanamke wake alikuwa akitusikiliza na kutuangalia bila kuongea kitu chochote kile

Mimi na bashir tulisimama na kutoka hadi nje ambapo kulikuw ana uwanja katikati ya ile nyumba.
Bashir alikuwa na maneno mengi sana hadi na baadhi ya wapangaji wengine walitoka ili wajue kuna nini hadi bashir anapigamakelele ya namna hii.
Kwa macho yangu nikawa nashuhudia milango ikifunguliwa na baadhi ambao walizima taa zao wakawa wanaziwasha ili waweze kushuhudia ni nini ambacho kinaendelea usiku huu

/////shoga angu leo kama siokuna timbwili hapa ngoja tulicheki atakae bondwa kama kawa kesho ntakuwa gazeti kitaa kizima yani.
Sema wee shoga nakuaminia kama ni ukiwembe tuu unajua
Acha zako mbona hata wewe uko hivo unakumbuka ile ulipozusha kuwa umenifumania.
Aaaah kausha bhana usije ukanikosesha mtanange huu bure////// ni wasichana wawili ambao majina yao hayajafahamika bado
Baada ya wapangaji kutoka pale bashir akaona huu ndio wakati wake wa kuonyesha uanaume wake maana wapangaji wote walikuwa wakimfahamu_______

______kwa baba______

Baba akiwa ametulia nyumbani amesha maliza taratibu zote mara simu yake ikawa inaita
Ngrrrrrrr x5
Naam haloo
Ndio mkubwa vipi ile mipango imekaa vizuri
Mipango gani
Mzee usifanye umesahau
Aisee hebu nikumbushe kwani wewe ni nani (simu ilikatwa na maongezi yaliishia hapo)
Baba hadi hapo hakuwa ameelewa ni nani aliyepiga simu kwa wkati ule na kuongea habari za mipango imekaa vizuri alizima tv na kuingia kulala

__________________________________
Tukirudi kwa yule mzee kwenye lile jumba tunamwona mzee ambae ni boss ndo anafahamika hivo
Yupo uwanjani anazunguka tuu peke yake huku nyumba ikiwa haina umeme na mafundi wote wapo bize kwa wakati ule.
Akiwa anaendelea kuzunguka mle ndani kama yeye ndie mlinzi mara simu yake ilianza kuita alipoangalia ilikuwa ni namba ya mlinzi wake mmoja bamboo jina lilisomeka hivo kwenye simu,. Ila mzee hakupokea maana aliona watakuwa wanampotezea tuu mda asijue wanataka kumwambia kitu gani,
Simu iliita hadi ina kata bila kuweza kupokelewa, lakini bamboo hakukata tamaa alipiga tena simu safari hii iliita hadi inakaribia kukata ndio ikapokelewa.
    Samahani boss gari mafuta yametuishia na hatukutembea na akiba yoyote sijui kama unaweza agiza mtu aje atuletee huku tuko hapa barabarani.;;.;.; bamboo aliongea bila nukta maana alijua lazima huyu boss atakata tuu simu ile na kutofanya chochote kile.
Boss alijibu hebu ngoja kama dakika tano hivi natoa majibu, kisha simu ilikatwa nae akaingia tena ndani ili------itaendeleaaaaaaaaI

Jumatano, 5 Oktoba 2016

Who am i

WHO AM I(mimi ni nani)
Benchrys
No. 08

-------baada ya kuita walinzi kwa mda mrefu kashangaa hata mmoja haji kuitika ule wito ndipo akachukua uamuzi wa kusimama ili akawaone mweyewe kule nje. Alishituka baada ya kutoka kule nje aliwakuta walinzi wote wakiwa wamewasha wimbo kwenye simu na kuanza kucheza
Yule boss wao baada ya kuwaangalia akajisemea ivi mkiwaachisha kazi itaonekana mnaroho mbaya sana kama mabos sijui niwamwage ubongo nao????
Lakini baadaya kufikiria sana akasema hapa sio bure lazima kuna kitu nyuma ya pazia himaya yangu imesha ingiliwa tayari.
Alisogea hadi pale walipo na kumshika mlinzi mmoja na kumwambia nenda kauzime mziki huo ili tuongee yule mlinz kwa kuwa ni boss aliongea aliamua kufanya hivyo
Aaaaaa bamboo mambo gani sasa hayo hebu washa mziki
Bamboo aligeuka na kuwaambia angalieni au hamumuoni boss baada ya bamboo kuongea yale walinzi wote walishtuka na kusimama kisawasawa ili wamsikilize boss wao maana walijua kabisa hapa tayari tumesha haribu
;;;;;jaman ivi ni mambo gani mnayoyafanya saizi hapa, mmekuja hapa kufanya kazi au kucheza hizo nyimbo zenu za kibongo mnazoita bongo freva sijui(baada ya boss kuongea yale alivuta pumzi akatulia kisha kaendelea) ok sio mbaya naomba kujua kwa hivi mnavofanya mwishoni mnanidai ujira wenu au na mimi niwachezee hivohivo. Mlinzi mmoja aliropoka kwakusema
Boss mziki ulikuwa mzuri sana
Wenzie walimgeukia na kumwangalia sana yule aliyekuwa jirani nae alimuwasha bonge la kofi ikifuatiwa na ngumi ya tumbo hadi yule aliyeropoka akakaa chini kwa maumivu(((maana kati ya ngumi ambazo ukishitukizwa unaweza kuzirai ni pamoja na ngumi ya tumbo)))
Boss aliendelea kuongea
Cheki kama huyu mwenzenu yaani ameahau kabisa nini kimemleta hapa ili aje kukifanya eti mziki ulikuwa mtamu. Ok nimewaita tokea mda mrefu sana lakini hakuna aliyeweza kusikia wakati huo nawaita sasa sijaelewa ni kwa sababu ya huo mziki au ni kitu gani sijui lakini nili taka mje sebuleni mkawatoe wenzenu na kuwapeleka mahali ambako mimi nitawaonyesha..
Baada ya kuongea yale alianza kuondoka akiwa na maana inatakiwa wamfuate ambako yeye anaenda ambako ni kule sebuleni

Baada ya kufika sebuleni kila mlinzi alibaki ametumbua tuu macho yake kuwaangalia wale ambao kwa mda ule walikuwa wamelala chini huku wakiwa na damu kwenye vichwa vyao maana walipigwa risasi za kichwa kilamtu. Walinzi hawa hata kama wamelinda kwa mda mrefu sana lakini hakuna hata mmoja ambae amewahi kupoteza uhai wa kwa namna yoyote ile kwa hiyo wote waliona kama ni tukio la ajabu sana ambalo boss wao amelifanya.,
Walipomaliza kuwakusanya wale maiti waliwapeleka moja kwa mojahadi kwenye gari moja ambalo lilikuwa limezibwa upande wote na ndani ya hilo gari ni giza totoro ambalo tungefanaisha na gari la kubebea maiti lakini kwa hili lilikuwa likimilikiwana mtu binafsi.

Boss aliita bamboo hebu njoo ili nikupe maelekezo mahali ambako inatakiwa kupeleka hiyo mizoga. Bamboo bila kuchelewa alimfata boss na kupewa maelekezo mahali kwa kupeleka ule mzigo ambao ni watu, baada ya hapo safari ilianza na yule boss wao akawa anarudi sebuleni lakini katika hali ya sinto fahamu akashangaa mlango ambao inatakiwa aingie unafungwa kwa ndani. Alikimbia ili penginepo aweze kuuzuia lakini jitihada zake hata hazikufanikisha jambo lolote lile na badala yake aliuacha ufungwe tuu
Kwa wakati huu boss hapa nyumbani alibaki yeye pekeyake bila hata mlinzi yoyote yule kwahiyo kwakuwa mlango  wa upande mwingine nao aliufunga kwa ndani na kibaya hakuchukua funguo hata moja ikambidi akae tuu pale nje huku akifikilia ni jambo gani atalifanya ili aweze kuingia tena ndani
Alikaa sana masaa yalienda hadi inaaanza kuingia giza hapo ndipo akaona mlango unafunguliwa tena lakini mtu anaefungua hakuweza kumwona. Kwakuwa ni nyumba ya kwake alijisemea hata nikifia kwenye nyuma yangu sio mbaya kuliko nikafia nje huko. Hayo yote alikuwa akiongea huku anaingia ndani ya nyumba ile ambapo ndan ilikuwa giza sana. Alipojaribu kuwasha taa hata moja hakuna taa iliyokubali kuwaka, alijitahidi kubonyeza swichi mara kadhaa lakini hakuna kilicho badilika akaanza kutafutiza simu yake alipoiweka ili ampigie fundi umeme aje arekebishe hadi kuipata simu yake ilichukua nusu saa kwa kuwa ilikuwa ni giza mle ndani hapo ndipo akatafuta jina la fundi umeme ili apige

-/-/-/-/ mteja unaempigia hapatikani kwa sasa tafadhali jabu tena baadae. Thank you for_____hakutaka kusikiliza zaidi. Alikata simu na kutafuta jina jingine la fundi umeme lakini nae majibu yakawa
Mteja unaempigia anaongea na simu nyingine tafadhali jaribu tena baadae alijitahidi kungoja na hatimae simu ikakatwa

_______________________________
Tukiwa katika maeneo fulani ambao ni giza totoro tunamwona ninja fulani akiwa kashika kileo na kukata waya wa nguzo ambayo ilikuwa jirani na mnara kisha akaruka beki tatu mfululizo ambazo zinamfikisha hadi chini na baada ya hapo anaondoka na kuendelea na safari
********************

Wale walinzi baadaya kuondoka walitembea hadi lile eneo ambalo waliambiwa wakatupe zile maiti walifika hadi lile eneo na kutupa zile maiti na kuanza safari ya kurudi ambapo saa zao zilikuwa zikionyesha kwamba ni saa tatu na dakika kumi na tano
Baada ya hapo walianza safari ya kurudi nyumbani ambako ndio kwa yule boss, walifika hadi maeneo fulani gari lilzima na kugoma kabisa kuondoka walipojaribu kuangalia wakagundua kuwa mafuta yamewaishia na hawakuwa na akiba ya dumu hata la lita tano tuu, kwahiyo walichokipanga ni kuomba kama gari likipita waombe msaada wa kufika hadi kituo cha mafuta ili wanunue

______kwa boN________
Baadaya mambo yote niliyoyafanya mchana ambayo ni yale mauzauza ambayo yalikuwa yanatokea kwa boss pale nyumbani kwake nilitafuta hadi sehemu ambayo yeye anatumia kwaajili ya kuweka hela zake na kuchota kiasi fulani cha pesa ambacho kiliniwezesha kupata chumba cha kupanga kilichokuwa mbali kidgo na pale kwa boss.
Usiku niliingia katika kile chumba ili nilale lakini nikagundua kuwa ninanjaa sana kwakuwa hapa palikuwa na watu wengine niligonga mlango mmoja na kumkuta bro mmoja ambae alikuwa na mke wake. Aliponikaribisha niliingia na kuuliza mahali ambapo naweza kupata mgahawa ili nipate angalau hata chakula mana mimi ni mgeni katika mazingira haya.
Yule bro akasema ungeenda kuuliza kwa balozi mana yeye ndiye anaejua mitaa yake yote.,., duuh hili jibu liliniudhi sana nikamwambia poa kaka angu nashukuru kwa jibu lako kwaheli nikawa natoka.
Mke wake ambae alikuwa nae kwa mda huo akasema nenda mtaa wa nyuma huo pana ukuta mmoja unataa kubwa hili mlango wa tatu ndio kuna mgahawa. Nilimshukuru kisha nikawa naondoka huko nyuma
Kwahiyo wewe ndio unajifanya unajua sana kusaidia hawa mafara wanaoingilia mitaa ya watu na kutusumbua.
- hata wewe unaweza ukawa fara kinacho kufanya ushobokee nyumba ya watu ni nini  siujenge ya kwako mi mwanaume mingine bhana sijui ipoje((huku msonyo ukisikika)) yaani wewe kabisa una-___---itaendeleaaaaa

Whi am i

WHO AM I (mimi ni nani)
Benchrys
No. 07

------utalipa dhambi za mwanao kisha akatoa kisu na kutaka amchinje baba lakini kabla hajatimiza lile lengo lake alishitukia mkono wake ukivunjwa asijue ni nani aliye mvunja ule mkono
Kisu kilianguka chini ambapo wale wenzake baada ya kuona vile wakabaki wanashangaa tuu.
Oya tuacheni uboya ivi mwenzetu imemtokea vile halafu nyie bado tu mnashangaa hebu twende. Mmoja wao aliongea yale maneno kisha wote wakaondoka na kufuata pale aliposimama baba lakini kabla hawajafika ulitokea mwanga fulani mkali sana ambapo kila mmoja akajikuta akiziba macho yake ili yasiumie zaidi.
Walipofungua tena macho yao hawakuweza kuona tena kitu machoni pao, kila mmoja wao alibaki na swali ni nini hiki sasa huyu mzee kaenda wapi

-------Tukirudi upande wa pili baba yupo ofisini anacheka tuu na wafanyakazi wenzake hata hana shida yoyote
;;tumeongea mengi ivi nlisahau kusema. Mda ule umeondoka kuna mzee fulani alikuja na kukuulizia wewe(alikuwa akisema sekretari kwa baba kama bosi wake)
---kwahiyo yuko wapi mbona sijamwona
-kiukweli baada ya kumwambia kuwa haupo na umesema yeyote akifika amngoje, yeye alikuwa mbishi sana hadi akataka nimpe namba yako ya simu ila nimekataa
---huyo mtu yupoje labda
- yeye ni____akiwa anataka aendelee kuongea simu yake ilianza kuita akaangalia aliona ni namba ngeni lakini aliipokea vile vile na kuiweka sikioni
Halo,,, hallo,, haloo mbona huongei
Shit labda niweke loud kwanza,. Baadaya kuongea vile akaiweka simu yake iwe loud kisha kaendelea kisikiliza. Hapo ndio ikasikika sauti
++++NASHUKURU SANA DADA KWA MSIMAMO WAKO LAKINI TAMBUA HAPA DUNIANI HAKUNA JAMBO AMBALO HALIWEZEKANI, NAMBA NITAIPATA TUU TENA KWA NAMNA YOYOTE ILE. PIA USISHANGAE HII NAMBA NIMETOA WAPI(kisha akavuta pumzi kidogo lakini iliyokuwa ni ndefu na kuendelea) KAMA UPO NAE HAPO SAIZI NAKUOMBA TUU UMPE SIMU ILI NIONGEE NAE KUHUSU MWANAE AMBAE ANAMTAFUTA++++
Maneno hayo yote baba aliyasikia kisha kaanza kwa kusema ndugu yangu najua ndio lengo uniteke mimi kwa jinsi unavoweza wewe lakini sidhani hilo swala kama litakuwa rahisi kama vile unavodhani jipange kwa jinsi unavoweza sawa kwaheli
(mda wote huo kitufe cha kurekodia kilikuwa kimeshikiliwa tena kiufasaha sana kwahiyo yale maongezi yalihifadhiwa)
Baada ya baba kuongea vile kwenye simu kilisikika kicheko

HAHAHAHAHAHAHAHAHAAAAA, HAHAAAAAA YAANI UNAJITIA MJANJA LEO HUKU HAKUNA UNALOWEZA KULIFANYA. HAYABASI UMESEMA SITAWEZA NI KWELI ILA KESHO UKIFIKA KAZINI HAPO NENDA KATOA SADAKA YOTE BILA KUBAKISHA HATA CHENJI KWAHELI  MKUBWA.

Alisema kwaheli lakini simu haikukatwa zaidi zilianza kusikia sauti za kilio. Hadi pale walibaki wanajiuliza kisha ikarudi sauti tena kwenye simu BABA MIMI BIN USIWE NA WASIWASI NA MIMI SASA HUYU NDIO HATA BAADAE HAIONI PUMBAVU ZAKE. Alimaliza hivo kisha ilisikika sauti ya upanga kama umekata kamba na hapo simu ilikatwa.
Pale ofisini ile siku hata kazi hazikuenda kabisa waliamua kujipa off ya wiki moja wawe nyumbani. Basi waliagana kila mtu na kuelekea kwake yule sekretari akiwa njiani alikuwa akiwaza mambo mengi sana inamaana amekufa au, ila isiwe shida sana sikaya taka yeye mwenyewe.
Akiwa anaendelea kwenda ulisikika mlio wa honi ya gari ambayo ilikuwa tayari ipo miguuni kwake kisha zikafuata sauti za jazba sana kutoka kwa dereva wa lile gari
////ivi wewe dada hii barabara ya baba yako,
Jaman samahani sikuwa naona
///hukuwa unaona. Inamaana kuna ukuta hapa si ndio au
Kakaangu samahani kwakweli mawazo yalikuwa mbali sana na hapa naomba nisamehe tu
/// ivi hii dunia sikuhizi sijui imeingiliwa na pepo gani>>>> oya chogo acha uboya mwache tuu bovu huyo tuna chelewa tu hapa au ushamnoki halafu unafanya kumpandishia acha uboya bhana (yalisikika maneno maneno hayo kutoka kwa mmoja ambaye alikuwa ndani ya gari lile)
Haya maneno inaonekena yalimuudhi sana chogo maana aligeuka na kumtupia jicho yule wa kwenye gari kisha akarudi na kuendelea na safari yao sijui walikuwa wakienda wapi.

______kwa bon au ben_______

Nikiwa nimetulia chumbani kule ambako nilipangiwa kukaa siku zote mara wakaingia watu kama wanne ivi wote wakiwa wameshika magongo na kamba. Wakasogea hadi pale nilipokaa huku wakiangalia huku na kule mwingine akaingia hadi bafuni kisha akatoka na kusema ---oya mbona hakuna mtu humu ndani sijui kaenda wapi---
Hichi kitu nilikishangaa sana hadi nikajiuliza inamaana hawanioni au wanaigiza ili waone nitafanya nini. Wakiwa wanaendelea kujadiliana nilienda hadi mlangoni na kufunga mlango kisha nikarudi kukaa kitandani
Wao baada ya kuangalia zaidi wakawa wanaondoka lakini walipofika kwenye mlango walishangaa kuona umefungwa na wasijue ni nani kaufunga huu mlango wakajikusanya wote ili wauvunje
*****nikiwa nimekaa pale mama alikuja na kunipa mavazi fulani ambayo aliniamrisha nivae kwa haraka yeye anaharaka sana nikafanya hivo, kisha akanipa ule upanga na kuupachika nyuma ya mgongo na kunikabidhi kitu kingine kama koti linalofanana na mavazi yale. Vyote nilivipokea kisha akaniambia ben fuata niliyokuambia yote usiache hata mmoja kati yao sawa. Kisha akanikabidhi kitu kama karatasi na kuniambia leo ndio siku yako ambayo ndio unatakiwa uondoke.
Alipoongea vile nilisimama na kujitazama kwenye kioo nikajiona ni ninja. Alinishika na kusema usishituke chukua na hii uivae kichwani ili kuzuia uso wako usionekane, nilipokea na kuvaa kile kikofia ambacho kiliziba hadi uso mzima kasoro macho tuu. Baada ya hapo mama alipotea nilipotazama niliona dirisha lipo wazi nikasogea na kutaka kuruka====huu ujasiri sijui hata ulitoka wapi

Nilifika kwenye dirisha na kuchumpa sekunde chache nikawa tayari nipo nje kwenye bustani za ile nyumba. Nikiwa nipo chini kabisa kuna walinzi walikuwa wakizunguka katika lile jengo mlinzi mmoja akamshitua mwenzie na kumwambia angalia kule. Yule mwenzie alipogeuka hakuona kitu akampiga mwenzie kofi.
Pumbavu kabisa ushaanza utoto wa kutishiana haya nimeangalia kuna nini ambacho ulikuwa unanionyesha kwenye huko tupo kazini hapa jinga
----hichi kitendo kilimshangaza sana yule mwenzie maana amemwona ninja mda si mrefu kwenye bustani lakini tayari hakuna kitu
Waliachana nayo na kuendelea na kazi yao

Kule chumbani wale wakiwa bado wanahangaika kufungua hatimae wakawa wameweza kuufungua ule mlango na wote wakatoka njee huku wakijua aliye watuma hii kazi ndie amewafungia mlango. Baadaya kutoka hatua ya kwanza walienda jumla hadi kwa boss wao ambapo walimkuta amekaa tuu anakunywa kahawa ule mda kati ya wale mmoja alienda na kumnasa kubao yule boss wake. Boss wake aligeuka kwa hasira na kuchomoa pipe akamtandika nayo kwenye ubongo. Kisha akawaambia na wengine huu mfano na mwingine atafuata nani amewatuma huu ujinga. Wote walibaki wanashangaa tuu alinyanyua tena pipe na kuwatandika wote pale kisha akaita walinzi ili watoa yale maiti-----itaendeleaaaaaaa

Who am i


WHO AM I (mimi ni nani)
Benchrys
No. 06

-------baada ya kusikia lile neno la usimwogope mtu wa humu ndani, nikauliza wewe ni nani unaesema hayo maneno?
Sikujibiwa tena kitu chochote zaidi ya sauti ya ndege ndio zilianza kusikika mle ndani, nilijaribu  kunyanyuka ili niweze angalau hata kwenda msalani lakini mwili ulichoka sana, sikuwa na la kufanya zaidi ya kuendelea kulala lakini nikiwa bado pale kitandani nimejifunika ndani ya blanket nilihisi kitu cha baridi kina tembea. Hapo hata nguvu sijui zilikotoka,
Niliruka juu kama nimepata zawadi katika shindano hiyo yote ni baada ya kugundua kuwa alikuw ni nyoka yupo pale kitandani, nilisimama pembeni huku nikiwa najiuliza huyu nyoka kaingiaje niienda hadi mlangoni ili niweze kupata msaada hata wa kutoka nje lakini baada ya kufika mlangoni mlango ulikuwa umelokiwa kwa nje, mama yangu na huyu nyoka itakuwaje sasa mungu nisaidie (niliongea maneno hayo huku nikiwa nasukuma mlango ule lakini sikuweza kufanikiwa kwa lolote) lakini akili yangu ikanituma kwamba tafuta hata chochote cha kuweza kujihami
Nikageuka tena nyuma ili nipepese hata macho mle ndani pengine naweza ona chochote, baada ya kugeuka nyuma macho yalitua moja kwa moja kwenye kona ya nyumba ambapo niliweza kuona ufagio fulani mrefu kwaajili usafi wa chumba nilinyoosha moja kwa moja ili niuchukue nikafaulu kuuchukua hapo ndipo nikarudi tena kwenye lile blanket ili nimtafute nyoka yule.
Nilivuta lile blanket kwa nguvu huku nikiandaa fimbo yangu lakini cha ajabu sikuweza kumwona nyoka tena pale kwenye kitanda sijui aliondokaje ili eneo basi nikaahirisha na kurudisha ile fimbo tena kuwa ufagio nakuenda kuurudisha mahali ambapo ulikuwepo nikiwa nipo pale kwenye kona nikawa nasikia sauti kwa mbali

Ya ndio hili swala sio gumu sana isipokuwa tu sisi tuwe  makini na akili ya na huyu dogo ni lazima tuu afanye kadiri sisi tunavohitaji
Sawa tutakutuma wewe hapo ili ukaandae mahali pa kumteketezea ili liwe ni swala la kimya kimya sana tuelewane hivyo\\\\\////// wakiwa wanaendelea kuongea khohooo!!!!

Waliposikia sauti hii kila mtu alishtuka. Mmoja akasimama na kuja hadi mlangoni kwangu baada ya mm kugundua kuwa kuna mtu aanakauja jirani na mahali ambapo mimi ndio nilikuwepo niliondoka kwa mwendo wa kunyata tena haraka sana na kuelekea bafuni

Alifungua mlango kisha kaingia ndani, nikiwa bafuni kule niliona nae akija katika mlango wa bafu, nilijibana ili nisionekane lakini alizidi kuingia hadi ndani. Nilipata hasira sana nikamuuliza ndugu ulinzisaizi hadi mtu akiwa bafuni inatakiwa alindwe tu. Hakuongea chochote na kuchomoa kisu fulani katika mfuko wake huku akiendelea kunisogelea, nikajua hapa bila kujitetea naweza kupoteza uhai huku nikiwa najiona.

Baada ya yeye kunisogelea hadi jirani kabisa nilipo, nilijikuta naanguka chini kwa kupigwa ngumi nzito ya taya wakati huo aliye nipiga namuona kama wapo wawiliwawili hivi na kizunguzungu dah nilipata hasira sana. Lakini nae bado alikuwa akinifuata tuu nilipo nami nikaanda ngumi nzito huku mkono wangu ukiwa nyuma ya mgongo, akiwa anaendelea kunifuata kwa mwendo wa taratibu alishitukia akipokea ngumi kama jiwe na kuanguka chini huku akiwa hajielewi kabisa kule bafuni ilikuwa ni damu tuu kwa wakati huo. Baada ya kitendo hicho nilitoka nje huku nikiwa nawaza kama amezirai itakuwaje hapa ndani si pata bana lakini basi nikawa natoka nje ya ile bafu kurudi tena mahali pa kulala mara nikaweza kuiona tena sura ya mama huku akipiga makofi na kusema +++safi sana hivyo ndivyo ambavo nilikuwa nataka kuwa sio watu mnaonelewa na watu kama nyinyi hii dunia ya wote bhana.////alionyesha mwenye furaha sana hadi nikashangaa inamaaana anafahamu kilichotokea nilipotaka kuongea nae gafla tuu akapotea

______kwa baba______________

Baba akiwa kazini kule alipigiwa simu ya kwamba mwanae bon amepatikana katika jumba moja hivi ambalo zamani sana katika historia walikuwa wakiishi watu wan chi nyingine ambao wamekimbia kutokana na matatizo mbalimbali(wakimbizi)

Baba alifurahi sana kupata hizi taarifa akaomba ruhusa pale ofisi kwa wenzake

- jaman naenda mara moja mahala nimepigiwa simu sasa hivi tuu nitakuwa hapa akija mtu mwambie aningoje kisha akaondoka na kupotelea
****alipoondoka tuu kuna mtu akaingia pale

samahani nilikuwa na shida ya kumwona mpl sijui nimemwona
Hapana halafu katoka sasa hivi ila amesema yoyote atakae fika amsubiri hapahapa kwa maana anarudi sasa hivi tuu unaweza ukakaa tuu hapo (alimwambia huku akimwonesha kiti ili akae) lakini yule mgeni akauliza unaeza niambia ameelekea wapi?
Hapana kiufupi hajasema ni wapi ameenda ila wewe msubiri tuu labda kama shidayako sio ya mhimu sana(secretari alijibu tena vile)
Ninaharaka sana basi ningeomba unisaidie hata namba yake ya simu tuu (aliongea yule mgeni)

------hapo sekretari alishituka huyu mgeni kwa nini ni kingang;anizi namna hii hapa kuna kitu sio bure

Kiukweli mimi hapa sina ruhusa ya kutoa namba yake labda angenipa ruhusa ndio ningetoa. Baada ya sekretari kusema vile yule mgeni aliondoka ikiwa inaonyesha kabisa kwamba hajafurahishwa hata kidogona majibu ya sekretari,
Lakini kibaya zaidi yale mazungumzo yao yote kuna sehem maalum ambayo waliiset mnapoongea mkianza na salamu yenyewe inaanza kurekodi, kwahiyo yale mazungumzo yote yalirekodiwa na kile kifaa

****************
Baada ya baba kufika lile eneo ambalo alipigiwa simu kwamba yupo bon alifika pale na kuita lakini palikuwa kimya kama hapaja wahi kukaliwa na kitu chochote chenye kutoa kelele yoyote ile
Bon bon bon
Bon aliita mara kadhaa lakini hakuweza kuitikiwa akaamua arudi tuu kazini lakini alipogeuka nyuma mara moja akakutwa ameshazingirwa na kundi fulani la watu. Baba alibaki ameduwaa asijue ni nini atafanya mara kila mmoja wao akaanza kumsogelea baba hadi pale alipo huku wengine wakiongea lugha isiyo eleweka, na mmoja ndio aliongea Kiswahili
(((((((mzee tuna busara sana lakini kwa kitendo ambacho mwanao amekifanya kwa mwenzetu kwakweli hatuwezi kufumbia macho hata kidogo
(huku akitoa kama sauti ya kulia) amuue ndugu yetu sisi ivi mnajua sisi ni akina nani katika huu ulimwengu nianuwezo wa kukugeuza kitoeo tena kwa kukumaliza m bichi kabisa lakini sitaki
,wakati huo wote baba alikuwa hawaelewi ni nini wanaongea mana kama ni mwanae bon anajua kabisa alipotea katika mazingira ya kutatanisha halafu wao tena wanaongea kuhusu tena.
Yule aliyekuwa akiongea kwa uchungu sana akatoa kisu na kusema hapa naona tunapoteza tuu mda utalipa dhambi za mwanao mzee sawa kisha aka-------itaendeleaaaaaaaa

benchrys.blogspot.com

Who am i

WHO AM I (mimi ni nani)
Benchrys
No. 05

------kwa jinsi alivokuwa akiniangalia nilijua kwamba dhahiri inawezekana tayari ameshaniona na ule upanga ambao nilipewa na mama, lakini cha kushangaza alianza kuongea habari nyingine kabisa licha ya kuwa zilinishtua lakini ilikuwa ni tofauti na ule upanga .

Kijana wangu nimekufata huku mimi kama mimi na hakuna anaejua kuwa mimi mda huu nipo huku nisikilize tena kwa umakini,
Najua nyumbani kwenu mama yako alipotea katika mazingira ambayo hakuna aliyeweza kuelewa ni wapi mahali ambako ameenda, ila itatakiwa utambue kwamba babu yako na bibi yako kipindi kile wamekuja kule kuwasalimia lengo lao haikuwa ni kuwasalimia ila ilikuwa ni kumpoteza mama yako, samahani kwa kukwambia hili( alivuta pumzi kidogo kisha akaendelea) mama yako hadi saizi sio binadamu kama binadamu wengine, unaweza ukabahatika kuonana nae na akakupa chochote cha kujilinda hebu pokea hata usikatae,
Kwa maana, walipogundua kwamba anampenda sana mwanae ambae ndie wewe, walichukua uamuzi wa kukuteka na wewe huku wakitumia uso wa baba yako ambao ulifanya kutengenezwa kama aina fulani ya kofia, nimekuja kukwambia haya kwamaana wewe bado ni mdogo na mambo watakayo taka kukukabidhi sio mema kwa kuishi na wenzio(alisimama na kuanza kuondoka huku akisema) naomba uyashike sana haya maneno kijana wangu.

*****nilishtuka sana pia nikabaki nikijiuliza inamaana huu upanga hauonekani au/////lakini sikukazia sana kuhusu hilo swala
Baada ya dakika chache usingizi ulinipitia

****usiku nikiwa nimelala nilianza kuota*****
+++++++++ hebu nyanyuka acha uzembe wewe utakuja kufa kizembe wewe, sa a awa naanya nyuka, (nilinyanyuka huku nikiwa nimechoka sana lakini huyu hakuwa na huruma kabisa++++haya ruka hizo kamba moja baada ya nyingine tena kwa sekunde ishirini tu ole wako ufeli mana kule chini kuna joka linalokula nyama za watu wazembe, kusikia hivo nilifanya kadiri nilivyoambiwa sijui hata nguvu zilitokea wapi niliruka kambamoja hadi nyingine hadi nikawa tayari nimeshafaulu lile zoezi na kujikuta nipo upande wa pili chini nilipoangalia niliweza kuuona ule upanga ambao nimepewa na mama kule chumbani. Roho ya kuokota sijui hata ilikotokea niliuokota ule upanga na kusimama toka pale chini nikiwa sifahamu lolote.. alitokea kiumbe fulani wa kutisha sana mwenye miguu minne na mkia mrefu mrefu wenye kushiba sana, hapohapo nilianza kuogopa nikasahau kuwa nilishika upanga, kile kiumbe kilianza kunisogelea huku macho yake yakiwa na rangi kama taa inayotoa mwanga mwekundu,
Nilianza kurudi nyuma kwa uoga sana(BON TUMIA HUO UPANGA KUPAMBANA NA HICHO KIUMBE KITAKUTEKETEZA) hii sauti hata sikuelewa ilikotoka lakini ndio ilinikumbusha kuwa nina upanga mkononi

Kile kiumbe kiligeuka kwa kasi ya ajabu na kuuzungusha mkia wake, niljitahidi kuukwepa usinipate lakini jitihada zangu hazikufanikiwa haa kidogo,
Ule mkia ulikita vyema katika mgongo wangu nikajikuta nikirushwa kule huku nikibaki na maumivu makali sana katika mgongo wangu,. Nikiwa bado pale chini nikasikia sauti nyingine tena ikisema UKIFANYA UZEMBE UMEKUFA BEN
Nilinyanyuka tena kwa spidi huku nikiangalia huku na kule kama yule kiumbe anakuja tena lakini niliweza kusikia tua sauti kubwa ya kutisha ukitoka katika pori la upande pili
\\\aghrrrrrrrrrrrrrrrr aghrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr aghrrrrrrrrrrrrrrr
Kwa kusikia hivo nilifahamu dhahiri ni yule kiumbe anataka kuja kwa mara nyingine, na kweli baada ya mda mfupi kilisikika kishindo kikubwa hadi tetemeko kisha yule kiumbe akaokea tena huku anafuka moshi kwenye matundu ya pua lake ambayo usingeweza kutofautisha na shimo la toilet(choo) kwa wakati huu uoga wote niliutupia kule na kujipanga ili nipambanane na huyu kiumbe.
Hili likiumbe lilitoka kasi sana huku likinyoosha kwangu, na mimi kwa ustadi mkubwa niliruka juu kama mita kadhaa huku nikiwa na upanga wangu kisha nikakadiria kwenye jicho moja la yule kiumbe,
Ule upanga ulipoingia tuu katika lile jicho kiumbe hiki kilianguka chini PUUUUU ambako tetemeko lililotokea msitu mzima ilikuwa ni vumbi tuu na baadhi ya miti ilianguka. Nikajua nieshamaliza kazi ya kumuungamiza huyu kiumbe, niliyanyua upanga wangu na kuanza kuondoka,
Lakini kabla sijarusha hata hatua kumi ardhi ilianza kutetemeka upya hadi nikahisi kizunguzungu, nilipogeuka nyuma kile kiumbe kiliamka tena huku macho yakiwaka moto halafu kinanifuata, nilijikuta nikipiga magoti kumwomba mungu anisaidie, kisha nikasimama tena kujiandaa kupambana tena, safari hii ikikuwa kila nikiruka najikuta navutwa chini kinachonivuta hata sielewi,
Lakini nikapata akili nyingine, niliporuka tena nikavutwa chini, nilitanguliza ule upanga nikashangaa kuona upanga hauja fika chini na mimi nikiwa juujuu, hapo nilidank na kutua kwenye mti nikaudaka kama nyani vile kisha nikajirusha hadi mgongoni mwa yule kiumbe, nilivuta pumzi ya kutosha kisha nikauchomeka ule panga mgongoni.
Fuuuuuuuu ni sauti ambayo ilisikika huku vitu kama maji yakitoka mule mgongoni kwa yule kuimbe. Kumbe aliendelea kufumuka mana yale maji yalukuwa ni mengi nikiwa sijakaa vizuri nilirushwa juu******

Nikazinduka kutoka usingizini huku nikiwa nimechoka kuangalia mkono wangu ulikuwa umeshonwa ikionyesha kwamba kuna kitu kiliuchana, kiukkweli nilikuwa na maumivu makali sana katika mwili wote. Nilitaka kuingia bafuni lakini mwili hata kutembea ulipata uvivu maana ulikuwa na maumivu sio mfano yani

Nililala hadi akaja kuniamsha yule baba ambae anatumwa alitumwa mara kwanza aniletee chakula.
Kijana chakula chako hicho(aliongea huku akiwa anasogeza kimeza fulani cha kusukuma jiran na mimi, ilikuwa ni breakfast.
Baada ya kuweka yeye aliondoka nikasikia sauti ikisema hebu kula hakina madhara hicho, mpaka sasa nilishatambua kwamba hii ni sauti ya mama ndie ambae mara zote ananipa taarifa kwa njia ya sauti.
Basi na mimi kwa fujo nilikunywa ile chai kwa haraka sana kwa maana nilikuwa na njaa isitoshe jana nimekataa kula kwa sababu ya mawazo. Dakika tano zilitosha kabisa kumaliza vitafuno vyote mikate mitano na chupa nzima ya chai.
Nilimaliza kula kisha nilianza kujishangaa nawezaje kumaliza chakula chote hiki mimi tuu ila basi nikapotezea na kurudi tena kitandani.
Yule baba alikuja na kutoa vyombo kisha akaondoka alipoondoka tuu mama alitokea, kisha kaniambia pole kwa kazi uliyofanya
Mama kazi gani tena mi nililala mbona
- ulilala angalia huo mkono umeumia kwa sababu gani
Mmmmh mbona hata sielewi halafu nimechoka kweli yani
- ok najua wewe umeona ni kama ndoto lakini hadi sasa uwezo wako wa kupambana ni mkubwa sana, kwahiyo utakaa humu ndani kwa wiki moja ambapo nitakuwa nikifanya mpango wa kukutorosha. Chukua hiki kitabu kina list ya watu wabaya wote wanaohusika na kuupoteza ukoo wetu utaanza na mmoja  baada ya mwingine iweke iwe siri yako tuu. Najua nikigundulika nitatolewa kabisa hata katika hii hali ambayo nipo nayo kwaheli(mama alipotea huku akiwa kaniachia kidaftari fulani kidogo) lakini mara ghafla nikasikia sauti USIMWOGOPE MTU WA HUMU NDANI---itaendeleaaaaaa

benchrys.blogspot.com